EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 6, 2013

Oloya, Ngassa wavuruga usajili usiku.

USAJILI wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulifungwa usiku wa kuamkia leo Jumanne, huku Simba na Yanga zikigongana uso kwa uso kwa wachezaji wawili; Mrisho Ngassa na Moses Oloya.
Mpaka usiku saa sita usiku wakati usajili ukifungwa, hakukuwa na muafaka kati ya Simba na 
 
 Moses Oloya (kushoto) na Abel Dhaira
Yanga, kwani zote zimepeleka jina la Ngassa na zimeacha nafasi moja ya Oloya.
Simba imewasilisha majina 28 huku Yanga ikienda na majina 29 kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Simba na Yanga zimefanya mazungumzo na Oloya anayecheza klabu ya Saigon ya Vietnam ambaye mkataba wake unamalizika Oktoba lakini amewaambia atafanya uamuzi baada ya ligi ya nchi hiyo kumalizika Agosti 31.

Katika orodha ya timu hizo kila moja ina wachezaji wanne wa kigeni na wamebakiza nafasi moja ya Oloya.

Simba ina raia wa kigeni Joseph Owino na Abel Dhaira wa Uganda, Amis Tambwe na Kaze Gilbert wote wa Burundi.

Yanga ina Hamis Kiiza wa Uganda, Mbuyu Twite na Haruna Niyonzima wa Rwanda pamoja na Didier Kavumbagu wa Burundi.

Kikanuni kila klabu inaruhusiwa kusajili wachezaji watano wa kigeni, lakini Simba na Yanga kila moja imeacha nafasi moja kwa ajili ya Oloya.

Usajili wa pili utaanza Agosti 15 kwa kipindi cha mwezi mmoja na utamalizika Septemba 15 ukihusisha wachezaji huru tu, upenyo ambao kati ya Simba na Yanga zitautumia kumalizana na Oloya.

Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala aliliambia Mwanaspoti  jana Jumatatu jijini Dar es Salaam kuwa: “Tumewasilisha majina 28 ya wachezaji wetu TFF na jina la Ngassa (Mrisho) likiwemo.”

Mtawala alisema wamebakiza nafasi mbili kwenye usajili huo na nafasi moja ni ya Moses Oloya na nyingine wanaweza kuitumia kwenye usajili mwingine wa Agosti 15.

Simba inadai ina mkataba wa mwaka mmoja na Mrisho Ngassa ambaye amekanusha vikali kuhusu kauli hiyo. “Sina mkataba wowote na Simba. Nilikuwa nikicheza Simba kwa mkopo nikitokea Azam FC. Sijasaini mkataba na Simba, baada ya ule wa Azam kumalizika,” alisema Ngassa.


Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah amewahi kusema siku za nyuma kuwa: “Kama Simba wanasema wameleta mkataba wa Ngassa TFF na ukasajiliwa waambie wawaonyeshe, kwa nini wanaficha. Kwa sasa hatuwezi kusema lolote ingawa muda ukifika kila kitu kitawekwa hadharani.”

Usajili mpya wa Simba uliowasilishwa TFF ni Makipa: Abou Hashim, Andrew Ntalla na Abel Dhaira.  Mabeki: Issa Rashid, Omary Salum, Rahim Juma, Hassan Khatib, Haruna Shamte, George Owino, Gilbert Kaze na  Shomari Kapombe.

Viungo: Abdallah Seseme, William Lucian, Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Said Ndemla, Abdulhalim Humoud, na Adeyoun Saleh.

Mawinga: Mrisho Ngassa, Ramadhan Singano, Ibrahim Hussein, Haroun Athuman, Marcel Kaheza na Edward Christopher. Mastraika: Amis Tambwe, Betram Mombeki na Sino Agustino

Usajili wa Yanga ni: makipa;  Ally Mustapha, Deogratius Munishi na Yusuph Abdul.
Mabeki: Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub, Kelvin Yondan, Juma Abdul, Oscar Joshua, Rajabu Zahir, Ibrahim Job na Issa Ngao.
Viungo: Athuman Idd, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Salum Telela, Hamis Thabit na Bakari Masoud.
Mawinga: Nizar Khalfan, Mrisho Ngassa, Simon Msuva, Abdallah Mguhi na Reliant Lusajo. Mastraika: Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza, Jerry Tegete, Hussein Javu, Shaban Kondo na Said Bahanuzi.
Kuna vita mbili kubwa zinakuja mbele kwa Simba na Yanga, nayo ni nani atampa Ngassa na nani atamkosa Oloya.
Credit: MWANASPORTS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate