EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 6, 2013

Wasanii wa Bongo Fleva na baadhi ya watangazaji wa Bongo ambao mwishoni mwa wiki iliyopita walikusanyika kwenye futari hiyo ikulu.

NI msimu wa futari ambao unaelekea ukingoni mwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani! Baadhi ya mastaa wa Bongo Fleva na filamu wamepata mwaliko wa futari kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alijiachia nao ikulu.
Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Msanii Zuwena Mohamed a.k.a. Shilole.
Walianza wasanii wa Bongo Fleva na baadhi ya watangazaji wa Bongo ambao mwishoni mwa wiki iliyopita walikusanyika kwenye futari hiyo ikulu iliyopo maeneo ya Magogoni, Dar.
Baadhi ya wasanii wakifuturu kwa Snura.
Wakiwa ikulu, mastaa hao waligonga mnuso wa maana pamoja na kwamba siyo wote walioalikwa walikuwa wamefunga.
 
Baadaye JK aliwapa neno la kuwatia moyo kuendelea kufanya muziki mzuri utakaopendwa na watu wote na wa kimataifa.
JK aliwahakikishia kuwa huwa anasikiliza muziki wao hivyo waongeze bidii.
Rais Kikwete akimpa tano Msanii Mkongwe wa Bongo Fleva, Gwamaka Kaihula a.k.a King Crazy G K.

JK AGONGA TANO!
Pia JK, sambamba na First Lady, Salma Kikwete walionekana wachangamfu huku prezidenti ‘akipewa tano’ kama sehemu ya swaga kutoka kwa baadhi ya wasanii kama Gwamaka Kaihula ‘Crazy GK’.

Kidogo tu kadosari kalitaka kujitokeza kwa vazi alilotinga Shilole kwani lilikuwa ‘transiparenti’ kiasi cha kuonesha rangi ya sidiria na ‘vifuu’ vyake kifuani.
 
Baadhi ya mastaa walioalikwa ni pamoja na prodyuza P- Funk, Lamar, AY, TID Mnyama, Marlaw, Chegge, Hemedy, Shilole, Mwasiti, Ali Kiba, Jafarai, Aslay, Fella, Ferouz, Z-Anto, Madee, Keisha, Nay wa Mitego, Linex na wengine wengi huku wale wa filamu wakialikwa kwenye futari Jumamosi iliyopita.
Mastaa wa kike wakipata futari kwa Snura.
MASTAA WALIOFUTURU KWA SNURA WANAHITAJI BAKORA
Wakati huohuo, Ijumaa iliyopita staa wa muziki na filamu za Kibongo, Snura Mushi naye alifuturisha nyumbani kwake lakini kukawa na dosari moja kubwa.
Katika futari hiyo iliyoendana na kumpongeza mtoto wa Snura kwa kufikisha miaka 3, iliyofanyika nyumbani kwake Mwananyamala, Dar, baadhi ya mastaa waliohudhuria wanahitaji kutandikwa bakora kwa kitendo walichokifanya.
Baadhi ya mastaa hao walikula futari na dakika chache baadaye walihamia baa iliyopo jirani na nyumbani kwa staa huyo kisha wakaanza kutandika bia ili kushushia futari, jambo ambalo ni kinyume na taratibu za mfungo.
Walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa suala hilo ni sawa na kukejeli au kumkufuru Mwenyezi Mungu kwani inajulikana kuwa futari ni chakula kinacholiwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani lakini kwa upande wa mwigizaji na msanii wa Bongo Fleva, Isabela Mpanda na wenzake waliokaa baa waliona ni kitendo cha kawaida.
Isabela na wenzake wakigonga bia baada ya futari.
“Unajua hawa mastaa wanakufuru sana, nini maana ya kufuturu ‘theni’ unahamia baa kunywa pombe? Hiki ni kitendo kibaya sana wamemdhalilisha mwenzao aliyewaalika, unadhani atajisikiaje akipewa taarifa kuwa wapo nje wanakunywa?
“Wameona baa wameshindwa kuvumilia, hii ni tabia mbaya mno,” alisema msanii mmoja ambaye hakutaka jina lipambe ukurasa huu.
Mbali na Isabela, wengine walionaswa baa dakika chache baada ya kufuturu kwa Snura ni pamoja na Jacqueline Pentzel na shosti wake (Mariam), msanii mmoja wa komedi na chipukizi wa filamu.
Mbali na kukaa baa, Jack na Mariam  walikuwa wakirushiana vijembe mbele ya watu kitendo ambacho kilionesha wazi kuwa si sahihi kwa watu kugombana eneo la kufuturu kulingana na mwezi kwani unahitaji stara.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate