EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, July 20, 2013

Wadau watofautiana uteuzi kamati TFF.

WADAU mbalimbali wa soka hapa nchini, wamechukulia kwa sura tofauti uteuzi wa Kamati mpya za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), uliofanywa juzi, baadhi wakiunga mkono na wengine wakihoji mamlaka ya kufanya hivyo ilhali katiba ikiwa bado haijapitishwa na msajili.

Wengi wa wadau hao wameelezea kufurahishwa na kuachia ngazi kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani, Idd Mtiginjola, na yule wa Kamati ya Uchaguzi, Deo Lyato, wakidai ndizo zilizoibua mgogoro uliosababisha hadi Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), kuingilia kati na kuagiza marekebisho ya katiba.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, mdau John Jambele alisema, Rais wa TFF, Leodegar Tenga, ameanza kukubalika na kufuata haki kimichezo kwa kukubali kujiengua Mtiginjola ambaye alionekana kuharibu soka kutokana na utendaji wake ambao ilifikia hadi kuja kumpinga na Tenga mwenyewe alipomtaka kufanya mapitio ‘Review’ ya wagombea waliokata rufaa.

Alisema ana imani kubwa majaji na mawakili walioteuliwa katika kamati hizo watafanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu, kutokana na kuwafahamu ipasavyo katika utendaji kazi wao, kwani hawawezi kukaa katika magenge na kujadili nani aenguliwe na nani apite wakati hawana vigezo.

“Tenga na kamati yake nawapongeza sana, kwani wamefanya suala zuri sana, kukubali kukaa pembeni kwa Mtiginjola, huyo Lyato yeye ilijulikana tu kwa kuwa sio mwanasheria na kamati yake ya uchaguzi ilihitaji mwanasheria, hivyo basi nina imani watatenda haki hao walioteuliwa sasa, kwa kuwa majaji hao nimekaa nao sana na nawajua,” alisema Jambele.

Naye Michael Wambura alisema kuwa huu haukuwa muda muafaka kwa sasa kutangaza kamati hizo wakati bado marekebisho ya katiba bado hayajapitishwa na Msajili wa Vyama na Klabu za Michezo na hata serikali pia.

“TFF, sijaona haraka waliyonayo, kwani bado katiba haijapitishwa mpaka sasa, wangesubiri kwanza msajili na serikali wakubaliane na marekebisho yao, halafu ndo watangaze hizo kamati zao, kwa mimi bado naona ni ubabaishaji, kwani hata hizo zitakuwa kama yale yale yaliyofanyika mwanzo,” alisema Wambura.

Kwa upande wake, Mussa Peter, aliwataka wote walioteuliwa katika kamati hizo, kutenda haki ili waweze kuwapata viongozi bora hapo baadaye, ambao watasaidia soka hapa nchini kukua na sio ubabaishaji uliopo sasa.

Wakati wadau hao wakinena hayo, Rais wa TFF, Leodegar Tenga, ametoa salamu za shukrani kutokana na utumishi wa Lyato uliotukuka akiwa madarakani.

Akizungumza kwa niaba ya Tenga, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema rais huyo na shirikisho hilo, linapenda kumshukuru Lyato kwa utendaji kazi makini uliochangia maendeleo ya soka nchini na kwamba litaendelea kuyaenzi mema aliyofanya.

Angetile aliongeza kuwa chini ya Lyato, Kamati ya Uchaguzi ilifanya mengi yaliyotukuka katika kusukuma mbele gurudumu la soka, licha ya changamoto kadhaa ngumu, hivyo TFF itaendelea kushirikiana naye kwa sasa atakapokuwa nje ya kamati hiyo.
Kwa upande wake Lyato, hakusita kuushukuru ushirikiano aliopata kutoka kwa Tenga akiwa katika kamati mbalimbali, huku akitoa shukrani kwa wajumbe wote na wadau wengine waliomwezesha kutekeleza majukumu yake vema.

“Nimeridhia mabadiliko yaliyofanywa na kutangazwa na Rais Tenga na kimsingi napenda kumshukuru kila mmoja kwa nafasi yake, katika miaka yangu minane ya kufanya kazi ndani ya kamati tofauti za TFF toka mwaka 2005,” alisema Lyato.

Aliongeza kuwa shukrani zaidi ziwafikie wadau wote wa soka, wakiwamo wajumbe wa kamati za Kuchunguza Mkasa wa Serengeti Boys, Kamati ya Maendeleo ya Taifa Stars, Kamati ya Kuboresha Mapato ya TFF na Kamati mbili za Uchaguzi (2009-11 na 2011-13).

Kamati ya Uchaguzi hivi sasa itakuwa chini ya uenyekiti wa Hamidu Mbwezeleni huku Makamu akiwa ni Moses Kaluwa na wajumbe Mustafa Siani, Hassan Dyamwale na Kitwana Manara.
Kamati ya Rufaa za Maadili itakuwa chini ya Jaji Steven Ihema akisaidiwa na Victoria Makani huku wajumbe ni Mohamed Misanga, Henry Tandau na Murtaza Mangungu, wakati Kamati ya Maadili ni Jesse Mguto mwenyekiti, Francis Kabwe makamu mwenyekiti na wajumbe DCP Mohamed Mpinga, Prof. Madundo Mtambo na Evod Mmanda.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate