EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 26, 2013

Waziri amuondoa, aagiza katiba mpya ifutwe, itumike ya zamani

SERIKALI imemuondoa Msajili wa Vyama na Klabu za Michezo nchini na kuagiza kufutwa kwa katiba mpya ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na badala yake itumike ile ya mwaka 2006.

Hatua hiyo, imekuja baada ya hivi karibuni kuibuka kwa utata juu ya katiba mpya ya TFF, iliyopitishwa kwa njia ya waraka, wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo uliopangwa kufanyika Februari 24 na ule wa Bodi ya Ligi Februari 22, kabla ya kusitishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alisema kuwa ameamua kumteua msajili mpya, baada ya aliyekuwepo kupitisha katiba mpya ya TFF kinyume na utaratibu.
Alisema kuna mengi yalijitokeza ikiwemo baadhi ya wagombea kulalamikia kuenguliwa, hivyo wizara iliamua kuliangalia hilo kwa uzito unaostahili na kuamua kuchukua hatua stahiki.
             Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara
Mukangara alisema sheria Na.12 ya BMT na marekebisho yake Na.6 ya mwaka 1971 pamoja na kanuni za BMT na kanuni za usajili Na. 442 mwaka 1999 zimekiukwa.

Alisema kuwa zipo taarifa kupitia vyombo vya habari kuwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) litakuja Tanzania, hivyo anamuelekeza Msajili na anailekeza TFF kuitaarifu kuhusu maelekezo hayo ya kutumia katiba ya mwaka 2006, na waambiwe hali halisi iliyojitokeza.
Mukangara alisema anaielekeza TFF iitishe mkutano mkuu kwa msingi wa katiba yao ya mwaka 2006 na kanuni za BMT na wafanye uchaguzi kwa mujibu wa katiba hiyo kwa kuzingatia sheria za BMT.

Alisema kanuni ya BMT Na.11(1), inaeleza wazi utaratibu wa marekebisho ya katiba haikufuatwa, kwani kimsingi, TFF ilitakiwa ijaze fomu Namba 6,7,8 na 9 kwa mujibu wa sheria na kanuni za BMT.
Mukangara alisema kimsingi upo utaratibu wa kurekebisha katiba za vyama vya michezo, kwa mujibu Sheria ya Baraza la Michezo iliyotungwa na Bunge, na kanuni zake ziko wazi na ni rahisi kuzielewa.

“Sasa TFF hawakufuata taratibu kwa mujibu wa sheria na kanuni za BMT.
“Baada ya kupitia taarifa mbalimbali za BMT, nimejiridhisha kuwa katiba itakayotumika ni ile ya mwaka 2006, ikiwa ni pamoja na TFF kuitisha mkutano mkuu na kutumia katiba ile ile ya mwaka 2006,” alisema Mukangara.
Alisema kwa mamlaka aliyonayo, anaagiza msajili awajulishe TFF, kufuta matumizi ya katiba ya mwaka 2012 na watumie ya mwaka 2006 na barua ilifikie shirikisho hilo kabla ya saa 7 mchana, jana.
Waziri huyo, alitoa maagizo kwa msajili kufuata taratibu za usajili kwa mujibu wa sheria na kanuni za BMT.

Alibainisha kuwa kuna taarifa ya uwezekano wa FIFA, ikachukua hatua kali juu ya serikali kuingilia, kitu ambacho amedai si kweli.
Mukangara aliongeza kuwa kila nchi ina Katiba yake, hivyo si kweli kama FIFA wanaweza kuifuta Katiba ya nchi.
Alipotafutwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, kuhusu uamuzi wa serikali, alisema ni mapema mno kwao kusema lolote hadi pale watakapopata rasmi taarifa hiyo.
“Hatuwezi kusema lolote, kwani hatujapata taarifa rasmi ya serikali tujue kama ni maoni, ushauri au agizo. Tukishajua ni kitu gani, TFF kama taasisi ndipo kwa kutumia vyombo vyake vya maamuzi, itatoa uamuzi na msimamo wake,” alisema Osiah.
Hata hivyo akaongeza kuwa kama ni agizo hakuna tafsiri nyingine ya kilichofanyika, isipokuwa serikali kuingilia masuala ya uendeshaji wa soka, jambo ambalo limekuwa likipingwa na FIFA.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate