EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 5, 2013

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, amemuagiza Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR - Mageuzi), kuandika maelezo kuhusu aina ya sumu anayoizungumzia kuwa inatokana na upungufu uliomo kwenye vitabu vya Hisabati.

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, amemuagiza Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR - Mageuzi), kuandika maelezo kuhusu aina ya sumu anayoizungumzia kuwa inatokana na upungufu uliomo kwenye vitabu vya Hisabati kwa shule za msingi ambayo inachangia kuua elimu ya Tanzania.
Makinda alitoa agizo hilo bungeni mjini hapa jana muda mfupi baada ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa, kumaliza kujibu swali la mbunge huyo wa kuteuliwa.
“Uandike maelezo na uyapeleke ukiwa umeeleza hiyo sumu inafanana fananaje ...kwani kauli ulizozitoa kuhusiana na sumu ni nzito sana,” alisema Makinda.
Mbunge huyo katika swali lake la nyongeza alitaka kujua kama serikali iko tayari kupiga marufuku vitabu hivyo kuendelea kutumika kwa kuwa ni sumu kutokana na miongozo yake kutofaa kwa taifa.
Pia mbunge huyo alitaka kujua mpango wa wizara kuwawajibisha watendaji.

Awali katika swali la msingi, mbunge huyo alitaka kujua kama vitabu hivyo vya Hisabati vilihaririwa na wataalamu wa somo husika na kama wataalamu hao hawakuweza kubaini udhaifu huo au kama ulionekana walichukua hatua gani.

“Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha South Carolina (USA), chini ya ufadhili wa USAID iliandika vitabu vya Hisabati kwa shule za sekondari, vitabu ambavyo havikuandikwa kwa ubora unaokubalika, hii ikiwa ni sababu mojawapo kubwa inayosababisha wanafunzi wengi kufeli somo la Hisabati,” alisema Mbatia.

Akijibu swali la nyongeza, Waziri Kawambwa alisema si kweli kabisa kwamba vitabu hivyo ni sumu na vinaharibu elimu ya Tanzania na ndivyo vinavyosababisha somo la hesabu kutosomeka.
Kawambwa alisema kazi ya kuhakiki vitabu hivyo ilifanyika kitaalamu na kiusahihi na wataalamu wa wizara na kubaini kuwa vitabu hivyo vina uwezo wa kutosha.

Kuhusu suala la kuwawajibisha wataalamu kwa madai kuwa wametoa majibu ya uongo waziri alisema hiyo ni taarifa ya kikazi hivyo wataifanyia kazi.
Akijibu swali la msingi, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, alisema mwaka 2009 Rais Jakaya Kikwete aliomba msaada wa vitabu vya Sayansi na Hisabati kutoka Serikali ya Marekani.

Alisema Serikali ya Marekani kupitia Shirika la USAID ilitoa msaada huo chini ya usimamizi wa Chuo Kikuu cha Jimbo la Carolina ya Kusini ambacho kilisimamia na kuratibu msaada huo.
“Wakati huo huo, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa imekwisha kupata msaada huo mwaka 2009 kwa masomo ya Sayansi na Hisabati hususan katika uandishi wa vitabu,” alisema.
Mulugo alifafanua kuwa wizara hiyo ilikubaliana na Chuo Kikuu cha Jimbo la Carolina na Shirika la USAID kutumia vitabu ‘Mathematics for Secondary School Book 1,2,3 na 4’.

Aidha, alisema wizara iliteua wataalamu sita wa somo la Hisabati ambao walifanya kazi ya kuvihariri vitabu hivyo mwaka 2010, na baada ya kazi hiyo, jukumu la kuvihakiki na kuvitathmini lilitekelezwa na watathmini ambao ni walimu watatu wa somo la Hisabati kutoka shule za sekondari, mtaalamu mmoja kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania na mshauri mmoja kutoka Chuo Kikuu cha Jimbo la South Carolina.

Alisema kazi hiyo ilipokamilika wizara kupitia EMAC ilivipitisha na kuvipa hati ya ithibati kuwa vitabu vya kiada katika shule za sekondari Mei, 2011.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate