EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 28, 2012

Yaliyojiri katika muziki, burudani 2012.

MWAKA 2012 ndio uko ukingoni, ambapo Jumanne ijayo panapo majaliwa yake Mungu tutaingia katika mwaka mwingine, yaani 2013.

Leo kwa vyanzo na kumbukumbu nyingi za habari za kisanii tutakuletea baadhi ya matukio yaliyotikisa katika mwaka huu.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlUJOLATpwxAiBOS2vl-D51vjuSohYxKtCD29n8pvKcrofzMOWXUiTKL5pUHRpeRsWGBGpd62Hygwtm5jqQOcQf1L3JDrGW9F12JWvCqWV8j-omrBeSmW6K4jPDSgpLEw9m_LdfV2aCojv/s1600/wema-vs-diamond.jpg
Katika mwaka wa 2012 wamiliki wengi wa bendi walionekana na kutawaliwa na mzimu wa kunyakuliana wanamuziki huku kila mmoja akiamini kwamba hiyo ndiyo ilikuwa njia ya kujipatia jina na kuzoa mashabiki.
Mwanzoni mwa kwaka huu bendi ya muziki wa dansi ya Twanga Pepeta ilipata mtikisiko mkubwa kwa kunyakuliwa aliyekuwa muimbaji kiraka wa bendi yake, Charles Gabriel ‘Chalz Baba’ aliyenyakuliwa na bendi ya Mashujaa.

Kama hiyo haitoshi, pia msanii huyo akiwa na rapa wa bendi ya FM Academia 33 waliandaliwa usiku maalumu wa utambulisho uliofanyika kwenye ukumbi wa Business Park, Dar es Salaam.
Charlz Baba alinyakuliwa mara tu baada ya bendi hiyo kutoka katika ziara yake nchini Uingereza ilikokwenda kwa mwaliko maalumu.


Aliyekuwa mnenguaji tishio na mwenye mvuto katiba bendi ya Twanga Pepeta, Aisha Mbegu ‘Queen Aisha’, maarufu kama Aisha Madinda alijikuta akishuka kiwango chake cha uchezaji pindi awapo jukwaani na wakati akiwa katika matibabu na mipango ya kujiweka sawa ili aweze kurudi tena jukwaani, akachukuliwa na bendi ya Extra Bongo na baadaye akashindwa kuendelea na kazi hiyo na sasa inasemekana ameachana na muziki wa dunia na kuamua kuokoka na kuwa kati ya waumini wa kanisa moja.
Msanii Kalala Hamza Kalala ‘Kalala Junior’ alitangaza kuachana na muziki na bendi aliyoiasisi ya Mapacha Watatu na kurudi katika bendi ya Twanga Pepeta na kwa mara ya kwanza akatunga kibao kinachovutia wengi sasa.

Mashujaa walizidi kuchukua wasanii Twanga Pepeta kwa kumchukua mnenguaji wake, Lilian Internet na Meneja Martin Sospeter.
Extra Bongo nayo haikubaki nyuma wakachukua wanenguaji wawili Maria Soloma, Sabrina Mayonise na muimbaji Khadija Kimobitel.
Mwinjuma Muumini alitimkia bendi ya Victoria akapiga kambi Mtwara na yeye anadaiwa kunyemelea wasanii katika bendi ya Twanga..
Bendi ya Skylight ilizinduliwa kwa makekeke huku katika bendi hii kukiwa na sura ya baadhi ya wanamuziki walioing’arisha bendi ya Machozi inayomilikiwa na Judith Wambura ‘Lady Jaydee’.

HABARI ZA UGONJWA
Kwa upande wasanaa ya filamu, ugonjwa wa Juma Kilowoko ‘Sajuki’, wazua jambo, kila kona ni michango.
Wasanii mbalimbali pamoja na viongozi wa kisiasa walijitokeza kumchangia na kupata fedha za kumpeleka nchini India kwa matibabu, akatibiwa na kurudi nchini, lakini hivi karibuni alianguka jukwaani akiwa katika onesho la kuchanga fedha za kumrejesha kwenye matibabu nchini India.
Jack Wolper alipata mchumba Dallas na kubadilisha dini sasa ni Ilham ila uchumba huo ulivunjika huku yeye akiahidi kubaki katika imani ya dini ya Kiislamu kwa kuwwa anaipenda na mama yake ana asili hiyo.
Mchekeshaji wa siku nyingi, Said Ngamba ‘Mzee Small’, alishikwa na ugonjwa wa kiharusi ghafla akitokea katika kazi jijini Mwanza, hadi sasa hali yake bado ni mbaya.
Mwanamuziki aliyetikisa kwa miondoko ya kutikisa kiuno na sauti nzuri na mwenye haiba awapo jukwaani, Rehema Chalamila ‘Ray C’, alijikuta akipoteza mvuto na mashabiki wake kutokana na ugonjwa ambao haukuwekwa wazi, hali iliyosababisha kusaidiwa na Rais Jakaya Kikwete hadi afya yake ilipotengemaa.

Akizungumza katika viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam, Ray C anasema anamshukuru Rais Jakaya Kikwete kwa kumsaidia gharama za kutibiwa ugonjwa wake ambao ulibaki kuwa siri.
Tamasha la Fiesta larindima huku likizinduliwa na msanii mahiri wa Hip Hop kutoka nchini Kenya.
Kwa mara ya kwanza katika tamasha hilo wasanii wa filamu wahusishwa akiwamo Jacob Steven ‘JB’, Vincent Kigosi ‘Ray’, Wema Sepetu, Aunt Gwantwa na Steve Nyerere.

Lakini wakiwa katika matamasha kadhaa na kwenye mikoa mbalimbali wasanii Wema na Aunt walijikuta wakiingia katika kashfa ya kuonesha sehemu zao nyeti walipokuwa jukwaani.
Kufuatia kadhia hiyo, Shirikisho la Filamu nchini liliwataka waiombe radhi jamii kwa kuikosea nao wakafanya hivyo katika mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dar es Salaam.
Msanii nyota katika filamu nchini Aunt Ezekiel alichumbiwa na kufunga ndoa na Sunday ‘Mzee wa Dubai.’

MAADHIMISHO
Klabu yenye hadhi ya kimataifa nchini, Club Bilicanas ilisherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa kwake.
Kampuni kubwa ya burudani nchini ya Clouds FM nayo ilisherehekea miaka 13 tangu kuanzishwa na kumleta msanii galacha kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Antoine Koffi Olomide na tamasha kubwa kufanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Kinondoni Dar es Salaam.

MAMA SAKINA APIGWA MWELEKA
Wakiwa katika uzinduzi wa albamu ya pili ya bendi hiyo mmiliki wa bendi ya Mashujaa, Mamaa Sakina, alianguka na kuzirai baada ya kuingia uwanjani Leaders Club na kukuta uwanja mtupu tofauti na alivyotarajia .
Uzinduzi wa bendi ya Mashujaa wakwama kuzinduliwa kama ilivyopangwa, huku onesho la mwanamuziki JB Mpiana likidorora na uzinduzi wa albamu ya bendi yake kushindikana kuzinduliwa kama ilivyopangwa.

MUZIKI WA KIZAZI KIPYA
Shindano la Bongo Star Search lafanyika na kuwaacha wenye vipaji nje ya wigo. Wadogo wa aliyekuwa mshindi wa 2009, Misoji Nkwabi, watupwa nje katika dakika za mwisho za shindano.

UDAKU KIDOGO
Uhusiano wa kimapenzi kati ya wasanii nyota Wema na Diamond waota mbawa, vyombo vya habari vikaripoti Diamond anatoka na aliyekuwa Miss Tanzania namba 2 Jokate Mwegelo. Lakini hawakudumu katika uhusiano wao.
Uvumi wa kuvunjika kwa ndoa ya msanii Irene Uwoya na mumewe Kataut Ndikumana, wazinguana na baadaye mambo yakawa sawa.
Wasanii wa kike wakanyambuana katika kipindi cha Take One kinachorusha na Zamaradi Mketema.
Irene Uwoya na Wema Sepetu wakamkashifu sana Jacqueline Wolper pamoja na Mama Wema kuingilia kati ugomvi wa mwanaye.
Wema ajitangaza na kujionesha jinsi nyumba yake ilivyo, mwenye nyumba amjia juu kwa kuinadi nyumba yake.
Msanii huyo alilazimika kufanya hivyo kufuatia kukashifiwa na Wolper kwamba hana pa kulala ndiyo maana ana tabia ya kuhamia kwa mwanaume, naye si mwingine bali ni Naseeb Abdul Diamond.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEix8nYvsO8cx_MsqQoD6AyRbohn9cnUbHBKkXrYm7OYMuuf8IWfdbZyX0lZ3XNP00o7EV12Ggj-UBl5oCTjKr67zr-3-SyWyl9F5XvfK38EhbeIueaCRApg96TnSdh2X53zseQBSy-F9hF3/s1600/BELLA.jpg
WASANII WA KIMATAIFA WALIOTUA BONGO
Msanii Rick Ross alitua nchini kwa ajili ya kunogesha tamasha la Fiesta 2012.
Msanii JB Mpiana alitua nchini akafuatiwa na Koffi Olomide.
Azonto akatua katika Sikukuu ya Krisimasi.

HABARI ZA SIMANZI NA VIFO
Kifo ya Steven Kanumba ‘The Great’ aliyefariki dunia ghafla nyumbani kwake maeneo ya Vatican Sinza, jijini Dar es Salaam, msiba wake utabaki kuwa na historia ya kuhudhuriwa na watu wengi waombolezaji waliotoka mikoani na hata nje ya nchi.
Hadi sasa msanii mwenzake, Elizabeth Michael ‘Lulu’, anashikiliwa kwa kusababisha kifo hicho.
Msanii John Stephano aliyefariki dunia kwa kutokuwa na umakini wa ugonjwa wake, alisumbuliwa na kongosho lakini madaktari wa Hospitali ya Mwananyamala wakampiga picha na kuona kwamba utumbo wake umetoboka, hivyo wakamfanyia upasuaji uliosababisha mauti yake.
Msanii wa filamu na mchekeshaji, Salum Mkieti ‘Sharo Milionea’ alifariki dunia kwa ajali ya gari alipokuwa akienda nyumbani kwao Tanga.
Aliyekuwa msanii wa kundi la Kaole Mohamed Khalid ‘Mlopelo’ afariki dunia.
Kwa upande wa muziki wa taarabu wapata pigo kwa kuondokewa na aliyekuwa msanii mwenye mvuto na mashabiki wengi, Mariam Khamis ‘Paka Mapepe’. Mungu azipumzishe roho za marehemu wote mahali pema peponi. Amina.Habari hii na Khadija Kalil.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate