EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 6, 2013

Makada wake wafutiwa shtaka la ugaidi.

KWA mara nyingine Mahakama Kuu, imetupilia mbali mashtaka ya ugaidi yaliyofunguliwa dhidi ya viongozi na wananchama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).


Jana, Mahakama Kuu Kanda ya Tabora iliwafutia shtaka la ugaidi wanachama watano wa CHADEMA ikisema kosa lao ni la jinai na halipaswi kuitwa la ugaidi.

Katika uamuzi wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Simon Lukelelwa, aliwaonya 
waendesha mashtaka kuacha tabia ya kutumia maneno makali ya ugaidi katika kesi za jinai, hatua aliyosema inaogofya wageni wanaotarajia kuja Tanzania.

“Suala hili la ugaidi kwa siku za hivi karibuni limeshika kasi, linazungumzwa kwa mapana ndani na nje ya nchi, lakini inavyoonyesha mazungumzo hayo hayajaeleweka undani wa madhara yake. Nchi ikiwa imekithiri kwa ugaidi kama inavyodaiwa vitu vingi vingeathirika, uchumi, utalii na mambo mengine.

“Ni vizuri mambo haya yakapewa nafasi yake na kwa umakini mkubwa, yasije yakaleta madhara kwa nchi pasipo ulazima wowote. Hata neno ugaidi tafsiri yake haijajulikana vizuri, kila mtu anatafsiri zake. Mtu unayemuona ni gaidi, anaweza kuwa mpigania uhuru kwa mwingine,” alisema Jaji Lukelelwa.

Hii ni mara ya pili kwa Mahakama Kuu kufuta mashtaka kama hayo kwa viongozi wa CHADEMA ambapo Mei 8, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ilimfutia mashtaka matatu ya ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama hicho, Wilfred Lwakatare.

Jaji Lawrance Kaduri alitoa uamuzi huo akisema ulitokana na kukubaliana na hoja ya mawakili wa Lwakatare, Tundu Lissu, Peter Kibatara na Mabere Marando.

Makada hao wa CHADEMA waliofutiwa shtaka hilo la ugaidi jana mkoani Tabora ni Henry John Kilewo, ambaye ni Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Kinondoni, Evodius Justinian, Oscar Kaijage, Rajabu Daniel na Seif Magesa Kabuta.

Vijana hao walipandishwa kizimbani katika mahakama ya wilaya ya Igunga na kusomewa mashtaka mawili, moja la ugaidi na lingine la jinai.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mawakili wao, Peter Kibatala na Profesa Abdallah Safari walipambana kuwanusuru na mashtaka hayo.

Mawakili hao walihoji uhalali wa mashtaka hayo, wakidai kuwa hakuna vigezo vya kutosha kuonyesha kuwa kuna ugaidi, huku pia wakihoji utaratibu wa kuwafungulia mashtaka katika mahakama hiyo badala ya kule walikokamatiwa.

Hivyo, waliiomba Mahakama Kuu ama iwafutie mashtaka hayo au iamuru kila mshtakiwa arudishwe na kushtakiwa katika mahakama za mahali walikokamatiwa.

Katika uamuzi wake, Jaji Lukelelwa aliongeza kuwa sheria za makosa ya jinai zipo wazi na zinaelekeza na kufafanua makosa na mashtaka yanayoweza kufunguliwa kwa wananchi wanaokwenda kinyume cha sheria zilizotungwa.

Jaji aliamru watuhumiwa hao warejeshwe wilaya ya Igunga walikotenda makaosa yao na wafunguliwe shtaka la kufanya matendo ya kusababisha madhara makubwa mwilini kwa kuzingatia sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.

Aliongeza kuwa hakimu atakayesikiliza shauri hilo awape dhamana kwa kutoa masharti atakayoona yeye yanalingana na shtaka linalowakabili watuhumiwa.

Wakili wa washtakiwa hao, Peter Kibatala, akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama na kumshukuru jaji kwa kupitia marejeo yao waliyoomba na kuyatolea maamuzi.

Awali wananchama hao watao wa CHADEMA kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini walikuwa wanatuhumiwa kwa makosa mawili likiwemo la ugaidi kwamba walimteka na kummwagia tindikali raia mkazi wa mjini Igunga.

Katika shtaka la kwanza walishtakiwa chini ya Sheria ya Kuzuia Ugaidi, wakidaiwa kumteka kwa nia ya ugaidi Mussa Tesha huko Igunga, Tabora na la pili wanashtakiwa chini ya Sheria ya Kanuni za Adhabu wakidaiwa kumdhuru Tesha kwa kummwagia tindikali.
Walidaiwa kutenda makosa hayo mwaka 2011, wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga.

Upande wa mashtaka uliongozwa na wakili wa serikali, Juma Masanja, akisaidiana na wakili mwingine wa serikali, Idelfonce Mukandara, waliodai mashtaka hayo ni halali.
Credit: Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate