EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 27, 2013

Madiwani Bagamoyo waishukia Tasaf..watumikisha wananchi kazi za miradi mbalimbali huku fedha wakichukua wao.

Habari na Zawadi Chogogwe wa Tanzania Daima.
MADIWANI wa Halmashauri ya Bagamoyo, mkoani Pwani, wamelaani kitendo cha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kufika katika vijiji vya Bagamoyo na kuwatumikisha wananchi kazi za miradi mbalimbali huku fedha wakichukua wao.

Madiwani hao waliibua hayo mjini Bagamoyo juzi katika kikao cha baraza la madiwani cha robo ya nne ya mwaka 2012 na 2013 kilichofanyika katika ofisi za mkurugenzi wa halmashauri hiyo ambacho kilihudhuriwa na wataalamu mbalimbali.

Diwani wa Kilomo, Hassan Usinga, alisema Tasaf wamekuwa na tabia ya kutofika kwa watendaji wa vijiji pindi wanapofanya kazi zao za miradi na badala yake wanaenda moja kwa moja kwa wanakijiji na kuwatumikisha katika miradi ya maendeleo huku wakiwalipa fedha kidogo.

“Kitendo cha kwenda kwa wanakijiji kuwafanyisha kazi na kuwalipa fedha kidogo kumechangia miradi mingi kuwa mibovu huku mingine ikiwa imekufa kama vile miradi ya kuku,” alisema Usinga.

Alisema taarifa za maendeleo ya vijiji zinaonyesha kuwa dawa za mifugo na matumizi zimetolewa kwa wanakijiji na kueleza kuwa taarifa hizo zikiwa hazina ukweli.

“Kutowashirikisha watendaji wa vijiji katika mikutano ya maendeleo kumepelekea kukosa wanakijiji wengi kushiriki katika mikutano yao,” alisema.

Alisema wanaoshiriki wanakuwa wachache hali inayowafanya Tasaf kuwavalisha fulana na kofia huku wakiwapiga picha na kuzipeleka kwa wafadhili kwa kuonyesha ushahidi kuwa wanakijiji wameshiriki mkutano huo wakati sio kweli.

Aliongeza kusema sh milioni 27 zilitengwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara za 
 Tukamisasa kwenda Mbuyu, katika kata ya Ubena lakini cha kushangaza barabara hiyo haijajengwa kwa kiwango kutokana na wananchi kulazimika kuitengeneza kwa majembe baada ya kuona hakuna juhudi zozote za mamlaka husika.

“Tunaiomba Tasaf iache kutuchezea mchezo mchafu sisi watu wa Bagamoyo kwa kuwatumia wanavijiji kwa manufaa yao wenyewe,” alisema.
Wakati huohuo, madiwani hao walilalamika kuwa watumishi wa halmashauri hiyo hawana nyumba za kuishi za kiofisi, hali inayowafanya waishi katika nyumba za kupanga.

Akizungumza katika kikao hicho, Diwani wa Fukayosi, Ally Issa, alisema inatia aibu kuona watumishi wa Halmashauri ya Bagamoyo wakiishi katika nyumba za kupanga badala ya nyumba za kiofisi.

“Halmashauri inakusanya mamilioni ya fedha lakini inashindwa kuwajengea watumishi wake nyumba za kuishi. Mkurugenzi acha mambo ya siasa tunachotaka ni kuona nyumba za watumishi zinajengwa na kukabidhiwa,” alisema Issa.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Samwel Sariaga, alisema katika bajeti ya mwaka huu watajenga nyumba nne za watumishi ambazo kila moja itagharimu sh milioni 40.

Katika hatua nyingine, madiwani hao wametishia kuiburuza Bima ya Afya mahakamani, kwa kitendo cha kuwakata asilimia 5 kila mwezi ndani ya miaka mitatu bila kuwapatia kadi za matibabu.

Diwani wa Viti Maalum, Hapsa Jumam, alisema wakati wanaingia madarakani waliahidiwa watapewa kadi za matibabu, lakini cha kushangaza mpaka sasa hawajapewa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate