EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 26, 2014

FLORA AKOMBA KILA KITU


Stori: Waandishi Wetu
MACHOZI upya! Habari halali kwa ubongo wako zinaeleza kwamba wakati mumewe, Emmanuel Mbasha (32) alipokuwa mahabusu, Dar kati ya Juni 15 hadi 17, mwaka huu, staa wa Gospo Bongo, Flora Mbasha (31) anadaiwa kwenda nyumbani na kukomba vitu vya ndani kuvipeleka kusikojulikana.
Sehemu ya chumba cha kupumzikia kilichobakiwa na kochi na zulia.
Ilisemekana kwamba wakati hayo yakiendelea, Mbasha alikuwa nyuma ya nondo za Mahabusu ya Keko jijini Dar es Salaam ambako alishikiliwa.
Kwa mujibu wa mtu aliyeambatana na Mbasha alipopata dhamana dhidi ya kesi yake inayomkabili ya ubakaji wa shemejiye mwenye umri wa miaka 17, alipofika nyumbani kwake Tabata-Kimanga, Dar alipigwa butwaa kukuta hakuna vitu ndani!
Chumba kingine kilichosafishwa kabisa bila ya samani yoyote.
Habari zilidai kwamba alipowauliza majirani kama walimuona mtu akiingia ndani walimwambia mkewe (Flora) ndiye alikuwa akiingia na kutoka mara kwa mara.
Ilielezwa kuwa vitu hivyo vilihamishwa Juni 16 ambapo Mbasha alitoka mahabusu Juni 17, yaani siku moja tu.

KITANDA CHA BEI MBAYA
Baadhi ya vitu vilivyodaiwa kuchukuliwa nyumbani hapo ni kitanda cha bei mbaya walichokuwa wakilalia kwenye chumba cha baba na mama huku akimwachia neti ikiwa inaning’inia.
SUTI ZA MAREKANI
Vingine ni makochi huku akibakisha sofa ndogo ya mtu mmoja, vitu vyote jikoni na nguo (suti za bei mbaya, walizonunua wakati wakiwa Marekani).
Pia alidaiwa kukomba vile vidani vyote vya dhahabu.
Mwandishi wa Global Bw. Harun Sanchawa akipata undani wa habari kutoka kwa baba mzazi wa Emmanuel Mbasha, mzee Maneno.
ZAIDI YA MIL. 13
Ukiacha zile hati za nyumba, viwanja na mashamba, gharama ya vitu vyote vilivyochukuliwa ndani ni zaidi ya Sh. milioni 13 za Kitanzania (kama zile ambazo Wema Isaac Sepetu alizomlipia Kajala Masanja asiende jela).
AMWAGA CHOZI
Baada ya kukutana na mazingira ya aina hiyo, lilikuwa ni pigo lingine zito kwa Mbasha ambaye alijikuta akimwaga chozi kwa mara nyingine kwa sababu ya mkewe Flora aliyedumu naye katika ndoa kwa takriban miaka 12.
Ilidaiwa kuwa, Mbasha aliumia kupita kiasi huku akiomba Watanzania waone ubaya aliotendewa.
Bw. Harun Sanchawa akihojiana na mama mzazi wa Emmanuel Mbasha.
AMANI LAPEKUWA CHUMBA HADI CHUMBA
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, Amani lilifika nyumbani hapo ambapo lilipata mwanya wa kuingia ndani ya nyumba hiyo kisha kupekuwa chumba hadi chumba na kujionea kulivyokuwa kweupe huku madirishani mapazia yakiendelea kubembea kwa upepo mkali uliopo Dar kwa sasa.
Kimuonekano, nyumba hiyo ilikuwa kama kuna familia ilihama hivyo inahitaji kupangishwa au kuhamiwa na mwingine.
Bw. Emmanuel Mbasha.
MBASHA ANASEMAJE?
Alipotafutwa Mbasha kuzungumzia ishu hiyo alikiri kukuta hali hiyo nyumbani kwake baada ya kupata dhamana.
“Nilipofika nyumbani kwangu nilikuta ufunguo wa nyumba kwa majirani. Niliwauliza kama kulikuwa na mtu anaingia nyumbani nikaambiwa ni Flora. Kama mnavyoona kuna vitu vingi vya ndani havipo,” alisema Mbasha.
Alipoulizwa kama ana uhakika kuwa mhusika ni Flora, Mbasha alisema  yeye alikuta nyumba nyeupe.
 Jitihada za kumpata Flora hazikuzaa matunda kwani simu yake ya kiganjani haikuwa hewani juzi Jumanne mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni.
Flora Mbasha.
TUMEFIKAJE HAPA?
Kabla ya Mbasha kukabiliwa na kesi hiyo ya madai ya ubakaji wa ndugu wa Flora, Mei 23 na 25, mwaka huu, tayari kulikuwa na mgogoro wa ndoa. Flora alishaondoka nyumbani na kwenda kuishi hotelini maeneo ya Sinza jijini Dar.
NINI KINAENDELEA?
Wakati kesi ya ubakaji ikiendelea kwenye Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar huku Mbasha akiwa nje kwa dhamana, kuna jitihada zinazoendelea ili warudiane kwani kashfa hiyo inashusha upako wa huduma yao kwa jamii huku wote wakiwa tayari kwa suluhu.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate