EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 26, 2013

CCM wadhalilishana Bukoba..Wamsusia meya, watuma ujumbe mzito kwa Mangula

CHAMA cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Bukoba Mjini, kimeingia katika siasa chafu za kudhalilishana huku vipeperushi vya kuwatusi madiwani 10 wa chama hicho na wale wa Chama cha Wananchi (CUF) vikisambazwa mitaani.

Madiwani hao waliochafuliwa kwa matusi mazito ya nguoni ambayo mengine hayaandikiki kwa kuzingatia maadili ni wale nane wa CCM akiwemo Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki, na wawili wa CUF waliosaini hati ya kumtaka mkurugenzi wa manispaa hiyo kuitisha kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani ili kumng’oa Meya Anatory Amani anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi.

Hatua hiyo inakuja siku chache tangu Dk. Amani aamue kupuuza maagizo ya Makamu Mwenyekiti wao chama hicho taifa, Philip Mangula, kwa kufungua kesi mahakamani kupinga kujadiliwa na kung’olewa na madiwani.
Mangula ambaye alilazimika kufika mjini Bukoba mwezi uliopita ili kunusuru mtafaruku huo, aliagiza madiwani nane wa CCM waliokuwa wamesaini hati hiyo, waondoe tuhuma hizo na kuzipeleka kwenye chama ili zipatiwe ufumbuzi.

Lakini katika hatua ambayo imetafsiriwa kuwa mgogoro huo unazidi kushika kasi, juzi vipeperushi hivyo vya matusi vilisambazwa na watu wasiojulikana kwa kuvibandika katika maeneo mbalimbali ya mji wa Bukoba.
Madiwani waliosaini hati ya kutaka kuitishwa kikao cha kumng’oa meya huyo mbali na Kagasheki ni Naibu wake, Alexander Ngalinda (Kata ya Buhende) na Yusuf Ngaiza (Kashai) ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Manispaa ya Bukoba.

Wengine ni Richard Gasper (Miembeni), Dauda Kalumuna (Ijuganyondo), Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi (Hamugembe) na Mulubi Kichwabuta (Viti Maalumu) na wale wa CUF ni Ibrahim Mabruk (Bilele) na Rabia Badru wa Viti Maalum.
Taarifa kutoka mjini Bukoba zilisema kuwa madiwani hao nane wa CCM, jana waliandika barua ya malalamiko kwenda kwa katibu wa chama hicho wilaya na nakala zake kwa mwenyekiti wa mkoa, mkuu wa mkoa na Mangula.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, barua hiyo ambayo ilikabidhiwa asubuhi wamekataa kushiriki vikao vyovyote vitakavyoongozwa na Meya Amani wakimtuhumu kuwa ndiye alihusika kusambaza vipeperushi hivyo vya kuwakashfu.
“Na katika kutimiza msimamo wetu, tayari madiwani wote nane wa CCM leo tumesusia kikao cha meya kilichojadili maandanlizi ya Baraza la Madiwani.
“Na kwa mujibu wa kanuni baada ya kukataa idadi ilikuwa haimruhusu kwendelea na kikao kwani wajumbe tuko 17 lakini alibaki na saba ambao ni pungufu,” alisema mmoja wa madiwani hao.

Katika vipeperushi hivyo, madiwani hao kila mmoja ametajwa kwa jina lake, kata na orodha ya tuhuma zake huku wengine wakidaiwa kulaghaiwa kwa fedha na mmoja wa viti maalum akidhalilishwa kwa tuhuma za ngono.
Mgogoro wa Bukoba mjini umekuwa na muda mrefu sasa na Meya Amani katika kujihami ili asing’olewe, kwa kushirikiana na mkurugenzi wake, Hamis Kaputa, walilazimika kuahirisha kikao cha Baraza la Madiwani kinyume na kanuni.

Kwa mujibu wa sheria namba 8 ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1982 kifungu namba 7 (1), mkurugenzi anapaswa kumwandikia barua kila mjumbe kumweleza mahali na siku vikao vitapofanyika na ajenda zitakazojadiliwa siku saba kabla ya kikao.
Madiwani hao hawakuwahi kujulishwa uwepo wa kikao hicho walichotaarifiwa na mkurugenzi kuwa kimesogezwa mbele kama kanuni hizo zinavyosema.
Kikao hicho kilikuwa cha kujadili utekelezaji wa shughuli za robo mwaka za fedha kati ya Oktoba hadi Desemba 30 mwaka jana, na kwa mujibu wa sheria kilipaswa kufanyika si zaidi ya Januari mwaka huu.

Katika barua hiyo yenye kumb. Na BMC/C.50/5/13, inayosomeka ‘Yah: Kusogezwa mbele ratiba ya vikao vya Baraza la Madiwani’, Kaputa hata hivyo haonyeshi ni lini kikao hicho kitakaa.
Kaputa, katika barua hiyo anadai kuwa baraza haliwezi kufanyika kutokana na wakuu wa idara wengi kuwa safarini kuelekea jijini Dar es Salaam kwa ajili ya vikao vya bajeti 2013/2014.
Amani ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kagondo, aliamua kwenda mbali zaidi huku akikiuka kanuni na sheria ambapo sasa amefungua pingamizi mahakamani ili kuzuia mkurugenzi asiitishe kikao chochote cha kujadili tuhuma zake kwa muda wote atakaokuwa katika wadhifa wake.VIA TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate