EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, April 9, 2015

VIGOGO 3 WASITISHWA KAZI RUBADA


Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA), Aloyce Masanja (kushoto).
KAIMU Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA), Aloyce Masanja na wenzake wawili wamesimamishwa kazi kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha na kujilimbikizia madaraka.
Viongozi wengine waliosimamishwa kuanzia jana ni Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji, Tatu Ndatulu na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Filozi Mayayi.
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira alisema baada ya kuwepo kwa malalamiko yaliyokuwa yanatolewa na wawekezaji kwa muda mrefu, serikali iliamua kuunda Tume Novemba mwaka jana.
Tume hiyo ilikuwa chini ya Semroki Mwanyika, ambaye sasa ni Mkurugenzi Msaidizi wa Ukaguzi wa Ndani wa Serikali katika Wizara ya Fedha (Hazina).
Wassira alifafanua kuwa viongozi hao wanasimamisha kazi kwa tuhuma za kuiibia Serikali kwa miaka miwili, utovu wa nidhamu na kushindwa kutimiza majukumu yao kikamilifu kama watumishi wa umma.
Pia alisema licha ya kuwasimamisha kazi viongozi hao, ripoti iliyoibua ubadhirifu huo, itapelekwa katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na Polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi ili hatua za kisheria zichukuliwe.

“Mimi kama Waziri nimeamua kuwasimamisha kazi watu hao kutokana na kutowajibika ipasavyo katika nyadhifa zao, pia wamekuwa watovu wa nidhamu. Suala la makosa ya jinai nitawaachia Polisi na Takukuru ambao watajua ni lini watawafikisha katika vyombo vya sheria,’’ alisema Wassira.
Waziri huyo alieleza katika miaka hiyo miwili, Rubada walikusanya zaidi ya Sh bilioni 2.7 kutoka kwa wawekezaji. Aidha, alisema kati ya hizo, Sh milioni 740 tu ndizo zilizotumika kihalali, huku kiasi kingine kikiwa hakijulikani kilipo.
Alifafanua kuwa, kati ya zilizotumika, Sh milioni 13.9 imeelezwa zimetumika kwa matumizi yao binafsi huku Sh milioni 13 zimetumika kwa ajili ya masurufu ambayo hayajarudishwa.
‘’Pamoja na hayo, Sh milioni 326 zilitengwa kwa ajili ya kujenga Kambi ya Kilimo maeneo ya Mkongo na hazikufanya kazi iliyotakiwa. Pia walichukua Sh milioni 58 ambazo zilitakiwa zipelekwe Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), lakini hazikupelekwa,’’ alidai.
Aliongeza; ‘’Kwa maana hiyo wafanyakazi walioko kazini kwa sasa wakistaafu, hawataweza kulipwa mafao yao kutokana na pesa zilizotakiwa kupelekwa hazijafikishwa sehemu husika’’.
Hii ina maana kwamba, mbali ya Sh bilioni 2 ambazo hazijulikani zilipo, kiasi kingine cha Sh milioni 384 kutoka mradi wa kambi ya Kilimo Mkongo na zile za NSSF, jumla ya fedha ambazo hazijulikani zilipo ni Sh bilioni 2.3.
Wassira, mmoja wa wanasiasa na viongozi wakongwe walioshika nyadhifa za uwaziri tangu enzi za utawala wa
Awamu ya Kwanza chini ya Rais Julius Nyerere, alidai watumishi hao walikuwa wanatembea na fedha mifukoni, wakijifanya wao ni wahasibu, ambapo fedha nyingine walikuwa wanaweka kwenye akaunti ya serikali huku nyingine wakiweka katika akaunti zao binafsi.
Aidha, alisema Rubada kulikuwa na uongozi mbaya kwa kuwa na ubinafsi, rushwa na kwamba mfumo wa ndani ulikuwa na ubadhirifu.
Akizungumzia suala la uteuzi wa viongozi wapya, Wassira alisema ameiagiza Bodi ya mamlaka hiyo kutafuta watu weledi na waaminifu, watakaokaimu nafasi hizo.
Akijibu swali kuhusu ubadhirifu unaofanywa na viongozi wanaokaimu nafasi mbalimbali, alisema; ‘’Suala la kukaimu sio sababu ya kuwa fisadi na kuwa mbadhilifu wa fedha za serikali, kwani wapo wengine wanakaimu na wanafanya vizuri hata kuthibitishwa na kuwa wakurugenzi.’’
(CHANZO: HABARI LEO)

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate