Na Mashaka Mhando,Korogwe
DADA wa Mwenyekiti wa Chama Cha 
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amefariki papo hapo 
baada ya gari alilokuwa akiendesha kupasuka tairi ya mbele na kuingia 
chini ya daraja baada ya kupinduka na kusababisha watu wawili kufa na 
wengine watatu kujeruhiwa vibaya.
Dada 
huyo, Grace Aikaeli Mbowe,  anayesadikiwa kuwa na umri kati ya miaka 47 
hadi 50, alikuwa akiendesha gari yenye namba T 277 CAJ aina ya Toyota 
Cresta akiwa na mumewe  aliyefahamika kwa jina la Ibrahim Lukindo (52), 
wakitokea Jijini Tanga, walipata ajali hiyo eneo la Kabuku wilayani 
Handeni.
Kamanda
 wa polisi mkoani Tanga (ACP) Costatine Massawe alisema kupitia Ofisa 
wake wa upelelezi mkoani Tanga, Bw Aziz Kimata, kwamba
 ajali hiyo ilitokea majira ya saa
 1:30 leo asubuhi  katika eneo hilo baada ya gari hilo kupasuka tairi ya
 mbele kulia na kisha kuingia chini ya daraja lililokuwepo eneo hilo.
"Ni kweli
 kuna ajali ilitokea eneo la Kabuku gari aina ya Cresta lililokuwa 
likiendeshwa na ndugu inavyosemekana wa Bw Freeman Mbowe, limepata ajali
 baada ya kupasuka tairi la mbele na kuacha barabara na kuingia chini ya
 daraja dereva anayeitwa Grace Aikael Mbowe na mtu anayesemekana ni 
mumewe anayeitwa Ibrahim Lukindo, wamefariki na watu watatu 
waliowachukua wamejeruhiwa," alisema RCO Kimata.
Aliwataja
 waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na Bw Ridhiwani Bakari (29) aliyekuwa na 
mkewe Zeddy Nzuke (29) raia wa Kenya aliyekuwa na mtoto wake mwenye umri
 wa miaka miwili na miezi minne aliyefahamika kwa jina la Mariam 
Ridhiwan ambao kwa sasa wamelazwa katika hospitali ya Magunga wilayani 
Korogwe.
RCO
 Kimata aliyezungumza kwa niaba ya kamanda huyo wa polisi alisema chanzo
 cha ajali hiyo inasemekana kimetokana na kupasuka kwa mpira huo na 
mwendo kasi wa kawaida na kwamba majeruhi na maiti zi9mehifadhiwa kwenye
 hospitali hiyo.
Mwandishi
 wa habari hizi, aliyefika kwenye hospitali hiyo na kuzungumza na 
Ridhiwani pamja na mkewe ambaye amelazwa wodi namba mbili ya wanawake 
katika hospitali hiyo, alisema kwamba ndoto zake za kufanya kazi Dar es 
salaam zimezimika ghafla kutokana na kwamba alikuwa aende kupamba kazi 
ya uofisa ugavi katika taasisi moja ya fedha ya marehemu Mbowe Jijini 
Dar es salaam.
"Nilikuwa naenda kupewa kazi na mama Mbowe katika Institution yake ya 
Micro-Financial Jijini Dar es salaam, mimi ni procurement 
(Mgavi-manunuzi) na ni Mkenya kwetu ni Eastern Province Kang'undo na 
nimeolewa na bwana Mtizedi...Lakini sasa ndoto zangu za kufanya kazi Dar
 es salaam zimezimika ghafla," alisema Zeddy akiwa kitandani amelala na 
mwanwe ambaye alikuwa haongei tangu amefika katika hospitalini hapo.
Mumewe na mwanamke huyo akizungumzia ajali hiyo alisema kuwa hakuwa 
akijua kwani alikuwa amelala dakika tatu kabla ya kutokea ajali hiyo 
ambapo alishtukia yeye, mkewe na mwanawe wametupwa chini kwenye majani 
wakiwa hawajijui na walikimbizwa katika hospitali hiyo ya Korogwe.
Ridhin ambaye ni mkazi wa Nguvumali Jijini Tanga, alisema safari yao 
hiyo ilikuwa ifanyike Jumamosi mchana lakini kutokana na na kuchelewa 
kwa wenyeji wao hao, waliondoka Tanga kwenye hoteli ya Doliphin 
walikolala majira ya saa 11:00 alifajiri kwa ajili ya kwenda Jijini Dar 
es salaam.
Muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo Bi Nayela Missingo alikiri kuwapokea 
wagonjwa hao ambapo alisema wanafanya jitihada za kuwahamishia katika 
hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam mtoto Mariam ambaye 
amepata majeraha katika kichwa chake na kwamba tangu afikishe hospilaini
 hapo hakuwa katika hali nzuri, haongei walakunyonya.
  Bi Zeddy Nzuke  na mtoto wake wakiwa wamelazwa katika hospitali ya 
Magunga wilayani Korogwe baada ya kupata majeraha katika ajali hiyo.
| Muuguzi wa zamu katika hospiotali ya magunga wilayani Korogwe Nayela Missingo akimsaidia kukaa kwenye kitanda Bw Ridhiwani Bakari baada kuopata ajali hiyo | 
 
 
 
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment