EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 29, 2013

Kinana: Serikali iwasikilize wananchi wa Mtwara

SAKATA la gesi sasa limeingia hatua mpya, baada ya watendaji wakuu wa CCM; Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kuitaka Serikali ikae na wana-Mtwara ili kuona namna ya kumaliza mgogoro huo kwa amani.
 
Kinana na Nape walitoa kauli hizo kwa nyakati tofauti jana. Wakati Kinana alisema hayo alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara mkoani Kigoma, Nape alifanya hivyo kupitia mtandaowa Twitter na baadaye kuthibitisha kauli hiyo alipoulizwa na mwandishi wetu.

Wakati watendaji hao wa CCM wakitoa matamko hayo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana alifanya vikao mfululizo mkoani Mtwara akisaka suluhu ya mgogoro huo.

Kinana na Nape
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Ofisi za CCM Wilaya ya Uvinza, Kigoma, Kinana aliitaka Serikali isikilize hoja za wakazi wa Mtwara na kuzitafutia usumbufu sahihi.

Mbali na kutoa ushauri huo, aliitaka pia Serikali kuwasaka watu wanaochochea mgogoro huo kwa kufanya vurugu na kuharibu mali za watu na kuwafikisha mbele ya sheria.
“Serikali ikae na wana-Mtwara na kuwasikiliza, wananchi hao wana hoja na Serikali inapaswa kutoa majibu sahihi kwa hoja hizo. Lakini pia iwasake na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha uvunjifu wa amani,” alisema Kinana.

Kwa upande wake, Nnauye aliitaka Serikali kuwasikiliza wananchi wa Mtwara kwa kuwa madai yao ni ya msingi... “Wakazi wa Mtwara na Lindi wanazo hoja za msingi juu ya suala la gesi, hoja ambazo ni muhimu kusikilizwa na kupatiwa majibu sahihi.”

Nape alisema hoja za wakazi hao ni za msingi lakini akaongeza kuwa kuna baadhi ya wahuni ambao wanatumia mwanya huo kupora na kuharibu mali za watu. “Kuna uhusiano gani kati ya hoja yao ya madai ya gesi na kuchoma nyumba za watu, kuharibu mali za umma na magari ya watu. Kuna kundi la wahuni ambalo Serikali inatakiwa kuhakikisha inapambana nalo na kuwachukulia hatua kali za kisheria,” alisema Nape.

Pinda asaka suluhu
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana alikuwa na kibarua kizito kusaka suluhu ya mgogoro wa gesi baada ya kuzungumza na makundi mbalimbali ya kijamii kupata mawazo yao.

Pinda aliyeongozana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja alianza kazi hiyo juzi kwa kufanya vikao vya ndani na viongozi wa Serikali mkoa wa Mtwara. Habari kutoka Mtwara zinaeleza kuwa kutwa nzima ya jana, Waziri Mkuu Pinda alikuwa akifanya mikutano mbalimbali na makundi kadhaa kwa lengo la kupata suluhu ya mgogoro huo wa gesi.

“Alianza kwa kufanya mazungumzo ya ndani na viongozi wa dini, wanaharakati, wanasiasa na baadaye viongozi wa Serikali za Mitaa,” kilieleza chanzo cha habari kutoka Mtwara.
Mbali na viongozi hao, Pinda pia alizungumza na wafanyabiashara, viongozi wa CCM na madiwani kabla ya mkutano wake na waandishi wa habari aliopanga kuufanya baadaye jioni.
Mmoja wa madiwani waliohudhuria mkutano huo wa Pinda alilieleza gazeti hili kuwa, Waziri Mkuu aliwaambia kuwa mkutano wake huo ni kwa ajili ya kukusanya maoni.

“Amesema amekuja kukusanya maoni na baadaye atakwenda kushauriana na Rais Jakaya Kikwete na atatoa tamko kuhusu hatima ya suala hilo baadaye,” alisema diwani huyo akimnukuu Waziri Mkuu Pinda.

Gesi kuteka Bunge
Mkutano wa Kumi wa Bunge unaanza leo mjini Dodoma, huku suala la gesi likitarajiwa kutawala mijadala mbalimbali ya wabunge.

 Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Habib Mnyaa ni miongoni mwa wabunge waliotangaza mapema kuwa watazungumzia suala hilo bungeni. Mnyaa alisema anakusudia kuwasilisha hoja binafsi za maombi ya wakazi wa Mtwara kupinga gesi kupelekwa Dar es Salaam.

Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Mawasiliano ya Bunge, Deogratius Igidio aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa shughuli zote zitakazofanyika ndani ya ukumbi huo zitajulikana leo baada ya Kikao cha Kamati ya Uongozi.Katika kipindi cha wiki nne sasa kumekuwa na maandamano, malumbano na vitendo vya ghasia kuhusiana na mradi wa kujenga bomba la kusafirishia gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam hatua ambayo inapingwa na wananchi wa eneo hilo ambao wanadai kuwa wamesahauliwa katika miradi ya maendeleo.

Wananchi hao wa Mtwara wanataka kusitishwa kwa mpango wa kusafirisha gesi hiyo kwa madai kuwa, eneo la Mtwara halijaendelezwa na mara zote Serikali haijaweka vipaumbele kwa ajili ya kusukuma mbele eneo hilo.

Wanataka uendelezwaji wa gesi hiyo ufanywe mkoani humo kwa madai kuwa utasaidia kuchochea shughuli za maendeleo na kuufanya uanze kuinuka kiuchumi.

Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa ambaye pia ni mwenyeji wa mkoa huo ametoa wito wa pande zote kukutana na kujadiliana ili kumaliza mvutano huo akisema ni jambo la kufedhehesha na kusikitisha kuona wananchi wakianzisha maandamano na kupinga mradi huo wa Serikali.

Chadema hakitaki
Chadema kimeitaka Serikali kusitisha mpango wa kusafirisha gesi iliyogunduliwa mkoani Mtwara kwenda Dar es Salaam mpaka itakapokutana na wananchi na kufikia maridhiano kwa pamoja.

Chama hicho pia kimeitaka Serikali iweke wazi mikataba yote 26 ya kampuni ilizoingia nayo kwa ajili ya kuchimba nishati hiyo ili wananchi waweze kuijua.

Mwenyekiti Freeman Mbowe alitoa wito huo jana alipokuwa akifungua mkutano wa siku moja wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam... “Kwa muda mrefu watu wamekuwa wakiuliza Chadema nini kauli yenu kuhusu mgogoro huo na kutaka kujua tuko na wananchi au Serikali? Chadema iko nyuma ya wananchi,” alisema Mbowe na kuongeza:

“Serikali iache kufanya kazi ikiwa Dar es Salaam iende kwa wananchi na kuzungumza nao na wakikubaliana kwa pamoja ndipo mradi huo utekelezwe.”
Habari hii imeandikwa na Raymond Kaminyoge, Kigoma; Ibrahim Yamola, Dar na Habel Chidawali na Ibrahim Bakari, Dodoma.
                                                            Chanzo Mwananchi

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate