EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 23, 2013

Obama, JK, Ridhiwan watumika kutapeli Dar

WAKATI watanzania wengi hawajasahau machungu ya kulizwa na kampuni ya kupanda na kuvuna mbegu ya DECI, kumeibuka taasisi mpya ya fedha inayojitapa kutoa mikopo kwa njia ya mtandao, huku ikitumia vibaya majina ya Rais Jakaya Kikwete na Barack Obama wa Marekani.

Mbali ya taasisi hiyo ya Tanzania Loans Society kutumia majina ya marais hao, imewahusisha pia Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Ridhiwani Kikwete, ambapo inahofiwa kutapeli mamilioni ya walalahoi.

Taarifa za taasisi hiyo zinaonesha kuwa ilianza shughuli zake mwaka 2012, na kupata ufadhili wa fedha kutoka kwa Rais Obama, ambapo inasimamiwa na Rais Kikwete, Waziri Mkuu Pinda na mratibu mkuu ni Ridhiwani.
Watendaji wengine ni Michael John ambaye namba yake ya simu ya mkononi ndiyo inayotumika kutuma pesa za usajili.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa taasisi hiyo, imekuwa ikijitangaza kutoa huduma ya mikopo na mawasiliano ya jinsi ya kupata mikopo hiyo, hufanyika kwa njia ya mtandao ili kuwawezesha wateja wa mikoani kupata mikopo hiyo kirahisi bila usumbufu wa kuja makao makuu yao jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wananchi walioomba kupata mikopo hiyo, waliliambia gazeti hili kuwa, fomu za mikopo ya taasisi hiyo hutolewa kwa sh 15,000 ambazo nazo hulipiwa kwa njia ya mtandao.
Mmoja wa wateja wa taasisi hiyo aliyedai kutapeliwa, Maywood Maganga alisema alionja machungu baada ya kuingia kwenye tovuti yake na kukutana na maelekezo ya kumtaka ajaze fomu na taarifa zake binafsi na kisha kutakiwa kutuma sh 15,000 kwenda kwenye namba 0656 73 64 16, iliyosajiliwa kwa jina la Michael John.
Maganga alisema kuwa alifanya hivyo, na kusubiri majibu.

Kwa mujibu wa mkopo huo wenye masharti nafuu, tena usio na riba, mteja hutakiwa kurejesha na kuanza kukatwa baada ya miezi miwili tangu siku ya kupokea pesa hizo za mkopo.
“Maelezo ya mkopo huo yanaonesha kuwa una masharti nafuu sana na marejesho yake ni sh 60,000 kila mwezi bila kujali kiasi ambacho mteja amekopa.
“Maelezo ya fomu niliyojaza yalinionesha kwamba nitapata sh 300,000 kama zawadi kwa kukubali kukopa na baada ya dakika 30, ningeingiziwa kiasi cha fedha za mkopo nilizoomba,” alisema.

Kwa mujibu wa Maganga, fomu alizozikuta kwenye tovuti ya taasisi hiyo, zilionesha mahala ofisi ilipo, lakini alipofuatilia na kuuliza, alibaini kuwa taasisi hiyo haina ofisi katika jengo la serikali la Utumishi wa Umma.

“Mwanzoni sikuwaza kama taasisi hii itakuwa ya kitapeli, lakini baada ya siku mbili ya kutokutumiwa pesa hiyo ndipo nilipogundua kwamba nimetapeliwa,” aliksema.
Maganga aliziomba mamlaka husika kuingilia kati kwa kudhibiti utapeli huo, kwani Watanzania wengi wameshalizwa kupitia taasisi hiyo inayotumia majina ya watu maarufu kutapeli.

Aidha, maelezo ya tovuti hiyo yanaeleza zaidi kuwa kwa kutambua ugumu wa maisha uliopo kwa Watanzania na kukua kwa teknolojia kama nchi zingine zifanyavyo, taasisi hiyo inatoa mikopo kwa njia hiyo ya mtandaao ili kuepuka usumbufu wa kuwafikia watu walioko mikoani ili nao wanufaike.

Mbali ya hayo, pia taarifa ya maelezo ya taasisi hiyo hiyo ilieleza kuwa kiwango cha chini cha kupata mkopo ni sh 100,000 na ofisi zake zipo katika jengo la utumishi wa umma, ghorofa ya tano chumba namba 30.
Ridhiwani hakuweza kupatikana kuzungumzia taasisi hiyo, lakini katika taarifa aliyoituma hivi karibuni kwenye ukurasa wake wa facebook, alikanusha yeye na viongozi wa serikali akiwemo Rais Kikwete kuhusika na taasisi hiyo.

“Maisha ni kuhangaika na kwamba inataka mtu anayefahamu njia sahihi kuweza kujua kuwa nikitumia njia hii hali itakuwa sawa na pengine mambo yangu yatanyooka.
“Hii inaweza kuwa ndiyo maana halisi ya kuhangaika ufanikiwe, lakini tafsiri hii haiwezi kuwa kutumia njia za kudhulumu, kukaba, kuiba au kufanya utapeli ili ufanikishe malengo yako mabaya dhidi ya mtu au kikundi fulani cha watu," aliandika Ridhiwani kwenye ukurasa wake wa facebook.

Kwa mujibu wa Ridhiwani, hivi karibuni alipokea ujumbe mfupi wa maandishi kupitia simu yake ya mkononi na barua pepe, ikihoji kuhusika kwake na kampuni hiyo.
Alisema mradi huo unadaiwa kuanzia katika mikono ya Rais Obama kuja Tanzania kupitia Kikwete na sasa yeye akishirikiana na Waziri Mkuu Pinda wanauendesha.
“Jambo hili si la ukweli hata kidogo, na naomba kutumia nafasi hii kulikanusha kabisa mbele ya umma wa Watanzania na wale wote ambao kwa namna moja au nyingine wanafuatilia,” ilisema taarifa hiyo ya Ridhiwani.
Vilevile taarifa ya Ridhiwani ilitahadharisha umma wa Watanzania kuwa makini na mambo ya mitandao ambayo hutumia jina lake kwa utapeli kwa lengo la kumchafua, lakini yeye na viongozi wengine hawahusiki na Tanzania Loans Society.
Viongozi wa taasisi hiyo hawakuweza kupatikana kwa njia yoyote ile kwani simu zao hazipokelewi na hata katika ofisi wanazodai kuwapo, hawaonekani.
                      CHANZO CHA HABARI NI TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate