EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 30, 2013

Wanaokwamisha ujenzi wa barabara kukiona.

SERIKALI imeonya kuwa haitaruhusu watu wachache wakwamishe juhudi za Serikali za kuunganisha nchi na mtandao wa barabara za lami.
Rais Jakaya Kikwete, alisema hayo jana katika eneo la Omugakorongo Kata ya Ndama, wilayani Karagwe, wakati akiweka jiwe la msingi katika barabara ya Kyaka –Bugene yenye urefu wa kilometa 59.1, inayojengwa kwa kiwango cha lami.
Rais Jakaya Kikwete akisimikwa kuwa Chifu wa Wahaya na kukabidhiwa mgolole na silaha za jadi za Wahaya katika sherehe ya kuzindua Wilaya mpya ya Kyerwa mkoani Kagera mwishoni mwa wiki. (Picha na Ikulu).
Alitoa kauli hiyo baada ya Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, kumuomba amuunge mkono wakati wa kupambana na wananchi wanne, waliokataa kupokea fidia na kubomoa nyumba zao, ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo.
Dk Magufuli alisema watu hao, akiwemo mzee marufu wa Wilaya ya Karagwe, Nehemia Kazimoto, wanataka fidia zaidi, la sivyo nyumba zao hazibomolewi au watakwenda mahakamani.
Alisema wananchi 400 waliokumbwa na athari za kubomolewa nyumba kupisha ujenzi wa barabra hiyo, wamelipwa fidia Sh bilioni 2.8 kwa mujibu wa sheria, isipokuwa wananchi wanne tu akiwemo Kazimoto, ambao wamegoma kupokea fidia.

“Hata wakienda mahakamani, sisi hatutaingilia Mahakama, bali barabara itaendelea kujengwa ikipitia katika maeneo yaliyoainishwa,” alisema Dk Magufuli.
Akitoa mfano wa mzee huyo aliyewahi kuwa kiongozi katika vyama vya wafanyakazi nchini, Dk Magufuli alisema amegoma kupokea fidia yake ya Sh milioni 101, ambazo zilitolewa na Serikali huku akidai kuwa hazitoshi na wala hatokubali nyumba yake ibomolewe kupisha barabara.
Kauli ya Rais
Akijibu maombi hayo, Rais Kikwete alimtaka Waziri Magufuli aendelee na kasi ya kutekeleza mipango yake ya ujenzi wa barabara ya Kyaka Bugene, ili ikamilike kwa wakati, ingawa kuna changamoto zinazokabili mradi huo kutoka kwa baadhi ya wananchi ambao si wapenda maendeleo.
“Hatutaruhusu watu wachache wazime na kukwamisha maendeleo ya Watanzania walio wengi, Waziri nimekusikia, endelea na mipango na kazi yako ya kujenga barabara hii, ili Wanakagera na Watanzania, waendelee kunufaika na matunda ya Serikali…tena hii ni ahadi yangu niliyoitoa wakati naomba kura mwaka 2005, pia ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2010,”alisema Rais Kikwete.
Alisema lengo la ujenzi wa barabara hizo, ni kuhakikisha nchi inaunganishwa kwa mtandao wa lami, kwani siku za nyuma wananchi wa Mkoa wa Kagera waliteseka kwa kusafiri umbali mrefu, kwenda Dar es Salaam.
Wakati huo wananchi hao walilazimika kupita Uganda na Kenya kwa siku tatu mpaka tano ili kufika Dar es Salaam, lakini sasa wanauwezo wa kusafiri kwa siku moja tu kutokana na barabara kutengenezwa na kupitika kwa urahisi.
Mafanikio
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, anatarajia ifikapo 2015 kilometa 18,000 za mtandao wa barabara wa Tanzania nzima zitakuwa tayari na kama itashindikana, basi zitabaki kilometa zisizozidi 2,000, ambazo zitakuwa hazijakamika lakini zitakuwa zikiendelea na ujenzi kwa hatua ya mwisho.
Naye Dk Magufuli, alisema wakati wa Uhuru 1961, nchi ilikuwa na mtandao wa barabara za lami za urefu wa kilometa 1,350, lakini katika muda wa Serikali ya Awamu ya Nne tu, chini ya uongozi wa Rais Kikwete, zimejengwa kilometa 11,154 za mtandao wa barabara kwa kiwango cha lami.
Akitoa historia ya ujenzi barabara ya Kyaka–Bugene, Dk Magufuli alisema mradi huo ulianza 2009 na mpaka kukamilika, katika muda wa miezi 27, utagharimu Sh bilioni 64.9.
Mradi huo kwa mujibu wa Dk Magufuli, unaendelea vizuri ingawa ulikumbwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo ya makandarasi wasimamizi wa mwanzo, Kampuni ya Sai kutoka nchini India kwa kushirikiana na Kampuni ya Data ya Tanzania, kufukuzwa kazi baada ya muda mfupi tangu kuanza mradi.
Alisema kuwa makandarasi hao walifukuzwa kazi, baada ya kuboronga na kushindwa kufanya kazi kama mkataba unavyoelekeza, wakati tayari walikuwa wamelipwa zaidi ya Sh bilioni moja. Kwa sasa mradi huo unasimamiwa na kikosi cha wataalamu saba kutoka Wakala wa Barabara (Tanroads) Makao Makuu.
Alionya kuwa Wizara yake haitosita kuwachukulia hatu ikiwemo kuwafukuza kazi makandarasi watakaokiuka utaratibu wa kazi, kwani Tanzania sio nchi ya watu kuja kuchota fedha.
Naye Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Makao Makuu, Alon Mfugale, alisema mradi huo wa barabara ya Kyaka –Bugene, unaojengwa na Kampuni ya China Chico kutoka nchini China, umefikia asilimia 38 ya mradi wote mpaka sasa na unagharimiwa na Serikali kwa asilimia 100.
VIA HABARI LEO

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate