EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, November 5, 2014

NGWEA FEKI AGOMBEA MAITI YA MAMA’KE

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
Kijana Mohamed Said almaarufu Ngwea feki, anayefananishwa na aliyekuwa staa wa Bongo Fleva, marehemu Alberth Mangweha ‘Ngwea’, ameingia katika mzozo mkali na ndugu zake akidaiwa kugombea maiti ya mama yake mzazi, Mariamu Enock (54).
Kijana Mohamed Said almaarufu Ngwea feki.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, tukio hilo lilijiri kwenye makazi ya familia hiyo, Tandale, Dar hivi karibuni ambapo mama huyo alifariki dunia kwa kuugua kwa muda mrefu.

Ngwea feki akizozana eneo la msiba.
Ilidaiwa kwamba, baada ya kifo hicho, uliibuka mzozo ambapo ndugu wa upande wa mama yake walitaka mwili wakaupumzishe mkoani Iringa huku Ngwea feki akitaka uzikwe Dar. Ilisemekana kwamba jamaa huyo alitaka iwe hivyo kwa sababu alikuwa na mama yake muda wote na alitumia gharama kubwa kumtibu.
Kaka wa Ngwea Feki, Hassan Said.
Akizungumza na mwanahabari wetu kuhusiana na sakata hilo, msemaji wa familia hiyo, Laurence Enock ambaye ni kaka wa marehemu (yaani mjomba wa Ngwea feki), alisema:  “Sisi kama familia tumeamua kumsafirisha ndugu yetu kwenda kumzika Iringa, ndiko kuna mashamba ya familia yetu lakini Mohamed (Ngwea feki) amekataa.”
Baba wa marehemu (babu wa Ngwea Feki), mzee Enock Mayenje.
Alisema kwamba, baada ya vuta nikuvute ndipo Ngwea feki akadai alipwe shilingi laki tatu (300,000/=) alizotumia kumtibu mama yake wakati anaumwa.Kwa upande wake, ndugu wa Ngwea feki aliyefahamika kwa jina la Hassan Said alionekana kutomuunga mkono ndugu yake.
Ndugu wa Ngwea feki, Hassan Said (kushoto) akiwa eneo la msiba.
Hassan alisema: “Mimi siko tayari kugawana vitu vya mama yangu kwa kuwa ndugu yangu amekataa mwili wa mama usisafirishwe hadi alipwe fidia yake hivyo imebidi tuuze vitu vya mama ili alipwe hiyo laki tatu.
Wa pili kushoto ni msemaji wa familia hiyo, Laurence Enock ambaye ni kaka wa marehemu (yaani mjomba wa Ngwea feki)
Alipofuatwa Ngwea feki ili kusikia upande wake aligoma kutoa ushirikiano: “Siko vizuri kwa sasa nicheki baadaye.”
Kwa mujibu wa baba wa marehemu, Enock Mayenje, mjukuu wake huyo amekuwa akijitenga na familia hivyo hawezi kumlazimisha ila amesikitika kwa kitendo chake cha ‘kuwauzia’ maiti ya mama yake mzazi.
Marehemu Mariamu Enock enzi za uhai wake.
Kamanda wa Ulinzi Mtaa wa Mkunduge, Tandale jijini Dar, Yusuph Banda, amekiri kutokea kwa tukio hilo na wamekubaliana kuuzwa kwa vitu vya marehemu ili gharama hizo zilipwe kwa Ngwea feki ili mwili huo usafirishwe kwenda Iringa kwa mazishi.Kujua mengi zaidi kuhusu tukio hilo, tembelea www.globaltv.tz

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate