EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 2, 2014

MAMA RWAKATARE AFIKISHWA POLISI


MCHUNGAJI Kiongozi wa Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God jijini Dar, Dk. Getrude Rwakatare (pichani) amefunguliwa mashitaka katika Kituo cha Polisi Wazo Hill kwa uharibifu wa mali inayodaiwa ina thamani ya shilingi milioni 20.
Bw. Grayson Justine anayelalamika kuvunjiwa nyumba yake na Mch. Getrude Rwakatare.
Taarifa zilizopatikana katika kituo hicho zenye Jalada la Kumbukumbu WH/RB/9029/2014 UHARIBIFU WA MALI na kuthibitishwa na mlalamikaji aliyejitambulisha kwa jina la Grayson Justine, zinaeleza mchungaji huyo alivunja nyumba ya Grayson kwa greda hali iliyomfanya mmiliki huyo kuzimia na kulazwa Zahanati ya Mico iliyopo Wazo Hill baada ya presha kupanda.
Katika mahojiano na waandishi wetu katika Ofisi za Global Publishers, Bamaga- Mwenge, Dar wiki iliyopita, Grayson alikuwa na haya ya kusema:
“Kiwanja nilichojengea nyumba nilikinunua kwa Jumanne Rajab, Agosti 24, 2011 na makubaliano yalifanyika kwa kuandikishiana Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju ‘B’ na kila mmoja alikuwa na mashahidi wake.
Nyumba ya Bw. Grayson Justine iliyobomolewa kwa greda.
“Kutokana na kuchoka katika kupangisha, niliamua kuchukua mkopo wa shilingi milioni 20 kazini ili nijenge haraka na kuhamia, ujenzi ulianza Septemba 21,  mwaka 2013 mpaka kufikia mwezi huu (Novemba) nilibakiza kupaua na nilitarajia kuhamia mwanzoni mwa mwaka kesho.

“Baadaye nilikwenda Moshi kwenye msiba wa baba, niliporudi Dar nilimaliza siku moja tu, nikaripoti kazini. Nikiwa kazini Novemba 11, mwaka huu nikapigiwa simu na jirani kwamba nyumba yangu inabomolewa na greda, alifikiri kwamba nimeshaonana na Mchungaji Rwakatare na kukubaliana naye.
“Nilikwenda kule, kufika nikakuta hakuna jengo! Nilidondoka chini, sikujua kilichoendelea, nilipoteza fahamu, nilijitambua nikiwa Zahanati ya Mico.
“Kinachoniumiza sana ni kitendo cha kuvunjiwa nyumba yangu bila kushirikishwa, bora hata angenifungulia mashitaka kama anaona nilivamia kikwanja chake.”
“Yeye ana uwezo, ana ghorofa ya zaidi ya shilingi bilioni moja iweje anionee na kunivunjia mimi maskini niliyejenga kwa fedha za mkopo?
Mch. Getrude Rwakatare.
“Kituo cha polisi nilifika karibu mara nne lakini mpaka leo hii sijapewa mpelelezi wala hawajafika eneo la tukio, nataka sheria ichukue mkondo wake.”
Mwandishi alifika katika eneo la tukio na kushuhudia kifusi kinachodaiwa kuwa ni iliyokuwa nyumba ya Grayson iliyovunjwa na imezungushiwa ukuta na geti kupigwa kufuli.
Hata hivyo, Uwazi lilifika katika Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju ‘B’ na kuonana na mtendaji Abdallah Mkeyenge ambaye alikiri kuwepo kwa mvutano baina ya watu hao.“Hii barua ya makubaliano ya kuuziwa Grayson kiwanja inaonekana imetoka ofisini hapa lakini mimi kipindi hicho nilikuwa sijahamia ofisi hii.Jumba la kifahari la Mch. Getrude Rwakatare.
“Ninachokumbuka kuna kipindi Mchungaji Rwakatare alikuja na milioni tano kuwapa Grayson na mtu mwingine yaani kuwapoza lakini walikataa kuzichukua,” alisema mtendaji huyo.
Mchungaji Rwakatare alipopigiwa simu kuhusiana na madai hayo alisema yupo bungeni hivyo alimwagiza msaidizi wake, Jerad Abeid kuzungumzia sakata hilo ambapo alisema eneo hilo mchungaji analimiliki  tangu mwaka 2005 na hati ziko ardhi Wilaya ya Kinondoni. Alibomoa nyumba ya Grayson akijua ni eneo lake la siku nyingi.
“Unajua katika maeneo hayo kuna watu walikuwa wakishirikiana na ofisi za mtaa kuuza kiwanja cha mchungaji kwa siri na tayari watu wanne walishauziwa lakini walikuwa hawajajenga,  mchungaji aliamua kuwapoza kiubinadamu na wameshaondoka bado watu wawili akiwemo huyo Grayson,” alisema Jerad.
CHANZO:GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate