EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 10, 2013

Wagonjwa Muhimbili wahaha.

 Habari na Tanzania Dima
MASHINE ya Magnetic Resonance Ination (MRI) inayotumika kupima magonjwa mbalimbali katika mfumo wa fahamu imeharibika kwa zaidi ya siku nne na kusababisha usumbufu mkubwa.

Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumamosi, umebaini kuwa wagonjwa wengi waliohitaji huduma hiyo wameshindwa kuipata kutokana na kuharibika kwa kifaa hicho muhimu cha kupima na kutambua magonjwa mbalimbali katika ubongo, uti wa mgongo na kifua.

Akizungumza kwa niaba ya mgonjwa wake, Joshua Shaka, alisema kuwa wamekuwa wakihangaika kutafuta huduma hiyo kwa siku nne mfululizo bila mafanikio baada ya kuelezwa kuwa mashine hiyo imeharibika.

Alisema kuwa kuna umuhimu wa serikali kuangalia namna ya kuagiza mashine mpya kwa kuwa iliyopo imekuwa ikiharibika mara kwa mara.

“Hii mashine sio mara ya kwanza kuharibika; unaweza kuja leo ukaambiwa inafanya kazi lakini baada ya muda mfupi inashindwa kuendelea na kazi …inawezekana ni kutokana na uchakafu,” alisema.

Alisema kuwa mashine hiyo ndiyo inayotoa huduma kwa hospitali zote za serikali kwa jiji zima la Dar es Salaam hivyo hatua ya kuharibika mara kwa mara imekuwa ikisababisha kuwepo kwa mlundikano wa wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo.

“Hata hiyo mashine ya CT SCAN inayosemekana ipo hivi sasa nayo haina filimu hivyo unapopigwa unashindwa kupewa majibu hapo hapo jambo linalozidi kumfanya mgonjwa azidi kuumwa zaidi maana anategemea aje hospitali apate huduma,” alisema.
Tanzania Daima Jumamosi, katika uchunguzi wake, lilidhihirishiwa uharibifu wa mashine hiyo na baadhi ya wahudumu waliokutwa hospitalini hapo.

“Mashine ni mbovu kama mnataka huduma labda mniache simu zenu kama itapona wiki ijayo nitawapigia ili muweze kumleta mgonjwa wenu kuliko mje tena mkute mashine haifanyi kazi mtakuwa mnamchosha mgonjwa wenu bure,” alisema mmoja wa wahudumu waliokuwepo.

Ofisa uhusiano wa hospitali hiyo, Aminieli Aligaesha, hakupatikana baada ya ofisi yake kufungwa kwa muda mrefu, na hata alipotafutwa kwa njia ya simu yake ya kiganjani nayo iliita mara nyingi na kwa muda mrefu bila majibu.
Hata hivyo Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Nsachris Mwamaja, alikiri kuharibika kwa mashine hiyo na kusema kuwa wamemaliza kukitengeneza jana na kwa sasa kinafanyakazi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate