EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 29, 2013

Kashfa nzito Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam


HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam imeingia katika kashfa nzito baada ya kuvunja nyumba ya mwanamke mmoja Ashura Swed mkazi wa Upanga kwa maelezo kuwa ipo barabarani.

Katika hali ya kushangaza, manispaa hiyo imemruhusu kujenga eneo hilo hilo mtu mwingine aliyejulikana kwa jina la Bahadur Dewji mwenye asili ya Asia.

Akizungumza na Tanzania Daima, mjukuu wa Ashura, Shamsa Salim ameiomba serikali kuingilia kati sakata hilo ili kuzuia kile alichodai kuwa uonevu wanaofanyiwa na watu wenye uwezo wa pesa.

Akisimulia huku akibubujikwa na machozi, Shamsa alisema Alhamisi ya wiki iliyopita walishangaa kuona nyumba yao namba 897 iliyoko Mtaa wa Mfaume, Upanga ikivunjwa huku wao wakiwa hawana taaarifa yoyote juu ya ubomoaji huo kwa madai kuwa ipo barabarani.

“Ilikuwa Alhamisi, wiki jana, majira ya saa tano asubuhi tulishtuka na kushangaa kuona kundi la watu waliojitambulisha kuwa wafanyakazi wa Manispaa ya Ilala wakivunja nyumba yetu. Tulipowaomba watupatie amri ya mahakama inayowaruhusu kuvunja nyumba yetu hawakutuonyesha badala yake waliendelea kuvunja tu.


“Kama wanadai kuwa nyumba yetu ipo barabarani, mbona jengo la SIDO halijabomolewa? Kama sio uonevu huu, ni nini jamani?” alisema kwa uchungu Shamsa.

Alisema kuwa bibi yake ambaye ni ajuza mjane, ni mmiliki halali wa nyumba hiyo hata kabla ya mumewe kufariki dunia Juni, 2009 na kuongeza kuwa kuvunjwa kwa madai kuwa wamevamia barabara na eneo lao kupewa mtu mwingine ni uonevu wa dhahiri kwa Mtanzania mnyonge.
Alisema wamefuatilia kwa siku kadhaa tangu wiki iliyopita walipoona ujenzi wa haraka unaanza na kubaini kuwa kuwa unafanywa na Dewji ambaye alidai anawanyima amani kwani amefikia hata kupiga risasi ili kuwatisha wasidai haki yao.

“Tulipoona tunanyang’anywa haki yetu tulienda kuchukua RB, tunayo na sasa tumefungua kesi, na kama huyo Dewji hilo ni eneo lake kwanini anafanya mambo ya ajabu ya kutunyima amani? Nina imani haki ya mtu haipotei, kwa kuwa sisi ni wamiliki halali wa eneo hili, na watu wasitumie fedha zao kutunyanyasa sisi wanyonge jamani,” alibainisha Shamsa.

Alisema kuwa walipoona hali si shwari usiku wa kuamkia Jumatatu, wiki hii walimpigia simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi ili awape msaada baada ya Dewji kufyatua risasi nne kuelekea katika nyumba yao.
Shamsa alisema kuwa Kamanda Minangi alifika kwa wakati katika eneo hilo akiwa na askari wake, lakini walishangaa kuona wakishindwa kumkamata mtuhumiwa wao na badala yake askari mmoja alianza kuwasihi walitupe ganda la risasi walilookota kwa maelezo kuwa wanaweza kugeuziwa kibao wakapata matatizo makubwa.
Amemtaka Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka kuingilia kati ili haki ipatikane.
Tanzania Daima lilimtafuta Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Mwendahasara Maganga ili kutolea ufafanuzi tuhuma hizo ambapo alisema kuwa hakuwa na taarifa yoyote kuhusu suala hilo na kumtaka mwandishi ampe muda ili alifuatilie kwa wasaidizi wake.
“Kwa kweli sina taarifa kabisa na suala unalonieleza, nipe muda niwasiliane na wasaidizi wangu, lakini ninachoweza kukuhakikishia ni kwamba sisi ni taasisi inayofanya kazi kwa utaratibu, hatuwezi kumpa mtu au taasisi yoyote kibali cha kujenga eneo ambalo ni barabara. Huyo jamaa aliwaonyesha kibali cha kuruhusiwa kujenga? Kama hakuwaonyesha basi huyo ni mhuni tu, nipe nafasi nilifanyie kazi,” alifafanua Maganga.
Kwa upande wake Dewji anayedai kuwa mfanyakazi wa Aghakan Foundation, amedai kuwa eneo hilo wamepewa kihalali na manispaa ili wajenge barabara ya kutokea wanafunzi wa Sekondari ya Aghakan.
Naye Kamanda Minangi alikiri kupigiwa simu na Shamsa kupewa taarifa za Dewji kurusha risasi, lakini akadai kuwa taarifa hizo zilikuwa za uongo.
Lakini katika hali ya kushangaza Tanzania Daima lilipofika eneo la tukio liliona askari polisi wakiwa wamewekwa hapo kupiga doria, hali iliyothibitisha madai ya Shamsa kuwa kulikuwa na tatizo kubwa eneo hilo tofauti na maelezo ya kamanda Minangi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate