EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 29, 2013

Chadema yagawa nchi mapande 10

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeibuka na mkakati mpya wa kushika hatamu za dola katika uchaguzi, baada ya kutangaza kufanya mabadiliko makubwa ya uongozi na utendaji wake kwa kupeleka mamlaka ya makao makuu ya chama kwenye kanda 10; nane zikiundwa Tanzania Bara na mbili visiwani Zanzibar.

Mkakati huo, ambao ni sehemu ya utekeyake ya majimbo, ulitangazwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, alipofungua mkutano wa dharura wa Baraza Kuu la Chama hicho, jijini Dar es Salaam jana, ulioitishwa kwa lengo la kujadili mikakakti ya uendeshaji wa shughuli za chama kwa ajili ya mustakabali wa chama.

Alisema uamuzi huo umefikiwa ili kuondokana na mazoea yaliyopo serikalini ya kung’ang’ania kila kitu kufanywa na kikundi cha watu wachache jijini Dar es Salaam.
Alisema Chadema imeamua kuuvunja mwiko huo kwa kuwa ni chama, ambacho kinathaminiwa na Watanzania wote, hivyo akawataka wanaChadema kuishi kwa kauli zao.

“Kwa hiyo, madaraka ya chama yanatoka makao makuu sasa yanakwenda kwenye kanda. Chama kimekua. Ukienda kila mkoa kipo. Hatuwezi kung’ang’ania Dar es Salaam tu. Chama sasa kipelekwe kwenye kanda zenu,” alisema Mbowe na kuongeza:

“Baada ya kazi kubwa iliyofanywa na makao makuu (ya Chadema) kwa miaka 20, lazima kama chama siasa tujipange kama dola. Tunakwenda kutawanya chama kwenye kanda 10. Tunakwenda na vikosi 10. Tutapeleka magari, pikipiki.”

Alisema kazi ya kuchukua dola si ya Mbowe wala ya (Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tanzania Bara, Said) Arfi) peke yake, bali ni ya wote.

Alizitaja kanda hizo kuwa ni Ziwa Magharibi, ambayo itahusisha mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera); Kanda ya Ziwa Mashariki (Mara, Simiyu na Shinyanga) na Kanda Magharibi (Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa).

Kanda nyingine ni ya Kati (Singida, Dodoma na Morogoro); Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Iringa, Njombe, Mbeya na Ruvuma); Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara) na Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam na Pwani). Nyingine ni Kanda ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara); Kanda ya Pemba (mikoa yote ya Pemba) na Kanda ya Unguja (mikoa yote ya Unguja).

Alisema katika kila kanda kutakuwa na ofisi na kwamba, chama kitagawa vitendea kazi vyote muhimu, yakiwamo magari na pikipiki ili kurahisisha na kufanikisha shughuli za chama.

Mbowe alisema kila kanda ina maofisa wenye uzoefu wa kukisimamia chama na zitajumuisha pia wabunge wa maeneo husika. Alisema wamefikia uamuzi huo ili kukataa malalamiko, ambayo yamekuwa yakitolewa muda mrefu kuhusu kila kitu kufanywa na makao makuu ndiyo maana wameamua kuyashusha chini mamlaka yake.

Mbowe alisema sababu nyingine, ni kujipanga kwa ajili ya uchaguzi, kuanzia ule mdogo wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji na uchaguzi mkuu na pia kudhibiti wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupita bila kupingwa katika uchaguzi.

“Tatizo kubwa la nchi hii ni watu kukaa makao makuu wakifikiri kuwa wanajua kuliko wote, wanajua mali kuliko wengine,” alisema Mbowe.

Alisema yanayotokea mkoani Mtwara ni mwanzo unaoashiria kwamba, wananchi hawana imani na serikali na kusema jambo hilo la kujisifu, lakini linastahili kupongezwa kutokana na ujasiri unaoonyeshwa na wananchi wa mkoa huo.

Mbowe alisema msimamo wa Chadema kuhusu gesi ya Mtwara, iko pamoja na wananchi.
 “Kama CCM wanafikiri ngoma imeishia Mtwara wangoje, kama ni noma na iwe noma. Wajiandae kutoa majibu kuhusu dhahabu, mafuta, uranium, twiga, pembe za ndovu na rasilimali za nchi,” alisema Mbowe.

Aliitaka serikali kusitisha mara moja mpango wa kuisafirisha gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salam hadi hapo itakapokaa na wananchi, wajadili, waridhie na suala hilo lifanyike kwa maslahi ya wote.

Aliitaka pia serikali kuiweka hadharani mikataba yote 26 ya gesi.
Alisema Chadema hawawachukii wawekezaji, lakini wanachohitaji ni wananchi na wawekezaji kila mmoja kufaidi rasilimali za nchi.

Mbowe alisema watu, ambao Chadema ina ugomvi nao ni viongozi waliofungua milango na kuruhusu wawekezaji wasiokuwa na uwezo kuja kuwekeza nchini.

Kuhusu Katiba aliitahadharisha Tume ya Mabadiliko ya Katiba na serikali akisema kama wanajidanganya kuwa watakuja kuwapandikizia katiba wanayoitaka, nchini  “hapatatosha”.
“Kama haitakuwa na maslahi ya Watanzania tunaikataa.  Kuandika katiba ni jambo jepesi, bali kuiridhia,” alisema Mbowe.

Alisema katiba ina maeneo mengi yanayohitaji kurekebishwa na kuonya kuwa iwapo watayafanyia maskhara hawataikubali na watakwenda kuwahamasisha wananchi ili waungane nao kuikataa.

Mbowe alisema Watanzania hawawezi kuwa na serikali mbili katika mfumo wa sasa na kupendekeza kuwa Wazanzibari wapewe uhuru wao, ikiwa ni pamoja na kutekeleza matakwa ya kuwapo pia na serikali ya Tanganyika.

Kuhusu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), alisema kama CCM wanafikiri Chadema watakubali kuingia kwenye uchaguzi na tume iliyopo, “basi wameula wa chuya, hatukubali.”

Alisema kadiri Chadema inavyokua ndivyo maadui nao wanavyozidi kukua, huku zikitumika mbinu chafu za kuwagawa viongozi na ‘kuwanunua’ wabunge wake.

Hata hivyo, alionya kuwa hawatasita kuwachukulia hatua za kinidhamu watu wanaotaka kuwavuruga na kusisitiza kuwa: “Tutakula nao sahani moja.”

Naye Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alisema ni upotofu kufikiri kwamba, mpango wa Chadema wa kwenda kuhoji namna rasilimali za nchi, kama vile dhahabu, uranium, twiga na meno ya tembo, zinavyotumika, ni uchochezi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate