
Mrisho
 Ngassa (katikati) akionyesha risti ya malipo aliyopewa TFF baada ya 
kulipa deni la mil 45, kushoto kwake ni mhasibu wa Yanga, Rose Msamila 
na kulia ni Afisa Habari wa Yanga Baraka Kizuguto
Kiungo 
mshambuliaji wa timu ya Young Africans Mrisho Khlafani Ngassa leo 
amelipa jumla ya mil 45, deni la mil 30 pamoja na faini ya mil 15 za 
klabu ya Simba SC kwa Shirikisho la Soka nchini TFF ili aweze kuitumikia
 timu yake kuanzia kesho.
Ngassa ambaye aliambatana na viongozi wa klabu ya Yanga mjumbe wa 
sekretariat Partick Naggi, Afisa Habari Baraka Kizuguto na mhasibu Rose 
Msamila alikabidhi hundi za malipo kwa idara ya fedha ya shirikisho 
hilo.
Mara baada ya kukabidhi hundi hiyo Ngassa aliongea na 
waandishi wa habari nje ya ofisi za TFF na kusema ameamua kulilipa deni 
hilo ili aweze kuitumikia klabu yake, kwani kukosa michezo sita 
kumemnyima fursa ya kuisaidia timu yake.
Naomba mnielewe hizi 
fedha nimezitoa mimi mwenyewe kwenye akiba yangu iliyopo bank, hivyo 
kama kuna mtu yoyote ataguswa na hili suala anaweza kuwasiliana na mimi 
katika kujaribu kunichangia juu ya hili.
Aidha Ngasaa amesema kwa 
sasa akili yake yote ipo kwenye michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom na lengo 
lake ni kuhakikisha anaisadia timu yake kufanya vizuri n akupata ushindi
 katika kila mchezo watakaocheza.
Kocha Ernie Brandts kwa sasa ana
 fursa ya kumtumia mchezaji Mrisho Ngasa kwa kuanzia kwa mchezo wa kesho
 kutokana na kuwa amekamilisha kila kitu.
Naye Afisa Habari wa 
Yanga Baraka Kizuguto amewaomba wapenzi, washabiki na wanachama 
kujitokeza kwa wingi kesho uwanja wa Taifa kuja kuishangilia timu yao 
itakapokua ikicheza na maafande wa Ruvu Shooting.
Young Africans itacheza na Ruvu Shooting katika uwanja wa Taifa majira ya saa 10:00 kwa saa za Afrika Mashariki. 
CHANZO NI BIN ZUBEIRY
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment