SWALI la nani atatwaa taji la Miss Universe Tanzania 2013, 
linatarajiwa kupata jibu leo wakati warembo 15 kutoka mikoa mbalimbali 
ya Tanzania watakapochuana kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, mkabala
 na IFM jijini Dar es Salaam kuanzia saa moja kamili usiku.
Warembo hao mbali ya kuwania taji la Miss Universe Tanzania, ambalo 
kwa sasa linashikiliwa na Winfrida Dominique, pia watawania taji la Miss
 Earth Tanzania na kupata tiketi ya kuiwakilisha nchi katika mashindano 
ya kimataifa.
Warembo hao kwa nyakati tofauti, wamekuwa wakitambiana huku kila mmoja
 akijigamba kutwaa taji hilo na kuiwakilisha nchi katika mashindano ya 
dunia yaliyopangwa kufanyika jijini Moscow, Russia Novemba 9.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications inayoandaa mashindano 
hayo, Maria Sarungi, alisema kuwa kila kitu kimekamilika na warembo 
wamepania kufanya makubwa jukwaani, ambapo warembo wote wana ari ya juu 
na kila mmoja akiwa na shauku ya kutwaa taji hilo.
“Kwa upande wetu, kila kitu kiko tayari, warembo wamejiandaa vilivyo 
na tumeandaa shoo bora na fupi, hivyo mashabiki wa masuala ya urembo 
wanatakiwa kufika mapema ili kuona nani anatwaa taji na kupata tiketi ya
 kuiwakilisha nchi kimataifa,” alisema Maria.Warembo watakaochuana leo 
ni Aziza Victoria, Irene Nsiima, Betty Boniface, Kundi Mlingwa, Mariam 
Ngwangwa, Naomi Kisaka, Glady Msemo, Salsha Lukiko, Upendo Dickson, 
Vestina Mhagama, Angela Lutataza, Consolata Mosha, Clara Noor, Agnes 
Thobias, Dinah David na Clara Noor.
 
 
 
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment