EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 30, 2013

Anayedaiwa kumuua Padri mbaroni


Omar Mussa Makame, mkazi wa Mwanakwerekwe Zanzibar
MTU mmoja, Omar Mussa Makame (35), mkazi wa Mwanakwerekwe Zanzibar, amekamatwa na Jeshi la Polisi Zanzibar, kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa Padri wa Kanisa Katoliki Zanzibar, Evaristus Mushi. Taarifa hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Kamishna wa Jeshi hilo Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa Kamishna Mussa, mtuhumiwa huyo alikamatwa Machi 13, mwaka huu, katika Mtaa wa Kariakoo, Zanzibar na atafikishwa mahakamani baada ya taratibu zote kukamilika.

“Huu ni mwanzo tu, kwani Jeshi la Polisi linaendelea na upelelezi wa kitaalamu ili kuhakikisha watu wote wanaohusika na matukio ya uhalifu hapa Zanzibar, wanakamatwa na kufikishwa katika mkondo wa sheria.

“Jalada la mtuhumiwa huyu tayari limeshapelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka kwa hatua za kisheria kwa sababu yeye ndiye atakayetupa mwongozo juu ya suala hili.

“Kabla mtuhumiwa hajakamatwa, tulifanya upelelezi kwa kutumia michoro na alipokamatwa, watu waliokuwa eneo la tukio siku ambayo padri aliuawa, walimtambua kwamba ndiye aliyekuwapo.
“Lakini, kwa kuwa tulikuwa tumeahidi zawadi ya shilingi milioni kumi kwa atakayesaidia kukamatwa kwa watuhumiwa na kwa kuwa mtuhumiwa huyu amekamatwa kwa msaada wa wananchi, aliyesaidia kukamatwa, atakabidhiwa fedha zake katika mazingira ya usiri kwa ajili ya kulinda usalama wake.

“Pamoja na kazi nzuri tunayoifanya kwa kushirikiana na wananchi, bado tunahitaji msaada wao katika harakati zetu za kukabiliana na uhalifu,” alisema Kamishna Mussa.

Padri Mushi aliuawa na watu wasiojulikana kwa kupigwa risasi kichwani Februari mwaka huu, wakati akiingia katika Kanisa Katoliki, Kigango cha Mtakatifu Theresia, Zanzibar.

Baada ya watu hao kufanya mauaji hayo, walitoweka kwa kutumia pikipiki waliyokuwanayo wakati wanamsubiri padri huyo awasili kanisani hapo.

Kutokana na uzito wa tukio hilo, Jeshi la Polisi nchini, lilifanya upelelezi kwa kuwashirikisha wataalamu wa masuala ya upelelezi kutoka Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) ambao waliwasili Kisiwani Zanzibar na kuchora michoro kuonyesha jinsi mauaji hayo yalivyofanyika.

Juzi, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, alizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kuonyesha jinsi asivyoridhishwa na ukimya wa upelelezi wa kuuawa Padri Mushi na kujeruhiwa kwa risasi, Padri Ambrose Mkenda.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate