EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, October 7, 2013

Serikali yapongeza Tamasha la Pasaka.

SERIKALI kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), imewapongeza waandaaji wa Tamasha la Pasaka, Kampuni ya Msama Promotions kutokana na ubora wake mwaka huu na kuwataka kuendeleza mipangilio hiyo.

Akizungumza katika mkutano wa kupokea ripoti na kutathimini tamasha la mwaka huu lililofanyika kwenye mikoa mitano hapa nchini, Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa wa Basata, Nsao Shalua, alipongeza jitihada na mipango inayofanywa na Msama katika kuliendeleza tamasha hilo.

Shalua aliongeza kuwa michango inayotolewa na kampuni hiyo kwa jamii kupitia matamasha hayo ni mfano wa kuigwa na kuwasihi wadau wengine kushiriki na kuchangia katika kutunisha mfuko wa matamasha ya Pasaka.

Naye Ofisa Sanaa Mkuu, Philemon Mwasanga, alitoa wito kwa kampuni hiyo chini ya Mkurugenzi wake, Alex Msama, mbali ya kujenga kituo cha kulea watu wenye uhitaji maalumu ambao ni wajane, walemavu na yatima kitakachokuwa nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, wawe na mkakati maalumu wa kuvumbua na kuibua wasanii wachanga katika tasnia ya muziki wa injili hapa nchini, kwa sababu muziki wa sasa umemezwa na teknolojia.

Mwasanga aliwataka waandaaji hao kuazimia kuanzia mwakani, kuacha matumizi ya CD wawapo jukwaani ili kuuokoa muziki ambao unapoteza mwelekeo wake hasa kimataifa.

Aidha, Mwasanga alitumia fursa hiyo kumsihi Msama kununua vyombo vyake vya muziki ili kufanikisha matamasha yake ili waimbaji waonyeshe vipaji vyao katika tasnia ya muziki.

“Ili kuendana na kasi ya muziki katika hadhi ya kimataifa, unaweza kutakiwa nchi za wenzetu, ili ukidhi inatakiwa kujipanga kimataifa katika utayarishaji na sio matumizi ya (mshindo nyuma) CD,” alisema.

Mwasanga alisema mtindo huo umepitwa na wakati, waimbaji wanatakiwa wajizoeze kumiliki jukwaa kwa kuimba na kupiga moja kwa moja.

Kwa upande wake, Ofisa Matukio wa Basata, Kurwijira Maregesi, alisema matamasha yajayo yawe ni mfano wa kuigwa kinidhamu na muonekano wa mavazi kwa waimbaji.

Maregesi alisema waimbaji wanaume wajiepushe na uvaaji wa hereni masikioni, kusuka nywele na kuvaa suruali chini ya makalio, kwa kuwa muziki wa injili unamtukuza Mungu.

Ili kunogesha tamasha lijalo, Ofisa wa Basata, Vick Temu alipendekeza kuwepo kwa ‘Projector’ zitakazofungwa uwanjani ili kuwapunguzia bughudha watazamaji watakaoukuwa mbali na jukwaa kuu.

Kamati ya Maandalizi ya Tamasha hilo kupitia Makamu Mwenyekiti wake, Abihudi Mang’era, ilitoa pongezi kwa Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ambayo matamasha yalifanyika, licha ya fununu za matishio ya ugaidi zilizosambazwa.
Mang’era alisema tamasha lijalo litakuwa la kimataifa zaidi, kwa sababu litaongeza idadi ya mikoa na waimbaji wa kimataifa. Kwamba lina malengo ya kuvuka mipaka ya Tanzania na kuingia nchi za jirani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate