EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 9, 2013

Serikali yawafunga midomo wabunge

*Wazuiliwa kujadili ripoti ya CAG
*Zitto adai Bunge lageuka kibogoyo

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema kitendo cha wabunge kufungwa mdomo kujadili ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kitaligeuza Bunge hilo kuwa kibogoyo.

Kauli ya Zitto imekuja muda mfupi baada ya Ofisi ya Bunge mjini Dodoma kutoa ratiba ya vikao vyake ambavyo vinaanza leo, ikionyesha ripoti ya CAG itawasilishwa bungeni, lakini hataijadiliwa kama ilivyozoeleka.

Alisema kutojadiliwa kwa ripoti hiyo, kutaendelea kutoa mianya ya ulaji ambayo tayari ilikuwa imeanza kuzibwa kutokana na ripoti hiyo kujadiliwa kwa kina na wabunge kama ilivyokuwa mwaka jana.


“Nina jibu moja tu, kutojadili ripoti ya CAG, sasa Bunge limekuwa kibogoyo. Kila siku nguvu za Bunge zinazidi kupungua.

“Ulaji utaendelea kwa kutojadili kwa uwazi taarifa ya CAG, wananchi wakatae Bunge kibogoyo,” alisema Zitto.

Lakini habari za kuaminika zilizopatikana mjini Dodoma jana na kuthibitishwa na Ofisi ya Bunge, zinasema ripoti ya CAG ambayo huwasha moto mkali katika utendaji kazi hasa wa mawaziri, itawasilishwa bungeni Ijumaa ya wiki hii.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Habari, Deogratius Igidio, alisema ripoti hiyo haitajadiliwa kutokana na mabadiliko ya ratiba ya vikao vya Bunge.

Alisema Bunge, linatimiza sheria inayotaka ripoti hiyo kuwasilishwa bungeni kila Aprili ya kila mwaka na kwamba kutojadiliwa kwake kunatokana na mabadiliko ya ratiba ya Bunge na kuwataka Watanzania waelewe hivyo.

“Sheria inataka taarifa ya CAG iwasilishwe Aprili, kutokana na mabadiliko ya ratiba ya Bunge ambapo mfumo mzima wa bajeti umebadilika, inatuwia vigumu kuijadili taarifa hii.

“Taarifa ya CAG, ikishawasilishwa kwa Rais, anatoa idhini iletwe bungeni, lakini mabadiliko ya bajeti ya Serikali, haitajadiliwa, bali itawasilishwa tu kama ambavyo ripoti nyingine za mwaka huu, zinavyowasilishwa bila kujadiliwa.

“Siwezi kusema lini itajadiliwa, ila hapa katikati baada ya kumalizika kwa mkutano huu, lazima kutakuwa na mikutano miwili kabla ya Bunge la Katiba, watakaopanga ratiba watazingatia hilo,” alisema Igidio. Kwa mujibu wa ratiba hiyo, leo Bunge linatarajia kupitisha Azimio la Marekebisho ya Kanuni za Kudumu.

Siku ambayo ripoti hiyo itawasilishwa itakuwa ni siku ambayo mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, utakuwa ukiendelea kujadiliwa.

Kesho Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, atasoma hotuba ya ofisi yake, itahusisha wizara tatu na itajadiliwa kwa siku tano.

Wizara ambazo zimo ndani ya hotuba hiyo, ni Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Baada ya wizara hiyo, hotuba za wizara nyingine zitafuatia na Bajeti ya Serikali itakayosomwa Juni 13, mwaka huu saa 10 jioni, siku ambayo nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki zatasoma bajeti zao.

Baada ya kusomwa kwa bajeti hiyo, kutakuwa na siku ya mapumziko kabla ya wabunge kuijadili kwa siku saba. Bunge linatarajiwa kuahirishwa Juni 28, mwaka huu.

Itakumbukwa mwaka jana, moto uliowashwa bungeni na wabunge kuibana Serikali, baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya CAG, uliwalazimu mawaziri wanane kutakiwa kupima uzito wa makosa yao na kufanya maamuzi, ikiwa ni pamoja na kutakiwa kujiuzulu.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, alitoa wito kwa wabunge wote kujiorodhesha kwa nia ya kupata saini za wabunge 71 ambao wangewasilisha kutimiza matakwa ya kisheria kupata asilimia 20 ya wabunge kwa ajili ya kumuondoa Waziri Mkuu.

Kutokana na hali hiyo, mawaziri kadhaa walimwandikia Rais Jakaya Kikwete, kwa ushauri wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuiokoa Serikali ya chama hicho isianguke kutokana na mpango wa wabunge kujiorodhesha kutaka kumuondoa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Waliotakiwa kuondoka, ni Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI0), George Mkuchika, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Jumanne Maghembe na Waziri wa Afya, Dk. Hadji Mponda.

Lakini baadhi ya walisakamwa na walijitetea hawahusiki kwa lolote na mambo wanayotuhumiwa nayo, huku baadhi wakiona mambo ni mazito na kusubiri panga la Rais.Via MTANZANIA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate