EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 9, 2013

Utafiti waonyesha maambukizi ya VVU yaongezeka.

UTAFITI uliofanywa na Mradi wa Mfumo wa Kijamii wa Matibabu ya Virusi vya Ukimwi (CoBaSys) unaonyesha maambukizi ya VVU yamezidi kuongezeka hapa nchini na duniani kwa ujumla.
Akizungumza Dar es Salaam jana, kiongozi wa mradi huo nchini Tanzania, Profesa Ernest Mallya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisema ongezeko hilo limetokana na sababu mbalimbali.

“Kusudio la mkutano wa mwisho ni kuthibitisha ufanisi uliopatikana kutokana na ushirikiano miongoni mwa wadau mbalimbali kitaifa na kikanda, ambao wanajishughulisha na kuzuia maambukizi na matibabu ya VVU na Ukimwi pamoja na matunzo ya waathirika katika ngazi za kimataifa na ngazi ya kikanda,” alisema Profesa Mallya.

Alisema mkutano huo utashirikisha matokeo ya utafiti uliofanywa na jopo la kitaifa kutoka nchi sita za Afrika, majadiliano kuhusu mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa kuhusiana na sera na mikakati ya pamoja iliyoafikiwa na ukanda wa Kusini Mashariki mwa Afrika.
Alisema itasaidia udumishaji wa mwitikio dhidi ya VVU na Ukimwi pamoja na mgogoro wa fedha unaoendelea ulimwenguni ambapo wadau mbalimbali walioalikwa watawasilisha matokeo ya ushirikiano uliokuwapo baina ya Afrika na Ulaya katika kutathimini sababu mbalimbali zinazoathiri kuwapo au kutokuwapo uzingatiaji wa matibabu na jinsi gani hali hiyo inaweza kupunguza unyanyapaa na kutengwa kijamii miongoni mwa waathirika.

Naye, Mratibu wa Mradi wa CoBaSys, Giovanni Guaraldi, alisema washiriki katika mkutano huo pia watajadili tatizo la uendelevu wa matibabu ya VVU na Ukimwi pamoja na utegemezi kwa wafadhili.

“Mkutano wa mwisho wa CoBaSys unakusudia kujadili jinsi mifumo ya matibabu ya kijamii itakavyobiliana na changamoto mbalimbali za usoni mara nyingi, zikijumuisha mabadiliko ya VVU na Ukimwi kuwa magonjwa sugu, ukosefu wa fedha kutoka kwa wafadhili na ongezeko la ukosefu wa usawa katika upatikanaji wa huduma bora za afya,” alisema Guaraldi.

Alisema hata kama mifumo ya matibabu ya kijamii haitaweza kukabiliana vya kutosha na ongezeko la changamoto nyemelezi zinazoambatana na umri mkubwa wa watu wanaoishi na VVU, ongezeko la haki za kiraia na uraia utahakikisha haki za kiafya na za kijamii zinalindwa na kutakuwapo na upatikanaji wa huduma bora za afya kwa usawa katika ngazi za kitaifa na kimataifa.

Alisema mkutano huo ni sehemu ya mradi wa CoBaSys unaokusudia kuanzisha mtandao wa kikanda kwa ajili ya kuhakikisha sera ya afya inaziwezesha jamii kusaidia mipango ya utoaji wa dawa za kurefusha maisha ya waathirika (ARVs) kwa wagonjwa wenye VVU katika nchi za Kusini na Mashiriki mwa Afrika.

“Mifumo ya kijamii ya kuwatunza waathirika imekuwa ikisisitizwa na Serikali na asasi mbalimbali kwa sababu inahimiza ushirikishwaji wa wadau mbalimbali, jamii ikihusishwa kikamilifu katika kubainisha matatizo na mahitaji yao, kisha kuchagua masuala yanayostahili kupewa kipaumbele na kuainisha rasilimali mbalimbali ambazo zinaweza kutumika kukidhi mahitaji hayo,” alisema Guaraldi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate