EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, November 23, 2014

EXLUSIVE: JAJA ‘OUT’ YANGA, MAXIMO ALETA NYOTA MWINGINE


Mshambuliaji wa Yanga, Genilson Santos ‘Jaja’ ameondolewa katika kikosi cha timu hiyo na nafasi yake itazibwa na kiungo mkabaji pia raia wa Brazil, Emerson Oliveira Neves Roque.
Jaja+Yanga
Jaja, ambaye yuko nchini kwao Brazil kwa mapumziko mafupi ya Ligi Kuu hatarejea nchini na sasa kocha mkuu wa Yanga, Marcio Maximo atarejea Jumanne jijini Dar es Salaam akiwa na Emerson pamoja na kiungo mwingine wa timu hiyo, Andrey Coutinho.

Ingawa inaelezwa kuwa Jaja hatarudi nchini kutokana na matatizo ya kifamilia, lakini presha kubwa aliyokuwa akiipata kwa mashabiki imechangia hilo na hivyo Maximo kuona ni bora ampumzishe kwani akiendelea kumng’ang’ania hata yeye anaweza kutimuliwa.

Mmoja wa wajumbe muhimu kwenye Kamati ya Usajili ya Yanga, Isaack Chanji aliliambia gazeti hili kuwa ni kweli Jaja hatarudi na Yanga, badala yake Maximo atakuja nchini na kiungo Emerson ili kufanyiwa majaribio na kama akifuzu, basi watamsajili.

“Kweli Emerson anakuja badala ya Jaja na atatua nchini Jumanne pamoja na Maximo, ila tutamwangalia kwanza ikiwamo kumfanyia majaribio na baadaye atafanyiwa vipimo vya afya yake na kama akifuzu, basi tutamsajili,” alisema Chanji.

Aliongeza: “Tunataka kuachana na Jaja kwani ni mchezaji ambaye tulitegemea makubwa kutoka kwake, lakini ameshindwa kuonyesha uwezo na hata mashabiki umeona wanalalamikia uwezo wake.



Jaja ambaye alijiunga na Yanga mwanzoni mwa msimu huu hakuonyesha kiwango kilichotarajiwa na wengi na hivyo kila mara kuwakera mashabiki wa klabu hiyo na hata baadhi ya viongozi.

Licha ya Maximo kumtetea mara kwa mara kuwa nimshambuliaji mzuri, hasa kwa kufunga mabao ya vichwa, lakini mashabiki wengi hawakukubaliana na utetezi huo na wengi kuwapa presha viongozi wakishinikiza ‘atoswe’ na wazawa Jerryson Tegete na Hussein Javu wapewe nafasi zaidi uwanjani.

Uzito wake uwanjani, kushindwa kumiliki mpira na pia kushindwa kupachika mabao kama matarajio ya wengi ndizo sababu kubwa zinazomwondoa Jaja Yanga katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.

Mchezaji huyo aliyejiunga na Yanga kwa mbwembwe, aliifungia mabao matano katika mechi 11 alizoichezea, yakiwamo mawili kwenye mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Azam kabla ya kuanza kwa msimu na moja la Ligi Kuu.

Mabao yake Yanga ni katika michezo ya kirafiki dhidi ya Chipukizi ya Pemba na Thika United ya Kenya, kisha akafunga mawili kwenye mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam na kuiongoza timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3- 0 na kuipa ubingwa na akafunga bao moja katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Stand United mjini Shinyanga.Kwa upande wake, kiungo Emerson ana miaka 24 na alizaliwa katika jiji la Rio de Janeiro nchini Brazil na anatua

Yanga akitokea klabu inayocheza ligi ya jimbo la Rio ya Bonsucesso. Klabu hiyo ilianzishwa 1913.


No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate