EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 9, 2013

Walimu walikimbilia bungeni

CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT), kimeliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingilia kati mgogoro wake na Serikali, ili kuilazimisha itekeleze mapema matakwa ya walimu kabla hawajachukua hatua zaidi.

Kauli hiyo, imekuja kufuatia Serikali kudaiwa kupuuza hukumu ya mahakama pamoja na ushauri wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, iliyoelekeza pande zote mbili zikae kwa majadiliano zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Rais wa CWT, Gratian Mukoba, alisema Serikali imeonyesha kutojifunza kutokana na mgomo wa walimu uliotikisa nchi nzima mwaka jana.

Alisema siku zote Serikali imekuwa haiwathamini walimu, licha ya kusema imekuwa ikiwajali siku zote.
Alisema dharau ya Serikali, imeonekana wazi kwa sababu imeshindwa kuheshimu vyama vya wafanyakazi, ambavyo vinatambuliwa kisheria.

“Kutokana na hali hii, tunatoa wito kwa walimu kuungana pamoja kuilazimisha Serikali kukubali kukaa meza moja na CWT kujadili mishahara ya walimu kwa ajili ya mwaka ujao wa fedha.

“CWT kinatoa wito kwa Bunge kuingilia kati suala hili, ili kuepusha mgogoro unaoweza kujitokeza ikiwa Serikali itaamua kupanga mishahara ya walimu, bila kujadiliana na CWT.

“Tunatoa wito kwa wazazi wa wanafunzi kuingilia kati, kuna hatari wanafunzi milioni 10 kukosa masomo ikiwa walimu watagoma kutokana na kushindwa kulipwa stahiki zao.”

Aprili 2, mwaka huu, makatibu wakuu wa vyama mbalimbali vya wafanyakazi, ikiwamo CWT, walikutana na makatibu wakuu wa Wizara ya Utumishi wa Umma, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ambapo Serikali ilieleza msimamo wake wa kutojadili mishahara kupitia majadiliano kwenye mabaraza ya kisekta, ikiwa ni pamoja na Baraza la Majadiliano la Walimu.

Kwa muda mrefu sasa, walimu wamekuwa wakiitaka Serikali iongeze mishahara kwa asilimia 100, posho za walimu wanaofundisha masomo ya sayansi asilimia 55, walimu wa sanaa asilimia 50 na posho ya mazingira magumu asilimia 30.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate