EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 29, 2013

Serikali yafuta ushuru wa mafuta.

HATIMAYE serikali imeridhia uamuzi wa wabunge na kukubali kufuta pendekezo la kuongeza ushuru wa bidhaa kwenye mafuta ya dizeli na petroli.

Katika marekebisho hayo, Waziri wa Fedha na Uchumi, William Mgimwa alikuwa amependekeza kuongeza ushuru wa mafuta hayo kwa sh 2 kwenye dizeli na sh 61 kwenye petroli kwa lita.

Kwa mantiki hiyo, alisema kuwa wataendelea kutoza ushuru wa bidhaa wa sh 333 kwa lita katika mafuta ya petroli na sh 215 kwa lita kwenye dizeli.

Wakijadili muswada wa sheria ya fedha wa mwaka 2013, wabunge walipinga mapendekezo hayo na kuishauri serikali itafute mapato kutoka kwenye vyanzo vipya vilivyoanishwa na Kamati ya Bunge ya Bajeti badala ya kuongeza gharama za maisha kwa wananchi.

Akijibu hoja za wabunge jana kabla ya kupitishwa kwa muswada huo kuwa sheria itakayoanza kutumika Julai mosi mwaka huu, Waziri Mgimwa alisema walikubali ushauri huo ili kuleta unafuu kwa wananchi na kuzuia mfumuko wa bei unaoweza kujitokeza.

Alisema serikali iteendelea kutoza ushuru wa sasa bila kuongeza hata senti, lakini wameongeza ushuru wa mafuta ya taa kufikia sh 425 kwa lita badala ya sh 400.30 zinazotozwa sasa hivi.


Alisema kuwa hatua hizo ni pamoja na kudhibiti uchakachuaji wa dizeli uliokuwa ukifanywa kwa kutumia mafuta ya taa na hivyo kuingiza nchi katika hatari zaidi.
Pia Waziri Mgimwa alisema kuwa serikali imeongeza ushuru wa mafuta ya petroli (fuel levy) kutoka sh 200 hadi 263 kwa lita ikiwa ni lengo la kuongeza mapato ya mfuko wa barabara nchini ili kugharamia barabara zinazopaswa kujengwa.

“Tumeongeza ushuru wa mafuta ya dizeli (fuel levy) kutoka sh 200 hadi 263 kwa lita. Lengo hili mbali na kuongeza mapato pia nazo zitasaidia kugharamia ukarabati wa barabara,” alisema.

Waziri pia alifafanua kuwa ushuru wa bidhaa kwenye simu hautatozwa kwenye huduma za kutuma na kupokea fedha bali kwenye huduma zingine kama kupiga, kutuma ujumbe mfupi au picha.

“Baada ya kuchunguza kwa undani na kupokea maoni ya kamati ya bajeti, tumeona kweli kuna uwezekano wa mtu kutozwa kodi mara mbili pale anapokuwa ameunganishwa kutoka mtandao mmoja wa simu mwingine. Hilo tutakaa na wenzetu wa TCRA kuliangalia,” alisema.

Aliongeza kuwa serikali imeafikiana na kamati ya bajeti kwamba mapendekezo ya msamaha wa kodi ya zuio kwa ndege za kukodi yasogezwe mbele hadi mwaka ujao wa fedha ili kutoa muda kwa serikali na wafanyabiashara wa sekta ya anga kuendelea kujadiliana.

“Serikali pia imeridhia mapendekezo ya kamati ya bajeti ya kukusanya mapato kutoka uvuvi wa bahari kuu na sasa linafanyiwa kazi ili kiwe moja ya vyanza vipya vya mapato vitakavyotupa mapato makubwa pamoja na uwekezaji kwenye migodi mikubwa,” alisema.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate