EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, November 14, 2013

DIAMOND, PENNY NI NDUGU...MAAJABU!

Maajabu! Jambo zito limefichuka kuwa mastaa walio katika uhusiano wa kimapenzi, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Penniel Mwingilwa ‘Penny’ ni ndugu, AMANI limepekua na kupata mkanda kamili.
Diamond kwa sasa ndiye mwanamuziki aliye matawi ya juu zaidi kuliko yeyote kwenye Bongo Fleva, akisumbua vibaya na kibao chake cha Number One wakati Penny akiingiza mkwanja kupitia utangazaji katika kituo cha Runinga ya Dar es Salaam ‘DTV’.

ISHU YABUMBURUKA!
Sosi wa karibu, ndani ya familia ya Diamond alinyetisha kwamba, Diamond na Penny ni ndugu wa damu lakini jambo hilo limefahamika hivi karibuni na hivyo wanahaha namna ya kuzima aibu hiyo.



 Penny
Kwa sharti la kutochorwa sosi huyo alisema: “Ndugu kwenye familia wanagongana. Wanajaribu kufichaficha hili jambo, lakini inashindikana. Unajua kinacholeta shida zaidi ni kwamba Diamond na Penny watakavyokuwa baada ya uamuzi kupitishwa.”
 
Alisema, pamoja na ukweli huo kugundulika bila shaka kuwa ni ndugu, bado kuna ugumu wa wapenzi hao waliozama kwenye dimbwi la mahaba kisha kuvunja amri ya sita, kuachana na kubaki wakiheshimiana kama kaka na dada.
“Tatizo ni je, Diamond atakubali kumchukulia Penny kama ndugu yake? Kama atakubali na Penny naye atakuwa tayari? Wote kwa pamoja wanaonekana kama wanapingana na jambo hilo,” alisema.
 
UNDUGU WENYEWE UKOJE?
Akieleza aina ya unasaba wa Diamond na Penny, sosi wetu huyo alisema, bibi mzaa mama wa Diamond na bibi mzaa mama wa Penny, wamezaliwa na mama mmoja.
Hapa anafafanua: “Kwa sababu hiyo sasa, unaweza kuona kuwa, wale ni sawa tu na mtu na kaka yake. Tena wako ndani ya ukoo kabisa, sema hao mabibi, kila mmoja alikuwa na baba yake, walichangia mama tu.
“Familia imejiridhisha kabisa, halafu isitoshe imeonekana kuwa, undugu wa kuchangia mama ndiyo wa uhakika zaidi kuliko wa baba ambao mtu anaweza kubambikwa hata mtoto asiye wake. Kifupi Penny na Diamond ni ndugu. Sema ndiyo hivyo historia za wazazi wao zinashangaza mpaka basi.”
Kwa mujibu wa sosi wetu, majina ya bibi hao wanaounganisha undugu ni Khadija Said Abas (bibi yake Penny) na Tatu Omar (bibi yake Diamond), wote kwa sasa wametangulia mbele ya haki.

MAMA DIAMOND ACHEKELEA
Wakati jambo hilo likileta msuguano wa kimyakimya ndani ya familia huku wengi wakitaka undugu huo uheshimiwe na uhusiano uvunjwe kabisa, imeelezwa kuwa mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ anafurahia undugu huo.
“Kinachoshangaza sasa, mama Diamond amefurahi sana na amezidisha mapenzi yake kwa Penny, ndiyo maana hataki kusikia mwanaye anakuwa na mwanamke mwingine zaidi ya Penny.
 
“Mwenyewe anasema, kwanza undugu siyo wa karibu sana hivyo haina madhara lakini pia anajua Diamond atampenda, kumheshimu na hatamnyanyasa kwa sababu ni sehemu ya damu ya familia yao,” sosi aliendelea kutiririka.
HAPA AMANI, KULE DIAMOND
Amani lilifanya juhudi za kumsaka Diamond katika simu zake zote za mkononi bila mafanikio, likahamia kwenye mitandao ya kijamii, likamnasa ambapo awali mahojiano yalikuwa na kigugumizi lakini baadaye mambo yalikuwa hivi;
AMANI: Mzee vipi, mbona hupatikani kwenye simu zako zote? Kuna jambo nataka kukuuliza bwana mkubwa.
DIAMOND: Niko Nigeria. Vipi, kuna nini tena?
AMANI: Kuna stori fulani... eti ni kweli bibi yake Penny mzaa mama na bibi yako wewe ni ndugu wa damu kwa maana wamezaliwa na mama mmoja?
DIAMOND: Yeah but wamechangia mama, kila mmoja na baba yake.
AMANI: Kwa hiyo Penny ni dada yako kiasili si ndiyo?
DIAMOND: Yap!
AMANI: Duh! Majanga... kwa hiyo unatembea na dada yako wa damu?
DIAMOND: Nilikuwa najua basi kaka?!
AMANI: Kwa hiyo sasa baada ya kugundua hivyo, unaachana naye au?
DIAMOND: Kama nilivyokuambia, niko Nigeria... halafu niko gym sasa hivi, nitakutafuta nikitoka.
AMANI: Sawa, naomba ujibu hili swali la mwisho. Tumesikia kuwa, mama yako anampenda sana Penny, ni kwa sababu amegundua kuwa una undugu naye?
DIAMOND: Ha! Ha! Ha! Nikitoka gym nitakupigia simu tuzungumze vizuri.
Diamond hakufanya hivyo. Hata alivyotafutwa baadaye kwenye mtandao huo, pia hakuonekana kuwa hewani.

PENNY MIKONONI
MWA AMANI
Penny alipopatikana juzi Jumanne, kwa njia ya simu alielezwa ilivyo ambapo alisema: “Ni kweli Diamond ni ndugu yangu wa damu. Tumegundua tukiwa tayari tumeshakuwa wapenzi.
“Hakuna jinsi tena, sanasana naona kama mapenzi yetu ndiyo yamezidi kuimarika. Nampenda sana Diamond wangu na sababu hiyo haitoshi kututenganisha maana kama ni makosa tayari yameshatokea.”

MAMA DIAMOND
Kwa upande wake mama Diamond, baada ya kusimuliwa kila kilichofika mezani mwa Amani na kutakiwa kueleza msimamo wake alijibu kwa kifupi: “Ndiyo ni kweli unayosema, lakini kwa sasa nipo huku Kariakoo (Dar), sipo kwenye nafasi nzuri ya kuzungumza. Njoo nyumbani jioni, tuzungumze vizuri.”
Diamond na Penny wamekuwa kwenye penzi lenye kasheshe nyingi kufuatia mwanamuziki huyo kuhusishwa na wanawake wengine akiwemo aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Wema Isaac Sepetu.
CHANZO CHA HABARI NI GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate