EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 2, 2013

Tanzania tukijipanga tutafuzu Afcon mwaka 2015

KOCHA wa Taifa Stars, Kim Poulsen amesema haoni sababu za kikosi chake kushindwa kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika zitakazofanyika 2015 nchini Morocco.

Mara ya mwisho Taifa Stars ilifuzu kushiriki Fainali za Afrika miaka 33 iliyopita nchini Nigeria na Taifa Stars kutolewa katika hatua ya makundi.


 
Hivi sasa Fainali za Afrika 2013 zinaendelea nchini Afrika Kusini zikiwa kwenye hatua ya robo fainali ambazo zitachezwa leo na kesho, huku mechi ya nusu fainali ikitarajiwa kuchezwa Jumatano na mechi ya fainali itachezwa Jumapili.

Ni wazi mwisho wa fainali hizi za 2013 utakuwa mwanzo wa fainali nyingine za 2015, ambapo ili kuweza kushiriki fainali za 2015 inabidi kufanya vizuri katika hatua ya makundi ya kufuzu kushiriki fainali hizo.

Mara kwa mara tumeshuhudia timu inayoshika nafasi ya kwanza katika kila kundi katika mashindano ya kuwania kufuzu ndiyo hufuzu kushiriki fainali, hivyo kuna umuhimu wa kuchagua wachezaji wenye uwezo.

Tunaungana na Kocha Poulsen kuamini Taifa Stars ina kila sababu ya kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika 2015, lakini hilo litawezekana iwapo maandalizi mazuri yatafanyika.

Taifa Stars inaweza kufuzu kama wachezaji wanaochaguliwa kikosi hicho watakuwa na uzalendo wa hali ya juu, umoja na kuwa na lengo moja, kwa sababu lengo moja huleta ushindi.
Tunasema hivyo kwa sababu tunafahamu wachezaji wa timu ya Taifa kazi yao kubwa ni kupigania kitu ambacho huwa na thamani na kumbukumbu kubwa kwa vizazi vingi vitakavyofuatia.

Kitu wanacholeta wachezaji wa timu ya Taifa ni ushindi, siku zote wachezaji wanaposhinda huwa wanaliletea Taifa lao furaha na kujisikia fahari kuishi katika taifa hilo.

Wachezaji hawatakiwi kuwa wabinafsi wanapokuwa uwanjani ila wanatakiwa kucheza kitimu na kusaidiana ili kulipigania taifa lao kwa hali.

Wanatakiwa pia kutambua umuhimu na wajibu wanaokuwa nao wakati wakiliwakilisha taifa, pia wafahamu hiyo ndiyo nafasi yao kujitangaza.

Tunarudia tena kusema kuwa, tunaungana na Kocha Poulsen kwamba tunaweza kufuzu kushiriki Fainali za Afrika 2015 kwani timu ya Cape Verde iliweza kufuzu na kushiriki Fainali za Afrika 2013 kwa mara ya kwanza wakati katika Fainali za Afrika 2012 timu za Niger na Botswana zilifuzu kwa mara ya kwanza pia.

Nchi za Botswana na Niger hazikufuzu kirahisi kushiriki katika fainali hizo za Afrika 2012, ila zilipambana katika makundi yao na kuzishinda timu kubwa kama Misri, Afrika Kusini na Tunisia na kushika nafasi ya kwanza katika makundi yao.

Pia Cape Verde haikufuzu kirahisi Fainali za Afrika 2013 kwani ilizifunga Madagascar na Cameroon na kukata tiketi ya kushiriki fainali hizo za Afrika.
Tanzania inatakiwa kufanya kama zilivyofanya Botswana, Niger na Cape Verde ili kuhakikisha inafuzu kushiriki fainali za Afrika zijazo, lakini ni wazi inatakiwa kuhakikisha inamaliza ya kwanza katika kundi wakati wa mechi za kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Afrika.

Ili kufanikisha hilo inabidi tuwe na wachezaji mahiri katika safu ya ulinzi, kiungo na ushambuliaji, pia viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wanatakiwa kuwa na mipango sahihi ya kuhakikisha tunafuzu kushiriki fainali za Afrika.

Hatutaweza kufuzu kama hatuna nia ya dhati ya kutaka kufuzu na kushiriki fainali hizo, ambapo tunatakiwa tuandae wachezaji wenye vipaji wanaoweza kushindana katika kiwango cha juu, wenye akili ya mchezo, mwili, stamina na kasi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate