EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, April 5, 2013

Njia zinazomfanya mjasiriamali afanikiwe.

 
HAKUNA njia ya mkato ya kufanikiwa katika biashara. Kama ipo, mambo yangekuwa ni rahisi, na tusingesikia habari zinazoelezea biashara zimekufa, ama kukosa mwelekeo. Lakini ukiangalia biashara zenye mafanikio, utaona mambo fulani fulani yanafanana katika uendeshaji wake.
Kuna hatua ambazo kampuni hizo zinafuata. Njia hizo ndizo zinazowafikisha kwenye mafanikio hayo. Zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo wajasiriamali wanazitumia na zimewafanya wafanikiwe katika biashara zao.

Ni vema ukafahamu kuwa kila unayekutana naye mtaani ana wazo la biashara. Lakini wazo moja kati ya mia uliyoyapata litakufanya uwe mjasiriamali. Lakini watu wengi wanaogopa kufanya biashara ambayo itawapatia hasara, au itawafanya watumie mshahara wao kwa ajili ya kuiimarisha. Kufanikiwa katika biashara, inakubidi ufanye uamuzi thabiti. Inakubidi kuwa jasiri wa kutumia wazo lako.
Pili, ndoto yako ndiyo itakayokufanya kuwa mfanyabiashara aliyefanikiwa katika kiwanda cha burudani.

Lakini huwezi kuwa na biashara hiyo kama haujui kitu chochote kuhusu filamu pamoja na ujuzi wa hali ya juu wa teknolojia.
Inakubidi kwanza kuwa na uelewa kuhusu kile unachotamani kukianzisha ili uweze kukisimamia.

Mjasiriamali yeyote anajifunza kutokana na makosa. Hapa namaanisha kuwa, kila hatua anayoifanya ambayo inasababisha ashindwe katika biashara yake, inabidi afanye utafiti na kujua ni jinsi gani atahimili changamoto hiyo, na kujitahidi asirudie kosa lililotokea katika biashara husika.

Hatakiwi kukata tamaa, pia anatakiwa kuwa na mawazo chanya kila wakati katika maisha na ujasiriamali anaoufanya.

Mwanzo wa biashara yako utaweza kufanya makosa mengi. Chukua makosa hayo kama ndio kipimo chako cha kufanikiwa, jitahidi kutorudia.
Kila changamoto unayokutana nayo ifanye kuwa ndiyo nafasi ya kujifunza na kufanya vizuri zaidi katika biashara yako.

Wakati unamiliki biashara unakuwa na uhuru. Tumia uhuru huo kufanya vizuri zaidi, pia jifunze kuwa na nidhamu ya biashara. Hapa itakubidi ufanye kazi kwa bidii na kujituma zaidi.
Inabidi ujikite zaidi kwa wazo lako la biashara na wale wote ambao walikuwa sehemu ya kukamilisha ndoto yako, ambao wanaweza kuwa wafanyakazi wako, marafiki ama familia yako.

Kama utakuwa umejizatiti katika biashara yako ndipo utakapofanya jitihada zaidi za kuiboresha ambazo zitakuwezesha kufanikiwa sana.
Kumbuka kuwa hakuna mti uliozaa matunda kwa usiku mmoja. Pale mti unapochomoza, ili ukue unapitia hatua mbalimbali.

Kama mjasiriamali inakubidi uwe na roho ya uvumilivu ili matunda ya kazi yako yaweze kukomaa. Pia kuongeza jitihada zaidi katika kila hatua, kuwa imara na mwenye malengo.
Kuwa tayari kukubali makosa na kuyasahihisha. Kuwa imara pia ni ufunguo wa mafanikio katika biashara.

Pia mawazo mgando hayahitajiki katika biashara. Inakupasa kujifunza na kuiga mambo mazuri kutoka kwa wengine, pia ukumbuke kuwa kila siku ina jambo jipya la kujifunza kuhusu biashara.
Mawazo yako yatawafikia wateja wako kwa urahisi, japo katika hatua za awali za biashara zako inawezekana ukapata wateja wachache. Hivyo inakubidi kuonesha bidhaa zako kwa wateja wako.

Kuwa tayari kujibu maswali kutoka kwa wateja wako, kwa mfano: “Bidhaa zako zina kitu gani cha tofauti zaidi ya wafanyabiashara wengine?”
Kama utakuwa na majibu ya kuwaridhisha utakuwa umefanikiwa katika hilo.
Pia ukumbuke kuwa kila biashara ina ‘risk’. Hivyo uwe tayari kukabiliana nazo. Ni vema ukawashirikisha wataalamu katika biashara yako.
Hizi ni baadhi tu ya hatua ambazo zitakusaidia katika kuboresha ama kukabiliana na changamoto katika biashara yako.
Maisha Yetu na  Lucy Ngowi

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate