EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, May 30, 2015

WAUMINI: MAPADRI WARUHUSIWE KUOA

Mwandishi wetu
Mpasuko! Kufuatia kuibuka wimbi la kashfa za ngono zinazowagusa waseja wa daraja la upadri duniani, baadhi ya waumini wa madhehebu mbalimbali yakiwemo Katoliki na Anglikana, wameibuka na kudai kuwepo kwa marekebisho ya sheria ya makanisa hayo yanayoruhusu watumishi hao kuoa kwani kwa sasa wanayaaibisha, jambo ambalo linaharibu imani juu ya Ukristo.
Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo.
NINI KIMETOKEA?
Hayo yanakuja kufuatia tukio la hivi karibuni la kunaswa kwa Padri Anatoly Salawa ambaye ana cheo cha Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference, Tec) aliyekutwa na mrembo vichakani.
Father Salawa alinaswa na mrembo huyo vichakani ndani ya gari maeneo ya Kurasini jijini Dar.
Mbali na tukio hilo, pia yapo matukio mengine ya mafumanizi likiwemo lile la Father Urbanus Ngowi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi aliyefumaniwa ‘laivu’ na mke wa mtu aliyetajwa kwa jina la mama P.

Katika tukio hilo la mwaka 2013 lililoripotiwa na gazeti ndugu la hili, Ijumaa Wikienda, Father Ngowi alikutwa na mwanamke huyo ambaye alikuwa muumini wake, chumbani kwake maeneo ya Marangu Wilaya ya Moshi Vijijini.
Padri Anatoly Salawa aliyenaswa na binti kichakani.
WAUMINI WAFUNGUKA
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, mwanzoni mwa wiki hii, waumini hao walitolea mifano ya baadhi ya viongozi wa madhehebu hayo kunaswa katika skendo za uhusiano wa kimapenziu hivyo kuona ni bora wakaruhusiwa kuoa ili kuliondolea aibu kanisa.
“Ni bora kama ni sheria irekebishwe ili hawa mapadri waruhusiwe kuoa kwani sasa hii ni aibu kwa kanisa, kuliko kuendelea kuchafua taswira ya misingi ya dini ambayo imekuwepo tangu enzi na enzi.
“Mbona mapadri wengine wa Ulaya Mashariki wa madhehebu ya Katoliki (Ukranian Greek Catholic Church na Coptic Catholic Church) wanaoa? Kwa nini na wa kwetu wasioe?” alihoji mmoja wa waumini hao katika mahojiano na mwandishi wetu ndani ya ofisi za gazeti hili, Bamaga-Mwenge jijini Dar.
BARUA YA WAZI KWA PAPA
Mbali na waumini wa hapa nchini, mapema mwaka jana, wanawake wapatao 26 waishio nchini Italia, walimwandikia barua ya wazi Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Katoliki Duniani, Papa Francis wakimueleza mateso wanayopata kwa kuwa na uhusiano wa siri wa kimapenzi na baadhi ya mapadri wa kanisa hilo.
Mkuu wa Kanisa la Katoliki Duniani, Papa Francis.
PAPA ANENA
Akifafanua sakata hilo katika mahojiano maalum na Jarida la Republica la jijini Vatikani, Papa Francis alikiri kuwepo kwa taarifa za mapadri kuwa na uhusiano wa kimapenzi, kauli ambayo ilipingwa vikali na msemaji wa kanisa hilo, Federico Lombardi kwa madai kuwa mwandishi wa jarida hilo alimnukuu papa vibaya.
Mbali na hayo, padri mmoja aishiye Italia kutoka Kanisa la Kigiriki la Byzantine lililo chini ya Mamlaka ya Vatican, Jani Pecoraro alisema ifike wakati sasa nyakati zitambuliwe kwani kuoa kwa mapadri hakuondoi weledi wa huduma zao.
“Tunapaswa kusoma nyakati na hakuna shaka kwamba jamii ya sasa imekuwa ikiibua hoja kuwa mapadri waliooa wanaweza kuwa na kiwango sawa cha utumishi na wengine,” alikaririwa padri huyo.
PAPA AWA MAKINI
Hata hivyo, Papa Francis amekuwa makini na jambo hilo huku akieleza kuwa zuio la mapadri kuoa liliasisiwa karne 10, ikiwa ni karne tisa nyuma kabla ya kifo cha Yesu Kristo huku kukiibuka sintofahamu juu ya uamuzi wa papa juu ya mapadri wanaokiuka misingi hiyo.
PIGO KWA KANISA
Mbali na waamini wanaotaka mapadri kuruhusiwa kuoa, wapo wanaoliona jambo hilo kuwa ni pigo jipya kwa kanisa kwani wanatamani mapadri kuendelea kuwa waseja.
Father Urbanus Ngowi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi.
Kuhusiana na sakata hilo, gazeti hili lilikwenda Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam na kukutana na Katibu wa Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, Denis Aminias na kuzungumza naye ambapo alisema:
“Sisi kama kanisa tutaendelea kusimamia katika misingi ileile ya mapadri kutooa.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate