EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 24, 2014

Sitta akwaa kisiki...UKAWA wasusia kikao chake, yeye aomba waje wayamalize

Sitta akwaa kisikiKIKAO cha Kamati ya Mashauriano kinachotarajiwa kufanyika leo chini ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, huenda kisifikie lengo lake la kutafuta suluhu ya kunusuru Bunge hilo liweze kuendelea Agosti 5, kutokana na wajumbe wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kushikilia msimamo wao wa kutohudhuria.
UKAWA wasipohudhuria kikao hicho, ni wazi mchakato wa kunusuru Bunge la Katiba utakuwa umegonga mwamba kwa mara nyingine, baada ya juhudi za Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi za kujaribu kuwakutanisha CCM na UKAWA nazo kutozaa matunda.
Sitta kwa kushirikiana na Makamu Mwenyekiti, Samia Hassan Suluhu, wameteua wajumbe 30 wa Bunge hilo kushiriki katika kikao cha Kamati ya Mashauriano kitafachofanyika leo na kesho katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam.

Wajumbe walioteuliwa katika kamati hiyo ni aliyekuwa Mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho, Profesa Costa Ricky Mahalu, James Mbatia, Freeman Mbowe, Ibrahim Lipumba, Peter Kuga Mziray, Vuai Ali Vuai, Askofu Donald Mtetemela, Sheikh Thabit Norman Jongo na Job Ndugai.
Wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, Amon Mpanju, Dk. Francis Michael, Tundu Lissu, Margareth Abdallah, Kidawa Hamid Saleh, Shamsi Vuai Nahodha, Abubakar Khamis Bakari, Dk. Asha Rose Migiro, na Othman Masoud Othman.
Wapo pia Stephen Wasira, Hamad Rashid Mohamed, Askofu Amos Muhagachi, Susan Lyimo, Sheikh Hamid Masoud Jongo, Anne Kilango Malecela, Mary Pius Chatanda, Profesa Mark Mwandosya, Magdalena Sakaya na Khalifa Suleiman Khalifa.

Tangu Sitta alipotangaza kuunda kamati hiyo na kuwaita wajumbe hao kwa ajili ya kujadiliana kutafuta suluhu, wajumbe wa UKAWA wameapa kutoshiriki huku wakimtuhumu kwamba ndiye alishindwa kulimudu Bunge la Katiba na hivyo kuwa sababu ya wao kutoka nje. Msimamo wao ni kukutana na Rais Jakaya Kikwete wakidai kuwa ndiye aliyelikoroga, hivyo lazima alinywe.
Hadi jana jioni, baadhi ya wajumbe wa UKAWA waliozungumza na gazeti hili, walisisitiza kutohudhuria kikao hicho wakidai kuwa msimamo wao unaeleweka tangu awali, kwamba vinginevyo labda wapate maelekezo kutoka kwa viongozi wao.

“Juzi kikao chetu na Jaji Mutungi kilimalizika bila muafaka kutokana na CCM kuleta mapendekezo yasiyotekelezeka na ambayo kimsingi hayawezi kutuondoa katika hoja kuu… sasa tunaenda kufanya nini huko kwa Sitta?
“Isitoshe msimamo wa chama changu kupitia Kamati Kuu iliyokaa mwishoni mwa wiki iliyopita ni kutoudhuria kikao hicho cha Sitta kwa kuwa hakina hoja za msingi zaidi ya kwenda kutuvuruga,” alisema mmoja wa wajumbe kutoka CHADEMA.

Viongozi wakuu wa vyama vinavyounda UKAWA hawakupatikana jana kuthibitisha kama hawatashiriki kikao hicho au la kutokana na kile kilichoelezwa kwamba walikuwa na kikao cha faragha.
Tanzania Daima lilimtafuta Sitta kupata kauli yake kama amepata taarifa rasmi za wajumbe wa UKAWA kutohudhuria kikao chake, ambapo alisema kuwa hawana sababu ya msingi ya kutohudhuria.

“Kikao cha mashaurino kipo kama kilivyopangwa leo na kesho… naamini wajumbe wote wanayo taarifa ya kuhudhuria na sehemu kitapofanyikia, hivyo sidhani kama wajumbe wa UKAWA hawatahudhuria, hawana sababu ya kutohudhuria.
“Nafikiri kikao hicho kitakuwa na ajenda nyingi, waje watuambie yapi yaliyo magumu ama tulipokosea katika vikao vya Bunge vilivyopita ili tujirekebishe na kutovirudia katika vikao vijavyo,” alisema Sitta.
Katibu wa Bunge Maalum la Katiba, Yahya Khamis Hamad aliliambia gazeti hili kuwa maandalizi kwa ajili ya kikao hicho yamekamilika.

Alipoulizwa kama anazo taarifa zozote za kutohudhuria kwa wajumbe wa UKAWA, alisema hana.
“Kama kungekuwa na taarifa zozote za wajumbe wa UKAWA kutohudhuria ningekueleza, kwa maana tangu notisi ya siku 10 na barua itolewe kwa mjumbe mmoja mmoja ya kuhudhuria kikao, hakuna aliyefika kunijulisha kuwa hatahudhuria, hivyo sina taarifa,” alisema Hamad.
Chimbuko
Aprili 16 mwaka huu, wajumbe wa vyama vinavyounda UKAWA, walisusia kikao cha Bunge hilo kwa madai ya upendeleo na ubaguzi uliokuwa unafanywa na CCM dhidi yao, na kwamba wasingeweza kuvumilia matusi yaliyokuwa yakiporomoshwa kwa aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Wajumbe hao kutoka vyama vya CUF, CHADEMA, NCCR-Mageuzi na wa vyama vingine, walichukua hatua hiyo pia wakituhumu kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, waliyodai kuwa ni ya ubaguzi na vitisho akiwa kanisani kwamba Wazanzibari wanaotaka serikali tatu wanataka Zanzibar ijitenge ili iwe nchi ya Kiislamu.
Pia UKAWA wanataka wajumbe wa Bunge hilo wajadili rasimu iliyowasilishwa na Tume ya Warioba badala ya waraka wa maelekezo kutoka CCM, unaoshinikiza muundo wa serikali mbili na kutupilia mbali mapendekezo ya wananchi ya serikali tatu.
CHANZO TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate