EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, October 4, 2014

UTAPELI MZITO: WABONGO WALIZWA 'MIKOPO YA OBAMA, JK'

 
Stori: Harun Sanchawa na Hamida Hassan
Utapeli mzito umeshamiri Bongo ambapo imebainika kuna taasisi iliyojipachika jina la Tanzania Loan Society inayojieleza kuwa inafadhiliwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wa Serikali ya Marekani huku ikiwarubuni watu kuwa inatoa mikopo bila riba.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Mrisho Kikwete.
Ipo kimtandao zaidi
Taasisi hiyo iliyoanzishwa muda mrefu ikapotea, sasa imeibuka upya na inawaliza wengi ambapo inaendesha shughuli zake kimtandao na wahusika hutumia utundu kuingilia mawasiliano katika akaunti za watu katika facebook na kuweka ushuhuda kuwa wamiliki wamefanikiwa kupata mkopo bila riba tena kwa masharti rahisi.

Mtandao umegundulikaje?
Mmoja wa wasomaji wa gazeti hili aliyefahamika kwa jina la Lulu, hivi karibuni alileta malalamiko yake akieleza jinsi wahusika wa utapeli huo walivyoingilia mawasiliano yake ya Facebook, wakamlisha maneno kuwa aliomba mkopo wa shilingi milioni 3 baada ya kutoa shilingi 95,000 kwa ajili ya uanachama na akapewa fasta.
Kwenye ukurasa wa Facebook wa Lulu, kulikuwa na maelezo ya kupika kuwa, Tanzania Loan Society ni taasisi iliyo chini ya Rais Jakaya Kikwete kwa msaada wa Rais wa Marekani Barack Obama huku watendaji wakuu wakiwa ni Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda na Mbunge wa Chalinze, Mhe.
Ridhiwani Kikwete.
Ikadaiwa eti muweka hazina wa taasisi hiyo ni Zainabu Kikwete huku namba zake za simu zikitajwa kuwa ni 0767 602 518  na 0713 009 819, lengo la mpango huo likiwa ni kuhakikisha Watanzania wanaondokana na umaskini kwa kupewa mikopo kwa masharti nafuu.
Chini ya maelezo hayo kuna linki ya kuingia kwenye mtandao wa taasisi hiyo feki (ambapo ukiufungua unakuta nembo ya serikali ya Tanzania na maelezo yanayomshawishi mtu yeyote kuamini kuwa siyo ishu ya kitapeli.
Kinachomsukuma mtu kuingia mtegoni ni kwamba, kwanza wanahusishwa viongozi wakubwa, pili matapeli hao wanaeleza kuwa makao makuu ya taasisi hiyo ni Posta jijini Dar kwenye jengo la Utumishi, ghorofa ya 5, chumba namba 30 na anayehitaji mkopo kuanzia laki moja hadi milioni 50 anatuma 95,000 kupitia namba za muweka hazina (Zainabu Kikwete feki).
Risasi laingia kazini
Baada ya kupatikana kwa taarifa hizo, Septemba 28, mwaka huu, waandishi walianza uchunguzi kwa kuthibitisha kama namba za Zainabu zimesajiwa kwa jina gani ambapo ilionekana imesajiliwa kwa jina la Zainabu Kikwete.
Kisha mwandishi wetu alimpigia Zainabu, alipopokea na kuulizwa kuhusiana na taasisi hiyo alisema ni kweli ipo na maelezo yote yapo kwenye mtandao wao huku akimsisitiza mwandishi kutuma pesa ili atumiwe mkopo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa Rais Barack Obama wa Marekani .
Waandishi watinga Jengo la Utumishi
Baada ya kujiridhisha, waandishi wetu walimpigia tena Zainabu na kumtaarifu kuwa wapo njiani kuelekea ofisini kwao, kwa kujiamini alisema hakuna shida na kama ni mkopo upo unawasubiria.
Baada ya waandishi wetu kufika kwenye jengo la Utumishi, walimpigia tena simu Zainabu kumjulisha kuwa wameshafika ambapo alidai wametoka kidogo ofisini (eti wameenda kukusanya madeni sugu) na kwamba wakutane kesho yake.
Waandishi wetu wakiwa nje ya jengo hilo, waliongea na mmoja wa walinzi na kumuuliza juu ya uwepo wa taasisi hiyo ambapo alieleza kuwa, haipo na wengi wamekuwa wakifika hapo baada ya kutapeliwa.
Ili kupata taarifa rasmi, waandishi walifika kwenye ofisi ya mmoja wa maafisa habari wa Ofisi ya Rais, Menejimenti na Utumishi wa Umma, Florence Laurence ambaye alikiri taasisi hiyo ya kitapeli kuhusisha jengo lao na walishatoa tahadhari kwa wananchi.
Msako wafanyika
Licha ya majibu yaliyotolewa na afisa habari huyo, waandishi wetu walifika katika Ofisi ya Polisi, Kanda Maalum ya Dar, Kitengo cha Intelijensi na kutoa taarifa ambapo walichukua taarifa kuhusiana na mtandao huo na kuahidi kudili nao.
Septemba 30, mwaka huu ofisi hiyo ilitoa polisi wawili ambao waliongozana na waandishi wetu mpaka katika jengo la Utumishi na mhusika alipopigiwa simu alidai siku hiyo pia walikuwa bize kukusanya madeni sugu na kwamba waende tena kesho yake.
Kutokana na kuchengachenga kwa wahusika, polisi walishauri waachwe wafanye kazi yao na kwamba kwa mbinu zao za kiintelijensia watawanasa wahusika. Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa, mtandao huu umewaliza wengi hivyo ni vyema watu wakawa makini.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate