EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 9, 2013

Uhuru aapishwa kuwa rais wa nne wa Kenya.

Viongozi kutoka mataifa kadhaa ya Afrika wamewasili jijini Nairobi kuungana na Wakenya kwenye sherehe za kuapishwa kwa rais mpya wa Kenya, Uhuru Kenyatta, kwenye uwanja wa mpira uliojaa maelfu ya wafuasi wake.
 
Kenyatta mwenye umri wa miaka 51 ni mtoto wa rais wa kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta. Ushindi wake wa asilimia 50.07 katika uchaguzi wa tarehe 4 Machi ulihalalishwa na Mahakama ya Juu baada ya pingamizi lililowekwa na Waziri Mkuu anayemaliza muda wake, Raila Odinga, kutupiliwa mbali na mahakama hiyo.
 
Kenyatta anayekuwa rais wa nne wa taifa hilo la Afrika ya Mashariki tangu lilipopata uhuru wake kutoka Uingereza mwaka 1963, anakuwa rais wa pili barani Afrika kuwa madarakani hali anakabiliwa na mashitaka kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kwa tuhuma za kusaidia kuchochea ghasia za kikabila zilizoukumba uchaguzi wa urais wa Kenya wa mwaka 2007. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mwezi Julai, ambapo Kenyatta na naibu wake, William Ruto, wanakabiliwa na mashitaka ya aina moja.
 
Hata hivyo, uchaguzi wa mara hii ulikuwa wa amani na kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, Wakenya wengi wanatarajia kwamba Uhuru atatimiza ahadi yake ya kuwa kiongozi wa watu wote na hatakuwa rais wa kabila lake tu, jambo ambalo limekuwa kawaida kwa wanasiasa wa huko.
Utata unaoyakumba mataifa ya Magharibi
Wanajeshi wa Kenya wakifanya mazoezi ya sherehe za kuapishwa Uhuru Kenyatta. 
Wanajeshi wa Kenya wakifanya mazoezi ya sherehe za kuapishwa Uhuru Kenyatta.
Kwa mataifa ya Magharibi, ambao ni wafadhili wakubwa wa nchi hiyo yenye uchumi mkubwa zaidi kwenye eneo la la mashariki mwa Afrika, Kenya ni mshirika muhimu katika mapambano dhidi ya makundi ya kidini yenye siasa kali kwenye eneo hilo.

Lakini sasa mataifa hayo yanakabiliwa na uchaguzi wa ama kuendelea kuimarisha mahusiano au kujitenga na kiongozi ambaye anakabiliwa na mashitaka kwenye mahakama ya ICC mjini The Hague.
Marekani na mataifa makubwa ya Ulaya yalisema yangelituma mabalozi wao kwenye sherehe za kuapishwa kwa Kenyatta, kiwango cha uwakilishi ambacho wanasema bado kinakwenda sambamba na msimamo wao wa kuwa na mahusiano ya lazima tu na watuhumiwa hao.
Mtaalamu wa masuala ya Kenya katika Chuo Kikuu cha Warwick, Daniel Branch, ameiambia Reuters kuwa mataifa ya Magharibi yamejikuta kwenye hali ngumu sana, lakini huenda kila nchi ikatafuta njia yake yenyewe na mahusiano na Kenya.
China huenda ikapata fursa mpya
Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga. 
Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga.
Ikiwa mataifa ya Magharibi yatagawika kuhusu mahusiano yake na Kenya chini ya Uhuru Kenyatta, hali hiyo itafungua njia zaidi kwa China na mataifa mengine makubwa ya Asia ambayo yamekuwa yakijizolea ushawishi wa kisiasa na kibiashara barani Afrika kwa siku za hivi karibuni.
Wakati kwenye sherehe hizo, viongozi wakuu wa Afrika watajikuta wamewekwa pamoja na mabalozi tu wa nchi za Magharibi, Kenya na India - ambazo zote mbili hazijasaini Mkataba wa Rome ulioanzisha ICC - zimetuma maafisa wao wa ngazi za juu.
Hata hivyo, mabalozi wa Kimagharibi wataepuka matusi mengine, baada ya maafisa wa Kenya kusema kuwa Rais Omar Hassan al-Bashir wa Sudan asingelihudhuria sherehe hiyo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate