EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, May 29, 2013

Tiketi za mabasi kukatwa kwa njia ya simu.

KAMPUNI ya ACG-E-Bus Ticketing ya jijini Dar es Salaam imekuja na huduma ya kukata tiketi za mabasi yaendayo mikoani kwa njia ya mtandao wa simu za mkononi.

Huduma hiyo ambayo tayari imeshaanza, itakuwa dawa ya kuwaondoa wapiga debe ambao mara nyingi wamekuwa wakilalamikiwa na abiria kwa usumbufu.

Akizungumza jana, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Martin Kaswahili, alisema huduma itafanywa kupitia mitandao yote ya simu za mkononi na itaondoa usumbufu wa abiria kulazimika kufika Kituo cha Mabasi Ubungo kukata tiketi.

Kwa mujibu wa Kaswahili, kuanzishwa kwa huduma hiyo ni matokeo ya utafiti wa muda mrefu katika vituo vya mabasi vya miji mikubwa ya Ubungo, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya ambao umebaini kuwapo kwa urasimu na usumbufu wa abiria kupata tiketi za mabasi wanayotaka kusafiri nayo.

“Tulifanya utafiti katika sekta ya usafirishaji wa nchi kavu hasa mabasi, tuliongea na wenye mabasi, baadhi ya mawakala, abiria wenyewe na tukagundua tatizo kubwa la abiria waendao mikoani hasa katika vituo vya miji mikubwa kama vile Mwanza, Dar es Salaam, Mbeya na mikoa mingine ni urasimu wa kupata tiketi na abiria kusumbuliwa hivyo njia ya mtandao ni suluhisho kwao,” alisema Kaswahili.

Kaswahili alisema huduma hiyo inapatikana kupitia mitandao ya simu za mikononi za Tigo, Airtel, Voda.

“Ili kupata huduma hiyo, abiria anatakiwa kupiga *150*16# kisha utakuja ujumbe wa kukukaribisha E-Bus Ticketing na kukuuliza lugha unayotaka kutumia.
“Ukishachagua lugha, utakuja ujumbe utakaokutaka ujaze kituo unachotoka. Kama upo Dar, Mbeya au sehemu yoyote utajaza, kisha utapata ujumbe unaokutaka ujaze unakokwenda, utapata ujumbe unaokuuliza kampuni ya basi unayotaka kusafiri, tarehe ya kusafiri, utakuja ujumbe wa kukutaka uchague nauli unayotaka kulipa.

 “Baada ya hapo utachagua kiti unachotakiwa kukaa kama ni dirishani au sehemu yoyote na kisha utapata maelezo ya tiketi yako,” alisema.

Kaswahili alisema ikifika asubuhi, abiria anapaswa kwenda na ujumbe wa tiketi yake kwenye simu na kama ujumbe huo umefutika kwa bahati mbaya, anatakiwa kutaja namba aliyotumia kununulia tiketi na kuonesha kitambulisho.

Alisema changamoto waliyonayo kwa sasa ni ya uelewa kwa abiria na wenye mabasi hivyo wanahitaji elimu zaidi juu ya huduma hiyo.
Alitoa wito kwa wateja na kuwataka abiria kujiandaa na mabadiliko hayo kwa ajili ya kuondoa usumbufu kwao.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate