EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 14, 2013

Risasi zatikisa Jiji la Mwanza.

 Habari  Sitta Tumma, Mwanza wa Tanzania Daima.
JIJI la Mwanza juzi liligeuka kuwa uwanja wa kivita, baada ya kutokea mashambulizi makali ya risasi baina ya askari polisi na kundi la watu wanaodhaniwa kuwa majambazi yaliyokuwa yakijihami kwa silaha za kivita.

Taarifa zilizoifikia Tanzania Daima Jumatano kutoka eneo la tukio zinaeleza kwamba mashambulizi hayo yaliyodumu kwa takribani dakika kumi yalitokana na kundi hilo la majambazi kutaka kuvamia kituo cha mafuta cha GBP, kilichopo kando kando ya barabara ya Kenyatta, Igogo jijini Mwanza majira ya saa mbili usiku.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, na Naibu Kamishna Ernest Mangu alithibitisha kutokea kwa tukio ambalo inaaminika majambazi hao walikuwa na silaha nzito za kivita. Majambazi watatu waliuawa katika mapambanao hayo.

Alisema polisi walipata taarifa za siri kutoka kwa raia wema dhidi ya majambazi hayo, na walifika eneo la kituo hicho cha mafuta kisha kuyakuta majambazi hayo yakijiandaa kuvamia.

Katika maelezo yake kwa waandishi wa habari, Kamanda Mangu alisema majambazi hayo yalilazimika kujibu mapigo ya polisi kwa kutumia silaha nzito za kivita aina ya SMG na kufanikiwa kuwaua watatu na wengine wakikimbia kusikojulikana.

“Idadi halisi ya majambazi haijafahamika hasa. Maana yalitokea majibizano makali ya risasi. 


Lakini askari walikuwa makini na wakafanikiwa kuyaua matatu na mengine yakakimbia,” alisema Kamanda Mangu.
Alisema katika mapambano hayo polisi walifanikiwa kukamata bunduki moja aina ya 

SMG yenye namba za usajili 2916 pamoja na risasi saba, na kwamba taarifa walizonazo majambazi hayo yanatoka Wilaya ya Ngara mkoani Kagera.

“Baada ya majibizano makali ya risasi, katika eneo la tukio yaliokotwa maganda ya risasi 22. Miili ya hawa jamaa imehifadhiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando,” alisema.
Kufuatia tukio hilo, Kamanda Mangu ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za siri kwa jeshi hilo dhidi ya wahalifu ili wahusika waweze kudhibitiwa kwa mujibu wa sheria.

Katika tukio jingine, watu wasiojulikana wameteketeza kwa moto nyumba tisa za nyasi za familia moja, katika Kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
Kamanda Mangu alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 11, mwaka huu majira ya saa 10 na 12 jioni, na chanzo cha tukio hilo kinadaiwa ni imani za kishirikina.

“Kuna kijana Severine Renatus (14), mwanafunzi wa darasa la saba Shule ya Msingi Nyehunge alipotea kwa muda wa siku nne.

“Baada ya kupatikana kwa mwanafunzi huyo na kuhojiwa na wazazi wake, alisema alifichwa kwenye nyumba hizo, ndipo wazazi walipotoa taarifa kwa sungusungu wa kijiji hicho, ambao waliamua kukusanyika na wanakijiji wengine kisha kwenda kwenye nyumba hizo, na wenye nyumba hizo waliamua kukimbia,” alisema Kamanda Mangu.
Hadi sasa hakuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo, lakini polisi wanaendelea na upelelezi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate