EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, December 3, 2014

VIROBA SI CHAI!

NI AIBU! Ndivyo unavyoweza kushangaa baada ya mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kunywa pombe kiasi cha kupoteza fahamu akiwa na sare za taasisi hiyo inayoheshimika nchini na kujikuta akilala karibu na mtaro, katika stendi kuu ya mabasi mjini Iringa.
Anayedhaniwa kuwa mwananjeshi akiwa amelala kwenye mtaro.
Habari kutoka eneo la tukio zinasema mtu huyo alipanda basi liitwalo Mgumba huko Mafinga, ambako ipo kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambalo lilikuwa likielekea mjini Iringa. Abiria waliokuwa pamoja naye garini, wanaripoti kuwa akiwa humo, tayari akionekana amelewa, aliendelea kunywa pombe kali inayokaa kwenye pakiti, maarufu kama viroba.

Akisimulia zaidi, mmoja wa abiria wa basi hilo alisema akiwa bado anaendelea kunywa, ghafla alianza kutapika na kujisaidia haja ndogo kiasi cha kuwachefua watu wengine.“Tulipofika stendi, tukalazimika kumsaidia kumshusha huku akiwa hajitambui kabisa. Akalala mtaroni, ikabidi tummwagie maji, ndipo alipozinduka na kupata fahamu kidogo.
Baadhi ya watu wakimshangaa mwanajeshi huyo.
Alikuwa anaona aibu sana, akajikakamua na kutoa namba ya simu ya rafiki yake, ambaye ni askari wa FFU mjini Iringa, ambaye alipigiwa na kuja kumnusuru,” alisema abiria huyo aliyekataa kutaja jina lake.
Gazeti hili liliwasiliana na kiongozi mmoja wa kambi ya Jeshi Mafinga, ambaye baada ya kuelezwa kuhusu askari huyo, alikiri kuwa ni mwenzao, lakini siyo wa kambi hiyo.
“Ni kweli nimeziona hizo picha, huyo jamaa kweli ni askari mwenzetu lakini siyo wa kambi hii, huyo anatoka Itende, Mbeya. Jaribu kuwasiliana nao kule wanaweza kukupatia taarifa maana sisi tulishawataarifu,” alisema kiongozi huyo, aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa vile siyo msemaji wa Jeshi.
Juhudi za kumpata Mkuu wa Kikosi cha Itende hazikuweza kufanikiwa, lakini Kaimu Msemaji wa Jeshi la Wananchi, Makao Makuu Dar es Salaam, Meja Joseph Masanja, alipatikana na yeye kukiri kuziona picha hizo mitandaoni.
“Ni kweli nimeziona picha hizo na ninazo hapa, lakini kama unavyoziona, kuna gizagiza kiasi kwamba huwezi kumtambua. Ni vigumu kusema huyo ni askari wetu kwa sababu picha haionekani, huenda ni mtu tu kalewa akiwa na nguo za jeshi.
Mkuu wa majeshi Davis Mwamunyange.
Alipoulizwa kuhusu adhabu anayoweza kupata endapo atafahamika kuwa ni mwanajeshi, Masanja alisema hayo ni masuala ya utawala yanayotofautisha makosa ya kijinai na nidhamu.
“Vilevile inakuwa vigumu kidogo kujua kwa nini mtu aliyepiga picha aliamua kuposti kwenye mitandao,” alisema Meja Masanja akisisitiza Jeshi bado linaendelea kutafuta ukweli wa picha hizo.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate