EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 28, 2013

Meya CCM Bukoba atoswa

MGOGORO ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bukoba Mjini, unazidi kuchukua sura mpya baada ya madiwani wake tisa kuungana na wenzao wawili wa Chama cha Wananchi (CUF) na wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukwamisha kikao cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kiketi jana kujadili bajeti ya 2014/2014.
Hatua hiyo inakuja siku moja baada ya madiwani 10 wa Halmashauri ya Mji wa Bukoba akiwemo Mbunge wa jimbo hilo, Balozi Khamis Kagesheki kutukanwa matusi ya nguoni kupitia vipeperushi vilivyosambazwa mjini humo na watu wasiojulikana.

Madiwani waliotukanwa matusi hayo mazito ni nane wa CCM na wawili wa CUF waliosaini hati ya kumtaka mkurugenzi wa manispaa hiyo kuitisha kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani ili kumng’oa Meya Anatory Amani anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi.
Halmashauri hiyo ina madiwani 24, watatu wa CUF, wanne wa CHADEMA na 17 wa CCM. Ili kikao cha baraza kiweze kuendelea ni lazima akidi ya mahudhurio iwe na nusu ya wajumbe jambo ambalo lilishindikana jana.

Wakizungumza kutoka mjini Bukoba, baadhi ya madiwani walisema kuwa Meya Amani ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kagondo, alipata wakati mgumu hadi kulazimika kukiahirisha kikao hicho.
Kwamba muda wa kuanza kikao ulipowadia, ukumbini walikuwemo wajumbe 11, yaani madiwani nane wa CCM, wawili wa CHADEMA na mmoja wa CUF, jambo lililomlazimu meya huyo kuwapigia simu baadhi ya wale ambao walikuwa hawajafika na kuwashawishi bila mafanikio.

“Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Zipora Pangani naye aliingilia kati kumsaidia meya kiasi cha kufikia hatua ya kuwapigia simu madiwani hao, kila mmoja akimbembeleza ataje mahali alipo ili amtumie gari imchukue au kitabu cha mahudhurio asaini huko aliko, lakini ilishindikana,” alisema mmoja wa madiwani.
Habari zaidi zinasema kuwa, Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera naye aliingilia kati kwa 

kumwagiza katibu wa wilaya awatafute madiwani wa chama hicho ambao hawakuwa ukumbini, lakini haikuwezekana kwani simu zao zilikuwa zimefungwa.
Baada ya kuona hali inakuwa tete, Meya Amani alikiahirisha kikao kwa muda hadi saa 6:30 mchana ingawa hali iliendelea kubakia vile vile, na hivyo ukafikia uamuzi wa kusitisha baraza hilo hadi Machi 1 na 2 mwaka huu.

Akiahirisha kikao hicho, Meya Amani kwa hasira alisema kuwa madiwani hao waliokwepa wanapaswa kupigwa mawe na kulaaniwa kwa kukwamisha maendeleo ya wananchi.
Hata hivyo, tarehe hizo zilizopangwa kufanyika baraza hilo zimezua utata kwani zilishapangiwa shughuli nyingine ya vikao vya kujadili utekelezaji wa bajeti ya robo mwaka ya pili ya 2012/2013.

Ni dhahiri kuwa mgogoro huo unazidi kukimega chama kwani Meya Amani kwa upande mwingine amepuuza maagizo ya Makamu Mwenyekiti CCM Taifa, Philip Mangula kwa kuamua kufungua kesi mahakamani kupinga kujadiliwa na kung’olewa na madiwani.
Mangula ambaye alilazimika kufika mjini Bukoba mwezi uliopita ili kunusuru mtafaruku huo, aliagiza madiwani nane wa CCM waliokuwa wamesaini hati hiyo, waondoe tuhuma hizo na kuzipeleka kwenye chama ili zipatiwe ufumbuzi.

Madiwani waliosaini hati ya kutaka kuitishwa kikao cha kumng’oa meya huyo mbali na Kagasheki ni Naibu wake, Alexander Ngalinda (Kata ya Buhende) na Yusuf Ngaiza (Kashai) ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Manispaa ya Bukoba.

Wengine ni Richard Gasper (Miembeni), Dauda Kalumuna (Ijuganyondo), Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi (Hamugembe) na Mulubi Kichwabuta (Viti Maalumu) na wale wa CUF ni Ibrahim Mabruk (Bilele) na Rabia Badru wa Viti Maalumu.
Taarifa kutoka mjini Bukoba zilisema kuwa madiwani hao nane wa CCM, jana waliandika barua ya malalamiko kwenda kwa katibu wa chama hicho wilaya na nakala zake kwa Mwenyekiti wa Mkoa, Mkuu wa Mkoa na Mangula.

Juzi, madiwani nane wa CCM walikabidhi barua kwa Katibu wa Wilaya wakipinga kushiriki vikao vyote vitakavyoongozwa na Meya Amani wakimtuhumu kuwa ndiye alihusika kusambaza vipeperushi vya kuwakashifu.
Katika vipeperushi hivyo, madiwani hao kila mmoja alitajwa kwa jina lake, kata na orodha ya tuhuma zake huku wengine wakidaiwa kulaghaiwa kwa fedha na mmoja wa viti maalumu akidhalilishwa kwa tuhuma za ngono.

Balozi Kagasheki ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii pamoja na madiwani wenzake kadhaa wa CCM, waliwasilisha barua zao kwa mkurugenzi ili kuondoa tuhuma zao kwa muda asubuhi ya Januari 23 mwaka huu, lakini mchana wa siku hiyo Meya Amani akafungua kesi ya kupinga asijadiliwe.
Mangula aliwataka madiwani hao kuunda kamati ya kushughulikia mgogoro huo chini ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fabian Massawe ingawa mkuu huyo pamoja na Pangani, Mwenyekiti na Katibu wa CCM mkoa wanadaiwa kumkingia kifua Amani.
Madiwani hao wanapinga mikataba ya miradi mikubwa miwili ya uuzwaji wa viwanja zaidi ya 5,000 na ujenzi wa soko la kisasa wakidai imasainiwa kifisadi kwa siri na Meya Amani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate