EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 25, 2013

Maskini Simba...Yalala kwa Mtibwa, vurugu kubwa zaibuka Taifa

KAMA ni mtoto, unaweza kusema si riziki. Hivi ndivyo hali ilivyo ndani ya klabu ya Simba, ambako imeendelea na mwenendo wa shaka katika Ligi Kuu Tanzania bara, baada ya jana kukubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa wakata miwa wa Mtibwa Sugar kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaam.

Simba ambao ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo, msimu huu imekuwa na mwenendo mbovu na hata kufuta mawazo ya kutetea taji hilo miongoni mwa mashabiki wake, ambao hivi sasa wako katika hali mbaya kutokana na kufanya vibaya.
Hadi sasa, Simba imepoteza mechi tatu huku ikijikongoja katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 31 baada ya kushuka dimbani mara 18. Yanga wako kileleni kwa pointi 39 huku Azam ikifuatia kwa pointi 36.

Katika mechi ya jana, Simba ilianza kwa kasi na dakika ya tatu tu, Shomari Kapombe alipokea pande la Amir Maftah, lakini shuti lake likaokolewa na kipa Hussein Sharrif, kabla ya Mtibwa kujibu mashambulizi na kupata kona ambayo haikuzaa matunda.
Alikuwa ni Salvatory Ntebe dakika ya 16, aliyeiandikia Mtibwa bao hilo la pekee, baada ya kuunganisha mpira uliotokana na kona.

Dakika ya 41, Simba walifanya mabadiliko kwa kumtoa Ramadhani Chombo ‘Redondo’ na nafasi yake kuchukuliwa na Kigi Makasi.

Redondo baada ya kutoka alikwenda moja kwa moja kwenye vyumba vya kuvalia badala ya benchi la wachezaji wa akiba. Kitendo kama hicho kilifanywa na Haruna Moshi ‘Boban’ siku walipocheza na Libolo kwenye uwanja huo.
Hadi mwamuzi Ibrahim Kidiwa kutoka Tanga akiashiria mapumziko, Mtibwa walikuwa mbele kwa bao hilo.

Kipindi cha pili, Simba walirejea kwa nguvu na dakika ya 49, shuti la Haruna Chanongo lilipaa langoni mwa Mtibwa sentimita chache.
Simba walifanya mabadiliko tena dakika ya 51, kwa kumtoa Boban na nafasi yake kuchukuliwa na Amri Kiemba, ambako kabla ya kutoka, alimkumbatia Kigi Makasi na kama mazoea yake, alikwenda moja kwa moja vyumbani.

Dakika ya 86, Simba ilipata pigo, baada ya Juma Nyoso kulimwa kadi nyekundu kutokana na kumkwatua Vicent Barnabas wakati mpira ukiwa umetoka nje. Hadi Mwamuzi Kidiwa akimaliza mpira, Mtibwa iliibuka kidedea kwa bao 1-0.

Matokeo hayo yaliibua vurugu miongoni mwa mashabiki wa Simba, ambao walitaka kuvamia jukwaa kuu kuwashughulikia baadhi ya viongozi waliokuwepo.
Kutokana na hali hiyo, polisi iliwalazimu kufunga baadhi ya njia za kuingilia maeneo ya jukwaa kuu ili kuwanusuru viongozi hao, hali ambayo ilisababisha adha kubwa kwa mashabiki wakati wa kutoka.

Lakini mashabiki hao wa Simba, walibaki nje ya uwanja wakiwa katika vikundi vikundi, hali iliyosababisha wachezaji kufungiwa vyumbani. Mashabiki hao walisikika wakiutupia lawama uongozi huku wakidai hawamtaki kocha, Mfaransa Patric Liewig.
Hali ilizidi kuwa mbaya, ambako Uwanja wa Taifa uligeuka uwanja wa vita, baada ya polisi kulazimika kutumia maji ya kuwasha kuwatawanya mashabiki hao, huku basi la Simba likiondoka likisindikizwa kwa ulinzi wa hali ya juu.
Simba: Juma Kaseja, Nassoro Masoud ‘Cholo’, Amir Maftah, Juma Nyoso, Komanbil Keita, Shomari Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Haruna Moshi ‘Boban’/Amri Kiemba, Haruna Chanongo/Mrisho Ngasa, Ramadhani Chombo ‘Redondo’/Kigi Makasi.
Mtibwa: Hussein Sharrif, Said Mkopi, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Salvatory Ntebe, Salum Swedi, Shabani Nditi, Jamal Mnyate,  Hussein Javu/Juma Liuzio, Shabani Kisiga ‘Malone’, Rashid Gumbo, Vicent Barnabas.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate