EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 7, 2014

Kila Kombe, Maximo kulamba Sh 19m Yanga

Kocha Mbrazili, Marcio Maximo.

WAKATI ujio wa Kocha Marcio Maximo ukiwa njiani kukamilika, ambapo mpaka sasa ni asilimia 95, klabu ya Yanga ipo tayari kumpa mamilioni kila atakapofanikiwa kubeba taji.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zinaeleza kuwa pamoja na gari la kutumia na nyumba ya kuishi, Mbrazili huyo amepewa ofa ya dola 12,000 (Sh milioni 19) kila atakapobeba ubingwa wa Tanzania Bara au Kombe la Cecafa.
Imeelezwa kuwa katika mazungumzo yanayoendelea kati ya Yanga na Maximo suala hilo limeshapitishwa moja kwa moja, na pia kuna ofa nyingine iliyozungumzwa kuwa iwapo ataifikisha Yanga katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho, pia atapewa kitita cha kama hicho cha dola 12,000.
Mmoja wa watu wa karibu na wakala anayeshughulikia suala la Maximo kuja nchini ameliambia Championi Jumamosi kuwa mambo yanakwenda vizuri na Maximo amevutiwa na ofa hizo.
Championi Jumamosi ambalo lilikuwa gazeti la kwanza kuandika ujio wa Maximo, lilipohoji juu ya siku rasmi ya ujio wa kocha huyo, mtoa habari alifunguka:
“Bado hakuna uhakika sana lakini ni kati ya tarehe 14 au 15 ya mwezi huu (Juni), lakini inaonekana kila kitu kinakwenda vizuri sana na mambo yanaenda kwa mpangilio.
“Wakala wake amekuwa akilishughulikia suala hilo kwa ufasaha na utaratibu mkubwa na sasa Maximo anajua anakuja kufanyakazi akianza na makocha wazawa,” kilifafanua chanzo.
Maximo ambaye amewahi kuinoa timu ya taifa, Taifa Stars na kufanikiwa kuivusha hadi michuano ya Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan), ameelezwa kuwa ataanza kazi na usaidizi wa Charles Boniface Mkwasa na Juma Pondamali.
Yanga imeamua kuanza kusaka makocha na katika maombi 44 ya makocha wa ndani na nje ya Tanzania, kamati ya ufundi ya Yanga iliona Maximo ndiye ameonekana kuwa na uzoefu zaidi na rekodi ya juu.
Hivyo, mazungumzo yakaanza kupitia Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji ambaye hivi karibuni wanachama wake waliamua kumuongezea muda wa miezi 12 kuendelea kuwepo madarakani baada ya muda wake wa awali kwa mujibu wa katiba kumalizika.
Katika hatua nyingine wachezaji wakongwe wa timu hiyo wameanza kujawa na hofu ya kupoteza nafasi zao.
Hali hiyo inatokana na nyota hao kukumbuka yaliyopita juu ya Maximo wakati alipokuwa akiifundisha Taifa Stars ambapo alikuwa ni muumini wa wachezaji wenye umri mdogo.
Kutokana na hali hiyo, baadhi ya wachezaji wenye umri mkubwa katika kikosi cha Yanga wameanza kuingiwa na  hofu ya kupoteza nafasi zao pindi Maximo atakapokabidhiwa jukumu hilo la kuifundisha timu hiyo ambayo msimu uliopita ilimaliza ligi kuu ikiwa nafasi ya pili nyuma ya Azam.
Mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu ya Yanga ambaye aliomba kutotajwa jina lake gazetini, alisema baada mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji kutangaza kuwa wapo katika hatua za mwisho za kumalizana na Maximo, baadhi ya wachezaji wenye umri mkubwa walikuwa wakimpigia simu wakitaka kujua ukweli juu ya jambo hilo.
“Mchezaji mmoja kati ya hao alionyesha wasiwasi mkubwa juu ya nafasi yake kutokana na umri wake kuwa mkubwa ambapo alisema: “Ngoja tuone jinsi itakavyokuwa.”
“Nilipomuuliza kwa nini anasema hivyo, aliniambia kuwa Maximo ni muumini wa wachezaji wenye umri mdogo na siyo wakongwe, hivyo atakapoanza kazi inawezekana atatimua wengi, labda awe amebadilika,” alisema kiongozi huyo.
Hata hivyo, wasiwasi huo pia ulionyeshwa na aliyekuwa kocha msaidizi wa timu hiyo ambaye sasa ni kocha mkuu wa JKT Ruvu, Fred Felix Minziro lakini aliuonya  uongozi wa Yanga kutomwingilia Maximo katika maamuzi yake atakayokuwa akiyafanya kwa manufaa ya klabu hiyo.
“Najua Maximo atakapofika klabuni hapo, atafanya mabadiliko makubwa ya kiufundi lakini pia nafikiri wachezaji chipukizi huo ndiyo muda wao wa kuonyesha kuwa wanaweza kwa sababu jamaa ni muumini mzuri wa vijana,” alisema Minziro.
CHANZO CHAMPIONI JUMAMOSI 7/6/2014

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate