EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, September 28, 2013

Bodi yatangaza wanafunzi waliopata mikopo katika mwaka wa masomo 2013/2014.

SERIKALI imetangaza kuwapatia mikopo wanafunzi wa elimu ya juu 29,754 kati ya wanafunzi 31,647 katika mwaka wa masomo 2013/2014.


Mkurugenzi wa Habari, Elimu na Mawasiliano, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa, alieleza hayo jijini Dar es Salaam jana alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu utaratibu wa utoaji wa mikopo hiyo kwa wanafunzi wapya na wanaoendelea na elimu ya juu.

Alisema uchambuzi wa maombi ya mikopo kwa mwaka huu wa masomo umekamilika na kwamba lengo la serikali ni kuwawezesha wanafunzi wa elimu ya juu kupata fedha kwa muda muafaka.

Alisema kuwa mchanganuo wa utuoaji wa mikopo hiyo ulizingatia vigezo na masharti ya uombaji mikopo na ruzuku.

Alisema idadi ya waombaji wapya waliotuma maombi yalikuwa 53,239, waombaji wanaoendelea na masomo 43,032, waombaji waliokuwa na maombi yenye matatizo ni 6,364.

“Wengine ni waombaji waliorekebisha matatizo kwenye maombi yao 3,151 na waombaji ambao hawakurekebisha matatizo kwenye maombi yao 3,213,” alisema.

Akifafanua zaidi kuhusu mchanganuo huo alisema waombaji wapya 53,630 watakaosoma  ndani na nje ya nchi wamepata mikopo hiyo.

Alisema maombi ya mikopo kwa wanafunzi wanaoendelea 61,692 ambao wanasoma ndani na nje ya nchi wamepangiwa kupata mikopo hiyo.


Mkurugenzi  huyo alisema bodi ya mikopo ya elimu ya juu inatarajia kutoa mikopo ya sh bilioni 306 kwa ajili ya ukopeshaji wanafunzi wapya na wanaoendelea na masomo.

Alisema mchakato wa upangaji wa mikopo unaendelea vizuri na kwamba hadi sasa umekamilika kwa zaidi ya asilimia 90.

“Matarajio ni kukamilisha mchakato huu kwa asilimia 100 ifikapo wiki ya kwanza ya Oktoba kabla ya vyuo vya elimu ya juu kufunguliwa, kwa mujibu wa Tume ya Vyuo Vikuu,” alisema.

Alieleza kuwa orodha kamili ya waombaji wapya waliopangiwa mikopo inapatikana kwenye tovuti ya bodi hiyo www.heslb.go.tz ambapo mwombaji anaweza kutafuta jina lake kwa kutumia namba ya mtihani ya kidato cha nne.

Alisisitiza kuwa taratibu za kupeleka mikopo yao vyuoni zinaendelea na kwamba watalipwa baada ya kufanya usajili.

Aidha alisisitiza umuhimu wa kila mwombaji kuwa na akaunti ya benki kwa ajili ya kupitishia mikopo hiyo.
Aliongeza kusema kuwa waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo wanawajibika kurejesha mikopo hiyo baada ya kuhitimu masomo yao.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate