EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 28, 2015

BVR Dar, sasa ni mateso

AWananchi wakiwa katika foleni ya kujiandikisha kupiga kura. 
Na Shani Ramadhani
WAKATI zoezi la uandikishaji kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa kutumia mfumo wa kielekrtioniki uitwao Biometric Voters Registration (BVR), jijini Dar es Salaam ukiendelea, mengi yameibuka kwenye baadhi ya vituo vya uandikishaji na kuwafanya wananchi wengi kukata tamaa wakidai kuwa zoezi hilo kwao sasa ni mateso.
IMG_1067Wananchi kadhaa waliohojiwa na gazeti hili walisema zoezi hilo la uandikishaji ni gumu kwa sababu baadhi yao huamka saa sita usiku kuwahi vituoni lakini baadaye wanajikuta wakiandikishwa siku ya pili.
Mama mmoja aliyekutwa Kituo cha Shule ya Msingi Kisiwani, Ubungo Dar, Mariam Ally alisema katika kituo hicho Jumamosi iliyopita wananchi walipigana kutokana na mwingiliano wa namba zinazotolewa kwa kila anayefika kujiandikisha.
2 (4)Mwandikishaji akiandikisha wapiga kura kwenye mfumo wa BVR.
“Kuna watu walifika saa sita usiku, lakini asubuhi walipofika wakakuta waliochelewa wanaandikishwa, fujo ilitokea ikabidi polisi kuitwa wakaweka mambo sawa, kifupi ni kwamba haya ni mateso,” alisema Mariam.
Nao wananchi waliokutwa katika Kituo cha Kimara walisema kuwa katika kituo hicho watu hukesha.
2 (5)…Akichukuliwa alama za vidole.
Mkazi wa eneo hilo, Massawe J. Massawe alisema japokuwa amepata kitambulisho cha kupigia kura lakini alifika kituoni hapo saa tisa usiku.
 “Ilinibidi niamke mapema ili niwahi kupata kitambulisho lakini tangu saa 9 usiku nilivyoamka nimekuja kupata kitambulisho saa 6 mchana, kiukweli watu wanateseka sana hasa wale wenye watoto wadogo na wazee, hawapewi kipaumbele na wananchi.

IMG_0005Mmoja wa waandikishwaji akikabidhiwa kadi yake ya mpiga kura mara baada ya kukamilisha taratibu za kujiandisha.
Naye Frida George mkazi wa Mbagala Rangi Tatu alipokutwa akitoka katika kituo cha kujiandikisha alisema: “Nimewahi tangu saa kumi usiku na sasa hivi ni saa kumi na nusu jioni, pima mateso niliyoyapata, ilikuwa nimlete mama yangu mzazi kuandikisha, sitafanya hivyo kwa sababu ni mtu mzima ana zaidi ya miaka themanini.”
Naye mkazi wa Sinza aliyejitambulisha kwa jina moja la Pius aliliambia gazeti hili kuwa wananchi wengi wamekuwa wakilalamikia uongozi kwa kutofuata mfumo unaotakiwa na kusababisha watu wengi kuishia kuchukua namba na kutorudi tena baada ya kuona usumbufu.
IMG_1069“Mimi nilikwenda pale saa moja asubuhi, nilipofika nikakuta foleni ya namba nikachukua namba tisini nikaamua kuchana namba na kwenda kuendelea na shughuli zangu kwa maana nahisi muda unakwenda bure labda nijipange tena kwa mara nyingine niamke mapema zaidi.”
Wakazi wa Kinondoni jijini Dar waliliambia gazeti hili kuwa, uandikishaji unakwenda taratibu hali inayofanya mtu mmoja kuchukua dakika 30 au zaidi kupata kitambulisho cha mpiga kura akiingia ndani.
“Hapa tulipo huwezi kuamini kama wengine tumekuja saa nane usiku lakini mpaka muda huu (saa sita mchana) tupo tu kwenye foleni ambayo haitembei, yaani ni mateso, tunapata shida sana serikali itambue hili, ikibidi iongeze siku,” alisema Fatuma Abdallah.
Festus Yohana aliyekuwa kwenye kituo cha kujiandikishia wapiga kura cha Shule ya Msingi Mwenge alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) ilipaswa kujua kuwa Dar ina watu wengi, hivyo mashine zingeletwa nyingi ili kuondoa mateso hayo wanayopata wananchi.
Uchunguzi wa gazeti hili umegundua kuwa licha ya zoezi hilo kuwa na changamoto nyingi lakini katika vituo vingi ambavyo waandishi wetu walitembelea kwa siku tatu walikuta zoezi likiendelea kwa hali ya utulivu huku akina mama wenye watoto wadogo na wazee wakilalamikia utaratibu wa kutowapa kipaumbele kuandikisha, wengine wakidai kuandikisha kwa rushwa katika baadhi ya vituo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki alisema kwa njia ya simu juzi kuwa wanaendelea kufuatilia mchakato huo ili kubaini dosari zilizopo na kuzitafutia ufumbuzi wake huku akiweka wazi wanafuatilia taarifa za kuwapo baadhi ya wanaoendekeza vitendo vya rushwa katika zoezi hilo.Pia, alisema wanaendelea na mikakati ya kuhakikisha wataalamu wa mashine hizo za BVR wanapelekwa vituoni ili kufanya matengenezo iwapo kutatokea mashine kuwa na tatizo linalokwamisha uandikishaji.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate