EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, November 1, 2012

Mtikisiko CCM Hali imezidi kuwa tete baada ya kuwapo mpango wa kutaka kufuta matokeo ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana (UVCCM) kwa madai kuwa uchaguzi wake ulitawaliwa na rushwa.

MATOKEO UCHAGUZI UVCCM, WAZIRI NAGU KUFUTWA
HALI ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imezidi kuwa tete baada ya kuwapo mpango wa kutaka kufuta matokeo ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana (UVCCM) kwa madai kuwa uchaguzi wake ulitawaliwa na rushwa kupita kiasi.
Mbali ya matokeo ya UVCCM, duru za siasa kutoka ndani ya CCM, zinaeleza kuwa chama hicho pia kimepanga kufuta matokeo ya uchaguzi katika baadhi ya maeneo yaliyolalamikiwa kwa vitendo vya rushwa.

Wilaya ya Hanang ambako kulikuwa na mnyukano mkali kati ya Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk. Mary Nagu, inaelezwa kuwa matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi Dk. Nagu, yanaweza kufutwa.Sumaye ndiye kada wa kwanza wa CCM aliyejitokeza hadharani kulalamikia matumizi ya rushwa ya mtandao kwenye uchaguzi huo ambapo aliangukia pua.
Mkakati wa kutaka kufuta matokeo ya uchaguzi wa UVCCM, unadaiwa kusukwa na mtoto wa kigogo wa chama hicho taifa.Kwa mujibu wa habari hizo, mtoto huyo alimpigia simu mmoja wa wagombea walioshindwa katika nafasi ya mwenyekiti kutoka Zanzibar na kumtaka aje jijini Dar es Salaam kwani Rais Jakaya Kikwete alitaka kuonana naye.

Baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam, kijana huyo alifikia katika Hoteli ya Bondeni na alipotaka kuonana na Rais Kikwete, aliambiwa yupo ziarani mkoani Kilimanjaro na kwamba amemwachia maagizo.Kwa mujibu wa habari hizo, maagizo yanayodaiwa kutoka kwa Rais Kikwete ni kumtaka kijana huyo kuandika barua ya malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa UVCCM ili kuwa na msingi wa hoja ya kutaka kufuta matokeo hayo.
Habari zinaeleza kuwa, kijana huyo aliandika barua hiyo ya malalamiko na kueleza sababu kubwa tatu za kutaka matokeo ya uchaguzi huo yafutwe.
Sababu hizo ni pamoja na kukithiri kwa vitendo vya rushwa ya mtandao, matumizi mabaya ya madaraka ambapo Katibu Mkuu wa UVCCM, Martin Shigela, anadaiwa kutumia nafasi yake vibaya kumsaidia mgombea ashinde.

Habari zinasema kuwa tayari barua hiyo imewasilishwa kwenye sekretarieti ya CCM kwa ajili ya uamuzi.Ukiachia mkakati huo wa kumtumia rais kutaka kufuta matokeo ya uchaguzi wa UVCCM, mkakati mwingine unasukwa na baadhi ya vigogo wa chama hicho ili kuionyesha jamii kwamba CCM imekerwa na rushwa.Mmoja kati ya vigogo wa chama hicho tawala, aliliambia gazeti hili kwamba ili kurejesha heshima ya chama, lazima baadhi ya matokeo ya uchaguzi wa jumuiya za chama na zile za mikoani na wilayani kulikokuwa na malalamiko ya rushwa, yafutwe.“Safari hii rushwa ilitumika vibaya sana kiasi cha kukitia aibu chama chetu. Namna bora ya kurejesha imani hiyo ni kufuta baadhi ya matokeo ya jumuiya, mikoa na wilaya, vinginevyo tutakuwa na wakati mgumu sana,” alisema mtoa habari wetu.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alipoulizwa na gazeti hili endapo barua ya malalamiko kupinga ushindi wa uongozi mpya wa UVCCM, alisema hawezi kukataa wala kukubali kwani hajaiona na sio lazima barua hiyo aione.“Barua zote za malalamiko zinafika kwa Katibu Mkuu. Kwa hiyo kama ameipata kabla hajaleta kwenye vikao, siwezi kujua, “ alisema Nape.Akizungumzia kanuni za chama kuweza kufuta matokeo, Nape alisema hilo linawezekana kama chama kikijiridhisha kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa kanuni za uchaguzi ikiwemo suala la matumizi ya rushwa.

Katika uchaguzi wa UVCCM uliofanyika hivi karibuni mjini Dodoma na kutawaliwa na vitendo vya rushwa, mgombea Sadifa Juma Khamis aliibuka mshindi katika nafasi ya Mwenyekiti wa UVCCM taifa. Nafasi ya Makamu Mwenyekiti ilichukuliwa na Mboni M. Mhita.
Baadhi ya wajumbe waliongia NEC kupitia jumuiya hiyo ni pamoja na Jerry Slaa, Deo Ndegembi, Anthony Mavunde na Jonas Nkya.Mbali ya kudaiwa kushinda kwa rushwa, mwenyekiti huyo mpya tayari ameshakutana na changamoto nyingine kwamba amedanganya umri wake.Habari na 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate