EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, August 8, 2013

Bilionea wa madini auawa kwa risasi KIA - - Ni Erasto Msuya.

 ARUSHA.
MFANYABIASHARA maarufu wa madini aina ya tanzanite jijini Arusha, Erasto Msuya, ameuawa kikatili kwa kumiminiwa risasi takriban kumi karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Tukio hilo lililogubikwa na utata wa hali ya juu kutokana na mazingira yake, lilitokea jana mchana eneo la Mijoholoni, wilayani Hai, wakati marehemu akiwa njiani kutokea Arusha.


Habari zilizopatikana jana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, zilisema kuwa mfanyabiashara huyo bilionea alikutwa na mauti hayo akiwa na gari lake la kifahari aina ya Range Rover lenye namba za usajili T 800 CKF.


Hata hivyo, Kamanda Boaz hakuweza kutoa taarifa zaidi  juu ya mauaji hayo kutokana na kile alichodai alikuwa akielekea eneo la tukio na kuahidi kutoa taarifa mara baada ya kurejea kutoka eneo hilo la tukio.


Taarifa zaidi zilidai kuwa Msuya alipigwa risasi na watu wawili waliokuwa wamepanda pikipiki na kupita eneo alilokuwa amesimama nje ya gari lake akizungumza kwa simu.


Baadhi ya marafiki zake jijini Arusha waliokuwa naye muda mfupi kabla ya tukio hilo walidai kuwa alipigiwa simu akiitwa eneo hilo kwa ajili ya kumuuzia madini.


Katika hali inayoacha maswali kuhusu tukio hilo, wauaji hao hawakuchukua kitu chochote kuanzia gari, fedha sh milioni 100 zilizokuwa ndani, simu za mkononi pamoja na ipad.

Mara baada ya kupigwa risasi.
Chanzo chetu cha habari kilidokeza kuwa tukio hilo huenda limepangwa ili kuzima vuguvugu la tuhuma za mauaji ya mchimbaji mmoja aliyeuawa hivi karibuni kwenye machimbo ya Mererani.


Kwa mujibu wa watoa habari walioomba kuhifadhiwa majina yao, sakata la kesi hiyo limekuwa na utata mkubwa kutokana na Jeshi la Polisi mkoani Arusha kutaka kumkumbatia mtuhumiwa wa mauaji hayo, kwa kutomfikisha mahakamani.


Marehemu Msuya anatajwa kama mmoja wa wachimbaji waliokuwa mstari wa mbele kuwashinikiza polisi kuhakikisha kesi hiyo inafikishwa mahakamani ili haki itendeke kwa wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.


Tukio hilo limeanza kuibua hofu miongoni mwa wananchi wa kawaida na wafanyabiashara juu ya kurejea kwa matukio ya ujambazi wa kutumia silaha uliokuwa umepoa kwa muda katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.


Baadhi ya wafanyabiashara waliozungumza na Tanzania Dama jana, wamedai kuwa tukio hilo bado limegubikwa na utata kutokana na mazingira yake, kwani gari la marehemu lilikutwa limeegeshwa pembeni mwa barabara kuu ya Arusha - Moshi kana kwamba kulikuwa na mazungumzo baina ya marehemu na wauaji.

Credit : 2jiachie

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate