KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya 
Morogoro, limewataka wanawake wanaokwenda kufunga ndoa katika kanisa 
hilo kuacha kuvaa mavazi yanayoonyesha maungo yao hususan matiti na 
migongo ili kuepuka kuwakwaza wachungaji.
Akihubiri wakati wa misa maalumu ya harambee ya kuchangia ujenzi wa 
kanisa hilo usharika wa Kilakala iliyoongozwa na Waziri Mkuu 
aliyejiuzulu, Edward Lowassa, msaidizi wa Askofu katika dayosisi 
hiyo, George Pindua, alisema kuwa baadhi ya wanawake wanaokwenda kufunga
 ndoa huvaa nguo zisizo na heshima.
“Nyie wanaume ambao mmepanga kufunga ndoa na wake zenu hakikisheni 
mnawanunulia nguo zenye heshima, atakayekuja na nguo zinazoonyesha 
matiti au mgongo hatutamfungisha ndoa,’’ alisema.
Alisema kuwa kina mama wa kanisa hilo wanapaswa kuandaa vitenge vya 
kuwafunika wanawake wanaovaa nguo zisizo na maadili ili kuepusha kanisa 
kupata aibu.
  Naye Askofu wa KKKT Dayosisi ya Morogoro, Jacob ole Mameo, alisema 
kuwa wamekuwa wakitoa mahubiri mema ili kuhakikisha waumini wao 
wanadumisha amani na utulivu.
  Alisema kuwa taifa hili limejengwa katika misingi ya kudumisha amani na utulivu hivyo kila muumini anapaswa kuilinda isipotee.
 
 
 
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment