EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 29, 2012

INAKERA VIBAYA SANA SOMA HAPA

KUDAMKA KUPIGA DEKI KWENYE KORIDO WAKATI KUNA WAGENI WAMELALA
NI jambo la ajabu sana, utakuta mwanamke amepata wageni, ndugu wa mumewe wametokea kijijini. Kwa sababu sehemu ya kulala ni finyu, mume anamwambia mkewe watandikiwe kwenye korido ndani walale maana watakaa siku mbili au tatu tu.
Cha ajabu sasa, mke huyo anayeonekana ana busara zake, anadamka saa kumi na moja alfajiri na kuanza kupiga deki hivyo kuwafanya wageni waamke na kwenda kukaa nje kwa sababu ya maji, tena ya baridi maana ni asubuhi. INAKERA SANA.
 
HII NAYO INAKERA
MKE KUULIZWA CHUMBANI, KWENDA KUJIBA SEBULENI
UTAKUTA mke wa mtu yuko na mumewe chmumbani, anamuuliza ‘dear ni kwanini leo chakula kinanuka sana moshi?’ mke badala ya kujibu kulekule chumbani, anatoka kama vile hajamsikia mumewe, akifika sebuleni ndiyo anaanza:
“Si ungepika wewe kama unajua kupika. Moshi moshi, wenzako Somalia wanatafuta chakula hata kinachonuka kinyesi hawakipati, acha hizo.”
Inakera sana, ukizingatia sebuleni anakokwenda kujibia kumepakana na dirisha la nyumba nyingine ya pili!
INAKERA SANA SANA
MGONJWA YU HOI, MHUDUMU MAPOKEZI HANA HILI WALA LILE
Hata Mungu hapendi! Kwamba, mtu anaumwa, ugonjwa wowote ule, hali inakuwa mbaya sana, nduguze wanamkimbiza hospitali.
Kufika mapokezi, mhudumu anaendelea na mambo mengine bila kujali, anatokea mlinzi na kumwonesha ndugu wa mgonjwa mahali pa kuchukua ‘wheel chair’ kwa ajili ya kumbebea mgonjwa wake ambaye amelala kwenye ngazi na kumpeleka kwa daktari.
Hii ilitokea hivi karibuni katika hospitali moja ya wilaya ambapo mlinzi aliyemwonesha wheel chair ndugu wa mgonjwa, alikiri tabia hiyo kuota mizizi mahali hapo. Inakera sana!
 
INGEKUWA VIPI?
INAKERA SANA
WAHUDUMU BAA KUTOKA CHOONI BILA KUNAWA KWA SABUNI
NI jambo ambalo lipo sana, utawaona baadhi ya wahudumu wa baa ‘mabaamedi’ wanaingia chooni na kukaa kwa karibu dakika tano kuashiria kuwa wako kwenye kushusha ‘mzigo mkubwa’, lakini cha ajabu wakitoka hapo hawaonekani kunawa mikono kwa maji na sabuni kama inavyoelekezwa na afya ya jamii.
Mbaya zaidi, wanaendelea kuhudumua wateja, pengine kwa kuwapelekea kongoro, mchemsho au kushika glasi ya kunywea kinywaji. Hii INAKERA SANA!
 -----------------------------------------------------------------------------------------------------
 VYOO VYA HOSPITALI VIKIWA VICHAFU, VYA MTAANI VITAKUWAJE?
Inasumbua sana akili kukuta vyoo vya hospitali eti ndiyo vichafu, havitazamiki, havina maji, uchafu nnjenje, je vya uswahilini vitakuwaje?
     

Utafiti uliofanywa katika baadhi ya hospitali, tena zaidi sana zile za serikali umebainisha kuwa licha ya kuwepo kwa wahudumu kwenye vyoo hivyo, lakini hakuna cha maana kinachofanyika ili kuvifanya viwe visafi.

Kwa mujibu wa mgonjwa mmoja aliyelazwa kwenye hospitali moja ya serikalk iliyopo wilayani Kinondoni, Dar, wahudumu wanaoshughulikia usafi kwenye vyoo hivyo wanapokumbushwa na wagonjwa kuhusu usafi au kuwepo kwa maji huonesha dalili za kukereka kwa kuambiwa huko.

Mbaya zaidi, mganga mkuu wa hospitali hiyo anajua malalamiko ya kuwepo kwa vyoo vichafu, lakini hachukui hatua yoyote na anaendelea kuidhinisha mishahara ya watumishi hao kila mwezi.

Hii ni kero sana tunaomba wahusika mjirekebishe!
 ---------------------------------------------------------------------------------------------------
WANA NINI HAWA MADEREVA WANAOONGEZA FOLENI KWENYE BARABARA MOJA?


Ziko barabara za njia mbili “Two Way”, lakini pia ziko za “One Way”. Mfano barabara ya kutoka Shekilango kwenda Mwenge ni “One Way”. Ina maanisha kwamba gari likiwa limesimama mbele barabarani, dereva wa nyuma hawezi kupita kama mbele kutakuwa na gari linalokuja.


Utakuta magari yapo Sinza Kijiweni foleni ni kubwa sana. Daladala zinakuja kutoka Shekilango na kukuta foleni hiyo. Cha ajabu sana sasa, madereva wa hizi daladala anakuja na kuyapita magari mengine ya mbele yake kwa kuingia njia ya pili ili awahi.


Kinachotokea hapo ni kukutana uso kwa uso na magari yanayotoka Sinza Kumekucha ambayo nayo yatashindwa kwenda mbele kwa sababu ya kuzuiwa na hao madereva vichwa ngumu wasiojua sheria waliokuwa wakitokea Shekilango na hivyo kuifanya foleni kuwa kubwa sana.


Askari wa Usalama Barabarani wangeliangalia hili ikiwezekana kutoa adhabu kali ili hawa wajinga wanaosababisha foleni bila msababu wajifunze.
------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Jamani wengi wetu wanaamini biashara asubuhi jioni ni mahesabu si ndio ee? Unashangaa nini kwani wewe haujawahi sikia kauli hiyo? Usizuge bhana hilo lako na kama si lako basi ni la jirani yako.
Eeh kuna watu wanajifanya akili zao hazina kitu kabsaa sijui wamerogwa! Eti utawakuta asubuhi na mapema muda wa wenzao kufanya biashara wao wanaleta kujuana, me wananikera vibaya mno! Mapema hata chai hawajanywa utawakuta hao wanakwenda kwenye vibanda vya wauza magazeti kwenda kusoma magazeti! 

Makubwa ya jongo! Yaani mwenzio yupo kwenye biashara we unakwenda kuleta Ujinga wako jamani! Kwani uliambiwa yeye anatoa msaada wa magazeti ya bure! Hata haya huna unakwenda  kumzingira kijana wa watu anapojitafutia riziki hii halali kweli? Tena utakuta wamerundikana rundo utadhani wananunua? Mna akili kweli nyie! Inafikia hatua mnunuzi akija anashindwa hata
kununua kwa jinsi mlivyorundikana utadhani pamechinjwa mtu!

Mnanikera mbayaa! Na kama kila mtu atatoka ntumbani kwake na kwenda kusomea hapo kibandani huyo muuzaji atapata riziki yake kweli! Na ile kauli ya biashara asubuhi jioni mahesabu italeta maana kweli! Maana jioni hatokuwa na mahesabu! Ahesabu nini wakati wanunuzi mmejisomea palepale tena kitu free bila ushuru wala bhugudha! Na hao wanaozalisha hayo magazeti si ndio maana wengi biashara inawashinda! 
Wasifunge mchezo, wabongo wanapenda free utadhani maiti kha!  Ebu kuweni wastaarabu bhana fanya kazi upate ela yako ununue gazeti usome kwa raha zako! Najua hapo mmenuna si limewagusa teh teh mtalinywa tu hata kama chungu si ndiyo dawa jamani! Haya nisameheni lakini meseji send kama hautaki we mbishi! Km hautaki kadeki bahari ciao

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate