EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 23, 2013

Yanga, Azam FC kumenyana leo

VINARA Yanga wanahitaji matokeo mazuri kwenye mchezo wao muhimu wa leo dhidi ya Azam FC ili kujiimarisha zaidi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Yanga inawakaribisha Azam wanaolingana nao kwa pointi kwenye msimamo katika mechi iliyoteka hisia za mashabiki wengi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kila timu ina pointi 36, lakini Yanga ikifaidika kileleni kutokana na tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa dhidi ya Azam inayokuja kwa kasi.

Endapo Yanga itapiga mwereka kwenye mchezo huo, basi itakuwa imeiruhusu Azam kupanda kileleni kwa mara ya kwanza katika mzunguko wa pili.
Mbali na matokeo mazuri yanayowaniwa na kila timu, upande wa pili wa mchezo huo ni Azam kuja na jaribio la kulipa kisasi baada ya mchezo wa kwanza kuogelea na kichapo cha mabao 2-0.

Ni wazi Azam itaingia uwanjani safari hii kwa lengo la kulipa kisasi ingawa Yanga nayo itapigana kuhakikisha inavuna pointi tatu na kuendeleza ubabe wake.
Mashabiki wa soka nao wana hamu ya kujua nani zaidi kati ya viungo mahiri na chipukizi, Salum ‘Sure Boy’Abubakari wa Azam na Frank Domayo wa Yanga.


Wachezaji hao siyo tu tegemeo kwenye klabu zao, lakini pia ni tegemeo kwenye kikosi cha Timu ya Taifa, Taifa Stars. Domayo anayecheza kama kiungo namba nane na Abubakar anayecheza nafasi ya kiungo namba sita, wana sifa zinazoshabihiana wakisifika kwa pasi zenye ‘macho’ na kutopoteza mpira ovyo. 

Kocha wa Yanga, Ernest Brandts ataendelea kumwamini mshambuliaji “Jerryson Tegete katika kusaka mabao, wakati Kocha wa Azam, Stewart Hall atamtumia John Bocco kwa shughuli kama hiyo.

“Ubingwa wetu uko mikononi mwa Azam ndiyo maana tumejifua kikamilifu ili kuhakikisha tunawafunga na kuweka pengo kubwa baina yetu,” alisema Tegete akizungumzia mchezo huo.

Daktari wa Azam FC, Mwanandi Mwankema amethibitisha kuwa wachezaji Brain Omony na Kipre Balou wapo fiti kuikabili Yanga leo.
Mechi nyingine leo hii ni Prisons iliyopokea kipigo cha bao 1-0 kutoka Simba katikati ya wiki hii dhidi ya Polisi Morogoro Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Mgambo JKT watapepetana na wenzao wa Ruvu Shooting katika pambano litakalorindima kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate