EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 7, 2013

Simba SC yakabidhiwa fedha za Mwinyi Kazimoto.


Mwakilishi wa Kamati ya Usajili ya Simba, Hans Pope (kushoto) akiwa na Mwakilishi wa Al-Markhiya Sports Club, Saleh Afif wakati akisaini fomu za usajili wa Mwinyi Kazimoto.


KLABU ya Simba imemuuza kiungo wake mshambuliaji, Mwinyi Kazimoto, katika timu ya Al-Markhiya Sports Club ya Qatar kwa dau la dola 50,000 (zaidi ya shilingi milioni 81) ambazo zaidi ya nusu zimeshakabidhiwa.

Kiungo huyo, hivi karibuni alitimkia huko kwa ajili ya kufanya majaribio kabla ya kusajiliwa na timu hiyo.

Akizungumza na Championi Jumatano katika makabidhiano ya fedha hizo, Mwakilishi wa Al-Markhiya Sports Club, Saleh Afif, alisema wametanguliza dola 35,000 (shilingi milioni 57).

Afif alisema fedha nyingine ambazo ni dola 15,000 (zaidi ya shilingi milioni 24) watazilipa mwishoni mwa Desemba, mwaka huu.

Alisema staa huyo akiwa kwenye timu hiyo, anatarajiwa kulipwa mshahara wa dola 7,000 (zaidi ya shilingi milioni 11).

Mwakilishi huyo alisema kiungo huyo amesaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuichezea timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Pili nchini huko.

“Kazimoto amesaini kuichezea Al-Markhiya Sports Club ya Qatar kwa dau la dola 50,000 ambazo sehemu yake  tayari leo (Jumatatu) tumezikabidhi kwa mwenyekiti wao wa usajili, Hans Pope.

“Tumetanguliza fedha nyingine ambapo dola 15,000 tutazilipa mwishoni mwa Desemba, mwaka huu.  Akiwa kwenye timu hiyo anatarajiwa kulipwa mshahara wa dola 7,000,” alisema Afif.

Naye Hans Pope baada ya makabidhiano alisema kuwa wamemruhusu kiungo huyo kwenda kuichezea timu hiyo.

Hans Pope alisema hawawezi kumzuia kiungo huyo kwenda kucheza soka nje ya nchi, pia ameitaka timu hiyo kutorudia kitendo walichokifanya cha kumtorosha kambini Kazimoto na kumpeleka huko Qatar kwenye majaribio.

“Sisi hatuwezi kumzuia mchezaji yeyote kwenda kucheza soka nje ya nchi, kikubwa kinachotakiwa ni timu kufuata taratibu na siyo mlivyofanya kwa Kazimoto, kumtorosha kwenye kambi ya Stars na kumpeleka huko Qatar kwenye majaribio,” alisema Hans Pope.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate